Napita humu ...nimeona huu mjadala nashangaa hata nyie watanzania mnaojiita wapenda amani mnaopaswa kuwa na upendo mnataka kuwaua watoto wenu wenye matatizo ya jinsia na mashoga na walio zaliwa na jinsia mbili na wenye mapungufu ya kibayolojia(hormonal imbalances and genetic mutations) na kisaikolojia.....nimesoma wengi wenu hapa mna chuki za kufa mtu....najiuliza jee? mgepewa mamlaka na nguvu kama za Mungu si mgewaangamiza zamani za kale.....Lo!.....ndio maana hamna anayemfahamu Mungu humu duniani labda wachache sana na hunyakuliwa mapema....na sio hata ufahamu wa asili mia moja.......hata vitabu vilivyoandikwa na wanadamu wasio na uwezo asili mia moja wa kujua mawazo ya Mungu.....hivo vitabu mnavyo husisha na Mungu mtashangaa mtakapo fahamu hamna hata moja inayokaribia ama kuyafahamu mawazo ya Mwenyezi Mungu.....ndo maana mnashinda mkipigana ...mara wakristo mara waislamu......mara wayahudi...mara..wahindi....nyie nyote .....hadi siku mtakapo fahamu kuwa Mungu ni upendo tu na mengine hatuwezi kuyaelewa kumhusu....muishi maisha yenu na muwapende ndugu,dada,watoto na majirani /jamaa zenu......nashukuru Mungu wa ukweli, huyu wa upendo wa kweli kwa kusaidia wakenya wengi kuwa na mawazo ya ncha na mapana,kutupa uvumilivu wa kutohukumu yale hatuyafahamu kabisa,kutokuwa wepesi wa hasira, ila bado utafiti unafanywa na wanaohusika na sio kwa sababu za siasa bali kwa utu,ueleo mkubwa na wa ndani wa kisayansi na ukweli dunia nzima......mpaka itakapo funuliwa kwetu.