Wanaowasha full light barabarani usiku

Wanaowasha full light barabarani usiku

Habari za jioni waheshimiwa, mo naomba bunge lijalo lipitishe sheria kali kwa wale wanaowasha taa full wakati wa usiku kwani huwa zinaumiza sana, kitu ambacho kinaweza kusababisha kutokuona vizuri na wakati mwingine ajali.

Unakuta madereva wengine wanawasha taa kali kama vile wanawinda maporini usiku. Huwa inakera sana wajameni.

Au kama sheria ipo tafadhali nijulishwe hatua za kufuata.

Ni hayo tuu kwa leo, nawasilisha ....

sheria ya usalama barabara no.30 ya mwaka 1973 na marekebisho yake no 16 ya 1996 sehemu ya 39 kifungu cha 39c kifungu cha 5 inasema: dipped (beam) itaruhusiwa kwenye
(a) mitaa ya watu wengi na zipo taa za kandokando mwa barabara,
(b) iwapo anamkaribia mwenzake ili wapishane vizuri
(c) iwapo anataka kulipita gari la mbele yake
(d) mtu yeyote akitenda kinyume cha hapo atakuwa ametenda kosa.
 
Mimi usiku nawasha full light kama hakuna gari napishana nayo, ila niko makini nikiona gari inakuja naondoa full light. Nikiona mwenzangu yuko full, na mimi naweka full ghafla naondoa tena kama hashtuki namwekea full moja kwa moja tukomoane tuu.

Kiustaarabu mwenzako akikushtua ni vyema ukamheshimu, la sivyo na yeye atakuwekea maana unamwumiza
 
Habari za jioni waheshimiwa, mo naomba bunge lijalo lipitishe sheria kali kwa wale wanaowasha taa full wakati wa usiku kwani huwa zinaumiza sana, kitu ambacho kinaweza kusababisha kutokuona vizuri na wakati mwingine ajali.

Unakuta madereva wengine wanawasha taa kali kama vile wanawinda maporini usiku. Huwa inakera sana wajameni.

Au kama sheria ipo tafadhali nijulishwe hatua za kufuata.

Ni hayo tuu kwa leo, nawasilisha ....
Ebu jaribu kutoa matumizi ya hizo taa,je ziwashwe mchana tu?
 
Nimeielewa hoja yako.

Mimi nashauri wataalam wetu wa semiconductors na electonics kutoka chuo kikuu, Dit pamoja na Veta wa-designe circuit itakayokuwa na uwezo wa ku kutambua mwanga ikimulikwa kisha inabadili automatically kutoka full light kwenda dimm light.

wirring hiyo ya magari ndio itungiwe sheria kushinikiza kila gari lazima lifungiwe kifaa hicho.

TATIZO LITAKUWA LIMEKWISHA.


Wala hawana haja ya ku design upya, zipo tayari duniani. Kuna magari yanakuja nazo.

Kiasi cha serikali kuagiza tu kuwa lazima kila gari ifungwe hicho kifaa.

Jisomee:Automatic Vehicle Headlight Dipper/Dimmer Circuit | Homemade Circuit Projects
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.

Nenda mafunzo ya udereva Ndugu ndio utajua matumizi ya taa ,wapi na wakati gani inapaswa kutumika.
 
Kama wewe hujui kuendesha gari usidhani wote wapo kama wewe> Nimesoma driving na leseni ninayo> ninaendesha magari tangu miaka ya mapema ya 1980. Usikurupuke humu jf.
 
Mimi usiku nawasha full light kama hakuna gari napishana nayo, ila niko makini nikiona gari inakuja naondoa full light. Nikiona mwenzangu yuko full, na mimi naweka full ghafla naondoa tena kama hashtuki namwekea full moja kwa moja tukomoane tuu.

Kiustaarabu mwenzako akikushtua ni vyema ukamheshimu, la sivyo na yeye atakuwekea maana unamwumiza

Umeongea jambo la msingi sana na kitu ambacho huwa nakifanya pia, ajabu kuna mtu unamshutua ili apunguze halafu wala hajigusi wanakera sana hawa watu kwakweli
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.

Asante kwa hii post, naamini kuna watu watabadilika baada ya kusoma huu uzi kama tu watajifunza kuwa wastaarabu
 
Katika latest design ya magari Toyota Landcruiser vx v8 inayotarajiwa kutoka mwaka 2016, hayo yote yameangaliwa, Gari itabadilisha yenyewe taa kulingana na mazingira na mahali, itapunguza mwendo yenyewe endapo umeisogelea gari nyingine kwa nyuma ili kuepusha ajali au kusimama yenyewe kama gari iliyoko mbele yako imesimama na kama wewe huko kwenye nafasi ya kuipita. yapo mengi sana yaliyoboreshwa.
 
Kweli kabisa hata kwa waenda kwa miguu...hususan tukiwa tumepiga maji
 
funga spot light anayekupiga full na wewe unafanya yako!

Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......
 

Attachments

  • image.jpg
    image.jpg
    19 KB · Views: 145
Kweli kabisa hata kwa waenda kwa miguu...hususan tukiwa tumepiga maji

Tena ukiwa maji......unaona kama ni pikipiki mbili zinakuzengua............bora kusiwe na hizo taa kabisa...........
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.

Haswa wale walio rithi leseni badala ya mali, wale walio okota leseni na wale wanao endesha magari ya shemeji zao wana adabu mbaya sana tena mara nyingine una mpa na ishara hata ashtuke chaa ajabu ana kuwa mkaidi na mwingine ndio anakuwashia na spotlight!
 
Hili tatizo liko sana kwa madereva wa mjini. Siku akioata safari atajuta atakapokutana na lori lina mifull ya ajabu.

Kuepukana na tatizo hili tembea na kioo cha kujiangalizia kile cha nyumbani ukipigwa full unakiweka pale mbele wala huna haja ya kumflash lazima atazima mifull yake maana reflection yote ataipata mwenyewe.
 
Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......

Hata kwenye double ukikaa upande wa kulia utajuta ukikutana na mtu ana sports light zake zile za xenon full hd headlight. Lazima utaingia mtaroni.

Kuepuka shari wakati wa usiku nakaa upande wa kushoto kwenye hizi double sitaki shida.
 
Unamuogesha na lijitaa hiloo........
ila mimi nadhani........ili kupunguza ajali.....serikali ifanye barabara zote za masafa marefu ziwe double road.......katika mfano huu.......Ili hata kwenye kupigana taa........msipatane.......

Hata kwenye double ukikaa upande wa kulia utajuta ukikutana na mtu ana sports light zake zile za xenon full hd headlight. Lazima utaingia mtaroni.

Kuepuka shari wakati wa usiku nakaa upande wa kushoto kwenye hizi double sitaki shida.
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.
Khaa!! Hapa inabidi ujisogeze kidogo kwenye driving
 
Usiombe kupishana na Coaster za bagamoyo huku Boko Ile mijitu haijui dim yenyewe ni full light halafu inaendesha hovyo,sijui ndo viroba fake halafu karibia wote...nshafunga spot lights ni mwendo wa piga nikupige nikikuflash ukawa mstaarabu Nami nanywea wengine wale wa maselela wanawasha maspots ya juu ni shida kabisa,tubadilike.
 
Back
Top Bottom