Wanashikiliwa kwa kumkashfu mtume

Wanashikiliwa kwa kumkashfu mtume

Ndio maana nilikuuliza je kusudio lake ni kuua? Mungu anasifa ya kujua yasasa na yajayo. Sasa kama ulivyosema mwanzoni kwamba uweke chupa za soda kadhaa halafu chupa moja uweke sumu kati ya chupa hizo za soda halafu umwambie mtu anywe soda ila chupa moja inasumu. Je lengo la kuweka hiyo chupa yenye sumu ni nini? Kama sio kumtega mtu?
kitedawili hicho, kukitegua hapa kunahitaji kujitoa akiri!
 
Kama ulivyosema Imani hailazimishwi.Ni swala la kueleweshana,usipoelewa siku ya mwisho ndio hukumu itaamua.
Kwa Mtu yeyote anayesoma biblia na kuiamini,Kutoka kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo YESU KRISTO anaongelewa kama MUNGU na sio tofauti.
Hata wanaosema Yesu sio Mungu pia hutumia Biblia hiyohiyo ambayo wewe unasema inaeleza kuwa Yesu ni Mungu.

Usiishie tu kuamini biblia,mfano maelezo ya Paul ya kumuona Yesu yana utata wa hali ya juu na ndiyo yapo humo humo kwenye biblia.
 
Hata wanaosema Yesu sio Mungu pia hutumia Biblia hiyohiyo ambayo wewe unasema inaeleza kuwa Yesu ni Mungu.

Usiishie tu kuamini biblia,mfano maelezo ya Paul ya kumuona Yesu yana utata wa hali ya juu na ndiyo yapo humo humo kwenye biblia.

Hakuna Mkristo anayeweza kusema YESU sio Mungu.Huyo ujue sio Mkristo bali anajifanya Mkristo.Hao tunawaita wapinga Kristo.Hawana tofauti na wale wanaomlinganisha Issa bin Maryam na YESU KRISTO.
Hakuna utata wowote wa Saul(Paulo),Stefano au mtu yeyote kumwona YESU kama imeandikwa kwenye Biblia.
 
Mkuu huwa naamini una uelewa mkubwa ila hapa naona unashindwa kuelewa hoja ndogo sana

Mungu ana utawala (Administration) na pia ingawa ana mamlaka juu ya vyote na uwezo katika vyote ila aliweka segments za uongozi.

Ni sawa na wewe uniambie "Kama Rais ana mamlaka na ni amri jeshi mkuu"

Ni kwanini asitoe hukumu juu ya mkosefu flani?

KUMBUKA: ingawa ni Rais na Ana uwezo huo hawezi kumuingilia Hakimu au Jaji hata kama alimchagua yeye"

Kuna Malaika wa Vita, Wa Nuru n.k

Sasa usipoelewa hapo sijui kama utaelewa zaidi.
so kama kuna malaika wa vita unadhani kazi yake nini kama sio kupigana?,
mbona iko wazi sema wewe unaweka complication
 
Hakuna Mkristo anayeweza kusema YESU sio Mungu.Huyo ujue sio Mkristo bali anajifanya Mkristo.Hao tunawaita wapinga Kristo.Hawana tofauti na wale wanaomlinganisha Issa bin Maryam na YESU KRISTO.
Hakuna utata wowote wa Saul(Paulo),Stefano au mtu yeyote kumwona YESU kama imeandikwa kwenye Biblia.
Wakatoliki wanaamini yesu ni mwana wa mungu na sio Mungu. Kuna baadhi ya madhehebu ndio yana amini kuwa yesu ni Mungu mfano walokole
 
Wakatoliki wanaamini yesu ni mwana wa mungu na sio Mungu. Kuna baadhi ya madhehebu ndio yana amini kuwa yesu ni Mungu mfano walokole

Fuatilia vizuri.Wakatoliki wanaamini sana kwamba Yesu Kristo ni nafsi ya Pili ya Mungu aliye na Nafsi tatu yaani BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU.Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja.
 
Hakuna Mkristo anayeweza kusema YESU sio Mungu.Huyo ujue sio Mkristo bali anajifanya Mkristo.Hao tunawaita wapinga Kristo.Hawana tofauti na wale wanaomlinganisha Issa bin Maryam na YESU KRISTO.
Hakuna utata wowote wa Saul(Paulo),Stefano au mtu yeyote kumwona YESU kama imeandikwa kwenye Biblia.
Farudume inaonesha wewe sio msomaji wa biblia bali ni msomewaji wa biblia. Angalia mfano wa haya maandiko yanasema yesu ni nani:

Matendo 3:13

Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe.
 
Fuatilia vizuri.Wakatoliki wanaamini sana kwamba Yesu Kristo ni nafsi ya Pili ya Mungu aliye na Nafsi tatu yaani BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU.Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja.
Sio wakristo wote wanaoamini kuwa yesu ni Mungu.
 
Farudume inaonesha wewe sio msomaji wa biblia bali ni msomewaji wa biblia. Angalia mfano wa haya maandiko yanasema yesu ni nani:

Matendo 3:13

Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe.

Ukisoma Biblia kama kitabu cha hadithi hutaielewa.

Angalia vifungu vifuatavyo;

1.Yoh.8:58 Yesu akawaambia,Kabla ya Abrahamu kuzaliwa mimi nipo.

2.Yoh.3:11-13 Hakuna mtu aliyepata kwenda mbinguni isipokuwa mimi.

3.Yoh. 10:30 Mimi na Baba tu wamoja.
 
Hakuna Mkristo anayeweza kusema YESU sio Mungu.Huyo ujue sio Mkristo bali anajifanya Mkristo.Hao tunawaita wapinga Kristo.Hawana tofauti na wale wanaomlinganisha Issa bin Maryam na YESU KRISTO.
Hakuna utata wowote wa Saul(Paulo),Stefano au mtu yeyote kumwona YESU kama imeandikwa kwenye Biblia.
Na hilo ndiyo tatizo la wakristo,mnadhani kuwa na imani sana ndiyo usahihi wa hicho unachokiamini...imani ziko nyingi na haiwezekani zote zikawa sahihi hivyo lazima kuwe na dalili za usahihi wa hiyo imani.

Najua uzito wa Yesu kuitwa mungu kwenye ukristo ila cha kushangaza pamoja na uzito wa jambo lenyewe ila bado wenyewe kwa wenyewe wakristo wanatofautiana uwelewa katika jambo kubwa kama hili,ni kuonesha utata uliyopo kwenye hili jambo.

Mkuu kuna utata wa wazi katika madai ya Paul kumuona Yesu,fungua biblia na usome pote mule Paul alipolielezea hili tukio la yeye kumuona Yesu utaona anavyojichanganya sana. Kama ukishindwa kufanya hivyo sema nikuoneshe.
 
wakristo waelewa,nadhani kwa kuwa wamesoma sana elmu dunia!ambayo imewawezesha kuzoea ukosoaji hata kupitia debates mashuleni!
Hivi huko mashuleni wanapofundishwa kuna madarasa ya waislam na tofauti na ya wakristo?
Hii ni Pumba ya kufungia mwaka.
 
Ukisoma Biblia kama kitabu cha hadithi hutaielewa.

Angalia vifungu vifuatavyo;

1.Yoh.8:58 Yesu akawaambia,Kabla ya Abrahamu kuzaliwa mimi nipo.

2.Yoh.3:11-13 Hakuna mtu aliyepata kwenda mbinguni isipokuwa mimi.

3.Yoh. 10:30 Mimi na Baba tu wamoja.
Ndiyo maana nasema hata wanasema Yesu sio Mungu pia hutumia biblia,mnachokifanya nyie mtu akiwapa andiko lenye kuonesha kuwa Yesu sio Mungu nyie mnaenda kutafuta andiko la kuhalalisha uungu wa Yesu.

Huoni kuwa ndiyo mnazidi kuonesha utata wa hili jambo?
 
so kama kuna malaika wa vita unadhani kazi yake nini kama sio kupigana?,
mbona iko wazi sema wewe unaweka complication
Ndio kazi yake ni kupigana vita...kwani kuna mahali nimebisha hilo?
 
Na hilo ndiyo tatizo la wakristo,mnadhani kuwa na imani sana ndiyo usahihi wa hicho unachokiamini...imani ziko nyingi na haiwezekani zote zikawa sahihi hivyo lazima kuwe na dalili za usahihi wa hiyo imani.

Najua uzito wa Yesu kuitwa mungu kwenye ukristo ila cha kushangaza pamoja na uzito wa jambo lenyewe ila bado wenyewe kwa wenyewe wakristo wanatofautiana uwelewa katika jambo kubwa kama hili,ni kuonesha utata uliyopo kwenye hili jambo.

Mkuu kuna utata wa wazi katika madai ya Paul kumuona Yesu,fungua biblia na usome pote mule Paul alipolielezea hili tukio la yeye kumuona Yesu utaona anavyojichanganya sana. Kama ukishindwa kufanya hivyo sema nikuoneshe.

Mimi naongelea Wakristo na sio wale wanaojifunza ukristo.
Wakati unafundisha watu imani mpya lazima kuna watu watakuwa na mashaka kwa sababu ya kutokuelewa.Haya ndio yaliyomtokea Paulo.
Ukishakuwa Mkristo(yaani mfuasi wa Kristo) ina maana mashaka yote kuhusu Yesu yameshaondoka.
Haiingii akilini mtu kujiita Muislamu safi huku akitilia shaka Utume wa Mohamad(S.A.W).Kitakuwa ni kituko kumwita huyu mtu ni mwislamu.
 
Back
Top Bottom