Mi nazungumzia utata wa Paulo kwenye Matendo 9:6 "Lakini simama uingie mjini nawe utaambiwa yakupasayo kutenda".
Yesu anamwambia Paulo aingie mjini ndiyo ataambiwa apasayo kutenda,lakini kwenye Matendo 26:15-18. Ambalo ni tukio hilohilo ila huku Yesu tayali anamwambia Paulo nini cha kufanya na si hadi aingie mjini kama ilivyoelezwa kwenye Matendo 9:6.
Wala hapo hakuna kujichanganya hata kidogo.
Mat.9:6 inaeleza jinsi Sauli alivyotokewa na Yesu na maono mbalimbali aliyopewa wakati Mat.26:15-18 Paulo alikuwa anatoa utetezi wake mbele ya Mfalme Agripa.
Hapa kwenye utetezi alikuwa anatoa muhtasari wa yaliyotokea kwa ufupi ambayo alikuwa hajyajaandikwa katika vifungu vilivyotangulia.Anania huko Damascus alimwombea Paul na hatimae kujazwa Roho mtakatifu.
Roho Mtakatifu ndio mwongozo na Roho ya utendaji kwa Wakristo.Bila Roho Mtakatifu huwezi kutenda mambo yoyote ya kimungu. kwa hiyo Yesu alipomwambia aende mjini na ataambiwa yaliyo sahihi kufanya alimaanisha atapokea Roho Mtakatifu.vifungu vyote vipo sahihi.