GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,548
- 108,882
Ikitokea GENTAMYCINE nagombea Uchaguzi wowote ule halafu Matokeo yakitoka naambiwa nimeshinda kwa Kishindo ( 100% ) upesi sana nitayakataa na kutaka Uchaguzi urejewe upya.
Ila ikitokea GENTAMYCINE nagombea Uchaguzi wowote ule kisha Matokeo yakatangazwa nimeshinda kwa 65% nitayapokea kwa Furaha zaidi kwakuwa nitajua Demokrasia ya Kweli na isiyo na chembe ya Unafiki imefanyika na Ushindi wangu huo ni wa halali kabisa
Kiongozi anayeshinda Uchaguzi kwa 100% Votes huwa anakuwa ameshalemazwa Kifikra, anafanywa Zwazwa fulani, anasanifiwa, hatokuwa na jipya na huenda hata hao waliompigia Kura hizo wakati wanampa ( wanampigia ) Rohoni Kwao / Mioyoni Mwao walikuwa Wakimzomea na Kumcheka kwa Kumdharau wakijua hana ( hatokuwa ) na jipya lolote Kwao.
Kiongozi anayeshinda Uchaguzi kwa 65% Votes Kwanza atakuwa na Adabu, ataongoza kwa Umakini, hatopenda Kuharibu, ataharakisha Maendeleo, ataheshimu zaidi Demokrasia na ataamini kuwa ana Changamoto nyingi za Kuzikabili ili aweze kwenda sawa na wale 35% waliomkataa katika Sanduku la Kura.
GENTAMYCINE namalizia kwa Kuwasisitiza Wanasiasa wa Tanzania kuwa kamwe msipende Kushinda Ushindi wa Kishindo ( 100% Votes ) kwani mnakuwa Mmechaguliwa tu Kinafiki na Kiuwoga zaidi pengine kutokana na Nafasi ( Nyadhifa ) ila Kiuhalisia mnakuwa si pendekezo lao.
Na hata Demokrasia ya Kweli inakuwa haipo kwani katika Falsafa za Kiuongozi kwa Watu wanaojitambua ( wenye Akili sawa sawa ) wanaamini kuwa hakuna Binadamu asiyekuwa na Mapungufu ( aliyekamilika ) hivyo kutokea Kundi la Watu Kukupinga ndiyo takwa halisi la Kiafya ndani ya Demokrasia ya uhakika ( ya kweli )
Naomba niishie zangu tu hapa niwaacheni mkishangilia Ushindi wenu wa Kishindo ( 100% Votes ) huku GENTAMYCINE nikiendelea zangu tu Kununa ( Kukasirika ) kwa Upuuzi uliofanywa na Mwamuzi ( Referee ) wa leo huko Nelson Mandela Stadium kwa Kuinyima Penati ya halali ( haki ) kabisa Prisons FC dhidi ya Yanga SC.
Ila ikitokea GENTAMYCINE nagombea Uchaguzi wowote ule kisha Matokeo yakatangazwa nimeshinda kwa 65% nitayapokea kwa Furaha zaidi kwakuwa nitajua Demokrasia ya Kweli na isiyo na chembe ya Unafiki imefanyika na Ushindi wangu huo ni wa halali kabisa
Kiongozi anayeshinda Uchaguzi kwa 100% Votes huwa anakuwa ameshalemazwa Kifikra, anafanywa Zwazwa fulani, anasanifiwa, hatokuwa na jipya na huenda hata hao waliompigia Kura hizo wakati wanampa ( wanampigia ) Rohoni Kwao / Mioyoni Mwao walikuwa Wakimzomea na Kumcheka kwa Kumdharau wakijua hana ( hatokuwa ) na jipya lolote Kwao.
Kiongozi anayeshinda Uchaguzi kwa 65% Votes Kwanza atakuwa na Adabu, ataongoza kwa Umakini, hatopenda Kuharibu, ataharakisha Maendeleo, ataheshimu zaidi Demokrasia na ataamini kuwa ana Changamoto nyingi za Kuzikabili ili aweze kwenda sawa na wale 35% waliomkataa katika Sanduku la Kura.
GENTAMYCINE namalizia kwa Kuwasisitiza Wanasiasa wa Tanzania kuwa kamwe msipende Kushinda Ushindi wa Kishindo ( 100% Votes ) kwani mnakuwa Mmechaguliwa tu Kinafiki na Kiuwoga zaidi pengine kutokana na Nafasi ( Nyadhifa ) ila Kiuhalisia mnakuwa si pendekezo lao.
Na hata Demokrasia ya Kweli inakuwa haipo kwani katika Falsafa za Kiuongozi kwa Watu wanaojitambua ( wenye Akili sawa sawa ) wanaamini kuwa hakuna Binadamu asiyekuwa na Mapungufu ( aliyekamilika ) hivyo kutokea Kundi la Watu Kukupinga ndiyo takwa halisi la Kiafya ndani ya Demokrasia ya uhakika ( ya kweli )
Naomba niishie zangu tu hapa niwaacheni mkishangilia Ushindi wenu wa Kishindo ( 100% Votes ) huku GENTAMYCINE nikiendelea zangu tu Kununa ( Kukasirika ) kwa Upuuzi uliofanywa na Mwamuzi ( Referee ) wa leo huko Nelson Mandela Stadium kwa Kuinyima Penati ya halali ( haki ) kabisa Prisons FC dhidi ya Yanga SC.