Wanasheria tusaidieni hili la CHADEMA na Polisi

Mrimi

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
1,691
635
Kwa sasa watu wamegawanyika ktk makundi mawili.

Kuna linaloona kwamba maandamano wanayofanya CDM ni uvunjaji wa sheria, na kukaidi amri halali ya jeshi la polisi.

Lakini lingine linaona kwamba ni haki yao ya kikatiba kufanya maandamano ya amani ili kuonesha hisia zao juu mambo yale wanayoona ni kinyume na haki yao kikatiba.

Sasa tena jambo lingine ni kuhusu kibali cha kufanya maandamano:

-Chadema wanasema utaratibu halali si kuomba kibali bali ni kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kisha jeshi hilo lisimamie usalama katika maandamano hayo. Na kuhakikisha kwamba maandamano yanafanyika kwa amani bila uvunjifu wa sheria.

-Upande wa jeshi la polisi unasema Chadema wanawajibika kuomba kibali polisi, kisha polisi wana opt kutoa au kutokutoa hicho kibali kulinagana sababu za kiusalama.

Sasa tulio wengi si wajuzi wa sheria, tunaendeshwa zaidi na emotions. Kwa hiyo basi naamini kuna wanasheria wengi tu mnapita humu JF naomba mtuweke sawa katika hili. Napenda sana michango inayozingatia uhalisia wa mambo kuliko ushabiki usiokuwa na maana.
 
Maandamano ni haki ya msingi kwa wananchi hasa yanapokuwa ya amani na lengo maalum. Polisi wanatakiwa kupewa taarifa tu kutoa ulizi wakati wa maadamano sio kuzuia maandamano hata kama kuna taarifa wanazoziita za kiitelijinsia za namna gani. Wananchi hawahitaji kibali, ila kunaweza kukawa na makubaliano ya siku maalum ya kufanya hayo maandamano labda kutokana na mazingira/hali ya hewa au shughuli zingine ambazo zitaingilia au zitaingiliwa na hayo maandamano.

POLISI HAINA HAKI YA KUZUIA MAANDAMANO. KUFANYA HIVYO NI KUWANYIMA WANANCHI UWEZO WAO WA KUPAZA SAUTI.
 
umeelezea vema sana lakini kwa kuwa polisi ndo vinala wa kuvunja haki za binadamu hilo wanaona lipo mikononi mwao na ccm yao
 
Wakuu vipi, mbona hiki kijiwe cha wanasheria ni kama hakina wateja wengi?
Nilitegemea hii thread ingechangiwa na watu wengi ili tuwekane sawa katika jambo hili, lakini naona watu wanapita tu kumya kimya.
Au niipeleke hii hoja pale sebuleni (habari mchanganyiko)?
 
Wakuu vipi, mbona hiki kijiwe cha wanasheria ni kama hakina wateja wengi?
Nilitegemea hii thread ingechangiwa na watu wengi ili tuwekane sawa katika jambo hili, lakini naona watu wanapita tu kumya kimya.
Au niipeleke hii hoja pale sebuleni (habari mchanganyiko)?


Sure ebu jaribu kuipeleka huko, ila nachokiona hapa ni kwamba kuna watu wanatumia vibaya nafasi zao, au hawajui majukumu yao pia hawajiamini kutenda kama sheria inavyowaruhusu. Watu kama hao ndio mara nyingi wanaleta mikanganyiko katika jamiii.........
 
Maandamano ni haki ya msingi kwa wananchi hasa yanapokuwa ya amani na lengo maalum. Polisi wanatakiwa kupewa taarifa tu kutoa ulizi wakati wa maadamano sio kuzuia maandamano hata kama kuna taarifa wanazoziita za kiitelijinsia za namna gani. Wananchi hawahitaji kibali, ila kunaweza kukawa na makubaliano ya siku maalum ya kufanya hayo maandamano labda kutokana na mazingira/hali ya hewa au shughuli zingine ambazo zitaingilia au zitaingiliwa na hayo maandamano.

POLISI HAINA HAKI YA KUZUIA MAANDAMANO. KUFANYA HIVYO NI KUWANYIMA WANANCHI UWEZO WAO WA KUPAZA SAUTI.

Polisi hawalipwi kwa ajili ya kuzuia wananchi kufaidi haki zao za msingi, kazi ya polisi ni kuhakukikisha kuwa wananchi wanazipata haki zao za msingi. Kitendo chochote kinachozuia wananchi kufaidi haki zao sio kitendo cha kihalali.

Jaji Mwalusanya ( Marehemu) alishaweka wazi suala hilo katika kesi ya Mtikila ya mwaka 1994. Kiutaratibu, Uamuzi huo wa Mahakama kuu kwa vile haujapingwa wala kubatilishwa na mahakama ya juu unakuwa sheria. Polisi wanatakiwa kupewa taarifa tu, hawana haki ya kuzuia mikutano/maandamano wao wanatakiwa kutoa ulinzi pindi wakiarifiwa.
 
Polisi hawalipwi kwa ajili ya kuzuia wananchi kufaidi haki zao za msingi, kazi ya polisi ni kuhakukikisha kuwa wananchi wanazipata haki zao za msingi. Kitendo chochote kinachozuia wananchi kufaidi haki zao sio kitendo cha kihalali.

Jaji Mwalusanya ( Marehemu) alishaweka wazi suala hilo katika kesi ya Mtikila ya mwaka 1994. Kiutaratibu, Uamuzi huo wa Mahakama kuu kwa vile haujapingwa wala kubatilishwa na mahakama ya juu unakuwa sheria. Polisi wanatakiwa kupewa taarifa tu, hawana haki ya kuzuia mikutano/maandamano wao wanatakiwa kutoa ulinzi pindi wakiarifiwa.


Inawezekanaje walinzi wa sheria watumike kuvunja sheria tena? Ina maana ktk jeshi la poilisi hakuna wanasheria wanaojua kitu hiki?
OK, fine sasa what is the way forwads?
 
Back
Top Bottom