Wanashikiliwa kwa kumkashfu mtume

Wanashikiliwa kwa kumkashfu mtume

Taarifa ya habari star tv. Kuna watu wawili wanashikiliwa na polisi zanzibar kwa kosa la kumkashfu mtume kupitia mitandao ya kijamii...!
Polisi wanasema watuhumiwa wanao na upelelezi unaendelea na watafikishwa mahakamani.. Ninatamani watu walio znzbr watupe ufafanuzi zaidi katika hili jambo.

Mkuu hawa watu wanashinda kesi vizuri kabisa...

Sijui kama katiba ya Zanzibar au bara inatambua neno mtume...na sijui kama mtume ni raia wa Zanzibar kiasi kwamba juridiction za zanzbar ina-muiclude....

Sio vizuri kutukana anyone dead or alive,ila concept nzima ya hayo matusi hatujayajua bado,i wish ningekua mahakamani nione mabishano yatakavyokua
 
Na hapo ndiyo tatizo.

Naongelea kufa kwa sababu wote tunakubaliana kuwa sifa moja ya mungu ni kuwa hafi,sasa kuzungumzia kufufuka kama ndiyo uthibitisho wa Yesu ni Mungu...Je vp na Yesu aliposema haijui siku ya mwisho ikiwa Yesu alikuwa na uungu?

Kama Yesu aliweza kufufuka kwa sababu alikuwa na uungu basi angekuwa anajua na siku ya mwisho pia kwa sababu ni Mungu.

Labda tuseme kwamba Yesu alifufuliwa na Mungu.

Yesu ni Mungu.
Unachotakiwa uelewe ni kwamba Yesu alipochukua umbo na kuja duniani alitenda kama binadamu.
Maajabu yote aliyoyafanya na aliyoyatenda aliyatenda kama mafundisho kwamba binadamu yoyote anayeamini anaweza kutenda.
Mambo mengine aliamua kuyaacha kwa sababu hayamfai binadamu kwa kipindi husika.
 
Mkuu umeingia kwenye vitabu, hivi umeelewa hoja yangu kwanza?
hoja yako niliiekewa ila nimeandika hizo vesi kutokana na na post hizi
Kwahiyo hapo mkuu atakuwa amekusudia kuuwa mtu ndio maana kaweka mtego. Lakini navyojua mimi ni kwamba Mungu ni mwenye upendo na haki.

Umewaza vyema. Kwa hoja yako hiyo hiyo uliyotoa ni kwamba kutokana na Mungu kuwa na nguvu, uwezo na mamlaka basi kulikuwa hakuna sababu ya kutambua hizi dini kupitia biashara za utumwa na movements mbali mbali za kueneza dini. Mungu angetuumba katika akili ya kufuata msimamo sahihi autakao yeye Mungu. Angeondoa hii hali ya ubishani na kutuweka katika umoja maana yeye ndiye mwenye nguvu na uwezo.

Soma mwanzo 1:16-17 utaelewa fasili ya hoja yangu hapo juu
 
hoja yako niliiekewa ila nimeandika hizo vesi kutokana na na post hizi
Hapo hakuna ulichonijibu kwa andiko lako. Mwanzo 1:16-17

Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.

17 Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi
 
Taarifa ya habari star tv. Kuna watu wawili wanashikiliwa na polisi zanzibar kwa kosa la kumkashfu mtume kupitia mitandao ya kijamii...!
Polisi wanasema watuhumiwa wanao na upelelezi unaendelea na watafikishwa mahakamani.. Ninatamani watu walio znzbr watupe ufafanuzi zaidi katika hili jambo.
Nenda youtube andika Dr abdallah amkashifu mtume. Utyakayosikia huwezi msimulia mtu.
 
Yesu ni Mungu.
Unachotakiwa uelewe ni kwamba Yesu alipochukua umbo na kuja duniani alitenda kama binadamu.
Maajabu yote aliyoyafanya na aliyoyatenda aliyatenda kama mafundisho kwamba binadamu yoyote anayeamini anaweza kutenda.
Mambo mengine aliamua kuyaacha kwa sababu hayamfai binadamu kwa kipindi husika.
Suala la Yesu kuwa ni Mungu itabaki kuwa ni imani na sitaweza kukulazimisha usiamini hivyo naheshimu tu imani yako.

Ila imekosekana dalili ya uungu wa Yesu,bado hili suala ni tata.
 
Yesu ni Mungu.
Unachotakiwa uelewe ni kwamba Yesu alipochukua umbo na kuja duniani alitenda kama binadamu.
Maajabu yote aliyoyafanya na aliyoyatenda aliyatenda kama mafundisho kwamba binadamu yoyote anayeamini anaweza kutenda.
Mambo mengine aliamua kuyaacha kwa sababu hayamfai binadamu kwa kipindi husika.
Farudume, kama Yesu ni mungu siwezi bishia imani yako ila ni wazi kulingana na biblia kuna Mungu mwengine aliyekuwa anamuongoza yesu hivyo basi Yesu ana Mungu wake ila wewe pia umemfanya yesu kuwa Mungu.

1. Yesu unasema kuwa ni Mungu alikuja duniani akauvaa ubinadamu je yesu alipokuwa duniani alikuwa tegemezi kwa mwingine mbinguni? au au alikuwa yeye yesu wa duniani anafanya kila kitu? Rejea wakati yesu anataka kufa, je alimuomba nani amuepushe na kikombe?

Yohana 5:37-38
Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.

38 Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.
 
Eti???? We unaona kosa dogo?? Kwa sehemu kama zanzibar 98% muslims afu useme sio haki..?? kwa Zanzibar ni kawaida na sio tu utashikiliwa na polisi hata Raia wake ama awe CUF au CCM watakufanya kitu mbaya....
Kwa hiyo wakiwa huko Zanzibar ni ruksa kumkashifu Yesu kwa sababu 2% tu ni wakristo?
 
Ila sometimes allah anachekeshaga.

Mfano pale pa kuwataka waumin kujiua kisha akakutunuku barka zake


Si kweli, dini haijawahi amrisha hivi. Usilo lielewa na sawa na usiku wa giza....Jinsi Christian wanavyoelewa uislam vibaya ndivyo baadhi ya Muslim wanavyouelewa ukristu vibaya. Ni sawa na aliyesoma kitabu cha Chemistry basi kwa kuwa hajasoma kitabu cha Biology atapiga na kusema hata asiyeyajua kwa kufuata maneno ya uongo ya kusikia. Ili kuweza zifahamu dini hizi ingia chimbo, soma vitabu vya dini kisha ponda hoja au tetea hoja.

Usipende ya kusikia Yupo christian kwa kuwa hapendi sheria fulani za christian japo yeye ni christian akaponda sheria hizo kwaajili tu ya kutaka kutekeleza maovu yake, au kwa kutokuijua dini yake, Na yupo Muslim ambaye Japo ni Muslim akawa hapendi sheria za kiislam kwa kisa tu ni kutaka kutekeleza maovu yake, basi akawa anafanya yake maovu na kusema kuwa yameamrishwa na Uislam. Binadamu ndivyo tulivyo. Hata kama mtu anajua dini lakini tukumbuke sisi ni wadhaifu na tunamadhambi ndivyo tulivyoumbwa....Usimuamini soma maarisho mwenyewe...

Ukitaka kujua hayo baadhi ya waislam wengine wanayoyatenda kwa kisingizio cha dini imeagiza pia kama ni mvivu wa kusoma basi angalia na kusikiliza Iqraa TV...HII INATOA MAWAIDHA KINGEREZA HAKIKA UTAELEWA VIZURI SANAA.

Mimi kwa upande wangu naheshimu sanaa dini zote, Issa/Yesu namtukuza sana na Muhammad namtukuza sana..
 
Suala la Yesu kuwa ni Mungu itabaki kuwa ni imani na sitaweza kukulazimisha usiamini hivyo naheshimu tu imani yako.

Ila imekosekana dalili ya uungu wa Yesu,bado hili suala ni tata.

Kama ulivyosema Imani hailazimishwi.Ni swala la kueleweshana,usipoelewa siku ya mwisho ndio hukumu itaamua.
Kwa Mtu yeyote anayesoma biblia na kuiamini,Kutoka kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo YESU KRISTO anaongelewa kama MUNGU na sio tofauti.
 
Si kweli, dini haijawahi amrisha hivi. Usilo lielewa na sawa na usiku wa giza....Jinsi Christian wanavyoelewa uislam vibaya ndivyo baadhi ya Muslim wanavyouelewa ukristu vibaya. Ni sawa na aliyesoma kitabu cha Chemistry basi kwa kuwa hajasoma kitabu cha Biology atapiga na kusema hata asiyeyajua kwa kufuata maneno ya uongo ya kusikia. Ili kuweza zifahamu dini hizi ingia chimbo, soma vitabu vya dini kisha ponda hoja au tetea hoja.

Usipende ya kusikia Yupo christian kwa kuwa hapendi sheria fulani za christian japo yeye ni christian akaponda sheria hizo kwaajili tu ya kutaka kutekeleza maovu yake, au kwa kutokuijua dini yake, Na yupo Muslim ambaye Japo ni Muslim akawa hapendi sheria za kiislam kwa kisa tu ni kutaka kutekeleza maovu yake, basi akawa anafanya yake maovu na kusema kuwa yameamrishwa na Uislam. Binadamu ndivyo tulivyo. Hata kama mtu anajua dini lakini tukumbuke sisi ni wadhaifu na tunamadhambi ndivyo tulivyoumbwa....Usimuamini soma maarisho mwenyewe...

Ukitaka kujua hayo baadhi ya waislam wengine wanayoyatenda kwa kisingizio cha dini imeagiza pia kama ni mvivu wa kusoma basi angalia na kusikiliza Iqraa TV...HII INATOA MAWAIDHA KINGEREZA HAKIKA UTAELEWA VIZURI SANAA.

Mimi kwa upande wangu naheshimu sanaa dini zote, Issa/Yesu namtukuza sana na Muhammad namtukuza sana..
Mkuu naheshimu sana Dini ya Kiislam na two of my best friends ni Muslims

Ninajua baadhi ya maandiko yaliyopo katika qur'an na yanafundisha mema kbs.

Ninachowapingaga hawa waislam hewa hapa ni unakuta anasimamia kitu ambacho hakijui effectively na hata kukitetea kimaandiko hajui isipokuwa kulalamika na kuuponda Ukristo.

Have peace mkuu.
 
samahani mwanzo 2:16-17
Ndio maana nilikuuliza je kusudio lake ni kuua? Mungu anasifa ya kujua yasasa na yajayo. Sasa kama ulivyosema mwanzoni kwamba uweke chupa za soda kadhaa halafu chupa moja uweke sumu kati ya chupa hizo za soda halafu umwambie mtu anywe soda ila chupa moja inasumu. Je lengo la kuweka hiyo chupa yenye sumu ni nini? Kama sio kumtega mtu?
 
Farudume, kama Yesu ni mungu siwezi bishia imani yako ila ni wazi kulingana na biblia kuna Mungu mwengine aliyekuwa anamuongoza yesu hivyo basi Yesu ana Mungu wake ila wewe pia umemfanya yesu kuwa Mungu.

1. Yesu unasema kuwa ni Mungu alikuja duniani akauvaa ubinadamu je yesu alipokuwa duniani alikuwa tegemezi kwa mwingine mbinguni? au au alikuwa yeye yesu wa duniani anafanya kila kitu? Rejea wakati yesu anataka kufa, je alimuomba nani amuepushe na kikombe?

Yohana 5:37-38
Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.

38 Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.
Mkuu Yesu ni Mungu kwani Mungu tangu anaumba ulimwengu aliweja dhahiri uwepo wa nafsi zake 3 aliposema

"Na tumfanye mtu kwa mfano wetu"

Nilishaeleza tena kwanini Yesu Kristo alikuja duniani kama Mwanadamu.
 
Farudume, kama Yesu ni mungu siwezi bishia imani yako ila ni wazi kulingana na biblia kuna Mungu mwengine aliyekuwa anamuongoza yesu hivyo basi Yesu ana Mungu wake ila wewe pia umemfanya yesu kuwa Mungu.

1. Yesu unasema kuwa ni Mungu alikuja duniani akauvaa ubinadamu je yesu alipokuwa duniani alikuwa tegemezi kwa mwingine mbinguni? au au alikuwa yeye yesu wa duniani anafanya kila kitu? Rejea wakati yesu anataka kufa, je alimuomba nani amuepushe na kikombe?

Yohana 5:37-38
Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.

38 Wala neno lake hamnalo likikaa ndani yenu, kwa kuwa ninyi hammwamini yule aliyetumwa na yeye.

Yesu ni nafsi ya Pili ya Mungu.Mungu ana nafsi tatu yaani BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU.Hutamkwa UTATU MTAKATIFU,MUNGU MMOJA.
Nafsi zote zinategemeana na kwa pamoja ndio zinatengeneza UMUNGU yaani MUNGU MMOJA.

Umejaribu kunukuu vifungu vya Biblia Takatifu.Ni jambo jema ila ni vizuri uiamini.Nipo tayari kukupa vifungu vingi zaidi kama unaiamini Biblia.
 
Mkuu Yesu ni Mungu kwani Mungu tangu anaumba ulimwengu aliweja dhahiri uwepo wa nafsi zake 3 aliposema

"Na tumfanye mtu kwa mfano wetu"

Nilishaeleza tena kwanini Yesu Kristo alikuja duniani kama Mwanadamu.
Mkuu embu nipe andiko Mungu akisema ana nafsi tatu. Nafsi tatu hiyo dhana tu ya uelewaji wa maandiko lakini hakuna andiko linalosema kuwa Mungu ana nafsi tatu.

Marko 12:28-30

Na mmojawapo wa waandishi akafika, akawasikia wakisemezana naye, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?

29 Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote
 
Mkuu naheshimu sana Dini ya Kiislam na two of my best friends ni Muslims

Ninajua baadhi ya maandiko yaliyopo katika qur'an na yanafundisha mema kbs.

Ninachowapingaga hawa waislam hewa hapa ni unakuta anasimamia kitu ambacho hakijui effectively na hata kukitetea kimaandiko hajui isipokuwa kulalamika na kuuponda Ukristo.

Have peace mkuu.


Kweli baadhi yao wanakuwa ni hewa kweli,
Kwanza haipaswi kuponda Ukristo wala kumtukana mkristo...siku moja nilisikiliza mawaidha IQRA TV sheikh akasema, sisi binadamu tunakosea, akataja baadhi ya maandiko kuwa,
Hatupaswi kumchukia mtu kwa tabia yake wala matendo yake au dini ya mwenzio bali Tunapaswa kumuweka karibu, kumpenda na kumuelimisha pale alipopotoka...Tunatakiwa tutende mazuri, mema ili yule aliyepotoka avutiwe kuwa karibu na mema.
Sasa ikiwa wewe kisa ni kumpinga mwenzio unamkashifu, unamponda bila kumuelimisha na kumuonesha upendo huyo mwenzio atakufuata vipi? Naimani mwisho wa yote nyote mtakuwa ni mliopotoka.. hakuna atakayeona uzuri wa kumfuata mwenzie uko wapi.

Ukitaka kujua Uislam umeamrisha mema ila tuu ni binadamu ndio Mashetani angalia kipindi cha MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN.
Humsikii mtu akitukana hovyo
Wanakuwa wakarimu,
Hawanywi wala kula vilivyokatazwa,
Wanakuwa ni wenye kutoa sadaka kwa wale wasiokuwa na uwezo,
Upendo unakuwa ulio jaa kwa kila namna...
Ila mwezi huu ukimalizika kila mmoja aliyeshetani anakuwa kama liyeshukuru kuwa alikuwa jela sasa ameachiwa....
Basi ukiona hivi ujue kuwa sio DINI YA UISLAM iliyoamrisha uovu bali NI BINADAMU TUU NDIO WAOVU, NDIO MAANA MWEZI ULE WANATENDA SANA MEMA....hatukuamrishwa kutenda mwema wakati mmoja tuu ila ni wakati wote..Na mwezi ule ni moja ya mifano ya miezi yote uliotilia mkazo kuwa uliyoamrishwa ni yapi.
 
Hao waliokamatwa wote waislam. Sijajua point yako ni nini? Cheki hiyo video ndio kosa lao



Ahh mbona sio mtume!! Watu kwa kuzusha !!! Anamtukana Sheikh sharif Hamad sio Mtume.
Halafu inaelekea huyu hajielewi, Eti ni Doctor halafu ametolewa na Serikali Uingereza amekuja kulipwa mshahara Laki mbili...
Hahahaha....nawasiwasi na huyu mtu, kama sio bwabwa sijui
 
Hii imekaaje wadau? Kuna watu wanashikiriwa na polisi zanzibar eti kwa kosa la kumkashfu mtume.! Kwa wanaojua zaidi mtujuze..
Chanzo star TV.
Hii imekaaje wadau? Kuna watu wanashikiriwa na polisi zanzibar eti kwa kosa la kumkashfu mtume.! Kwa wanaojua zaidi mtujuze..
Chanzo star TV.
Hii imekaaje wadau? Kuna watu wanashikiriwa na polisi zanzibar eti kwa kosa la kumkashfu mtume.! Kwa wanaojua zaidi mtujuze..
Chanzo star TV.
Unauliza ila tayari ukiwa unajibu lako, maana ukiuliza kitu ukaweka eti, tayari unajibu jibu lako wewe. alafu acha wanadini waamini wanachoamini, msiwapangie waaminije, mbona sisi ikiwa hivi tunafanya hivi, hayo ndiyo yanayotufautisha imani zetu. mbona hamuwashangai wale wanaochomana moto wakifa, hapa Tanzania tunafanya hayo.
 
Back
Top Bottom