Nilivyokuwa na miaka 14 nilipata ajali mbaya ya kogogwa na Gari Arusha. Mimi na rafiki yangu wakati huo tulikuwa kwenye baiskeli tunashangilia kuchaguliwa kuingia form 1. Mimi ndiyo nilikuwa abiria na bahati mbaya ndiyo niligogwa na gari la kampuni ya caterpillar na dereva akakimbia. Bahati nzuri gari lilikuwa na namba kubwa ubavuni na boss yule akashikwa baada ya uchunguzi.
Hii kesi yangu ilianza mwaka 1990 na mpaka leo sijui iliendeleaje lakini mpaka namaliza form 4 mwaka 1993 watu watatu mashahidi upande wangu walikuwa wamekufa kwa ulakini mmoja alikiwa polisi. Baada ya kuona watu wanakufa na mahakama inachukuwa muda yawezekana kesi waliamua kuifuta. Lakini cha ajabu mpaka leo kesi za Tanzania zinachukuwa muda sana na sijajua vizuri hasa sababu ni nini?
Naomba watu ambao ni mawakili, majaji au waendesha mashitaka watueleze ni kwanini kesi zinachukuwa muda mrefu sana na kunyima watu haki zao za msingi.
Hii kesi yangu ilianza mwaka 1990 na mpaka leo sijui iliendeleaje lakini mpaka namaliza form 4 mwaka 1993 watu watatu mashahidi upande wangu walikuwa wamekufa kwa ulakini mmoja alikiwa polisi. Baada ya kuona watu wanakufa na mahakama inachukuwa muda yawezekana kesi waliamua kuifuta. Lakini cha ajabu mpaka leo kesi za Tanzania zinachukuwa muda sana na sijajua vizuri hasa sababu ni nini?
Naomba watu ambao ni mawakili, majaji au waendesha mashitaka watueleze ni kwanini kesi zinachukuwa muda mrefu sana na kunyima watu haki zao za msingi.