masdinero masproblemas
JF-Expert Member
- Mar 19, 2022
- 224
- 178
Kuna vituko sana lakini hakuna zaidi ya ujinga wetu binadamu.Bila Wakaidi na Wapingaji tungekuwa hatuna maendeleo huku tukiishi kwenye sayari yetu ambayo ni tambalale na jua linaizunguka....
Na wala tusingehoji wala kutafuta / kujua mazingira yetu ili tupambane nayo sababu tungekuwa tunakengeuka kama waliotaka kujenga mnara wa Babeli (Na bila hao kutaka kujenga huo Mnara huenda hizi lugha tofauti zingekuwa hazipo)
Hence binafsi ninapenda uwepo wa hao so called wakaidi
Yaan kama sio wachache kuhoji na kukataa kushikiwa akili dunia ingekuwa bado ndio katikati ya ulimwengu. Kila kitu kinazunguka sayari hii maalum, na sisi wanadamu ndio tungekuwa tumeekewa vitu vyote(sayari za kila aina gesi na jiwe, nyota za kila aina, mawingu yanayozaa nyota, miundo mbalimbali ya vikundi vya nyota n.k) ulimwenguni. Ili tu kuwaaminisha na kushangaza viumbe binadamu uwezo wa mwenyezi mungu. Lengo tuabudu huyo mungu. Mambo yote mwisho ibada!
Lakin wap... sayari yetu ni ndogo, ya kawaida mno. Jua letu nyota kubwa kiasi, isiyo na maajabu yeyote. Mtaa wetu wa nyota umedorora, hamna matukio yoyote makubwa ya kiulimwengu yanayotokea au kuendelea ukitoa kijamii chetu kinachojiita cha pekee. Knachodai kuumbwa na muumbaji wa ulimwengu wote unaotuzunguka sisi(sio kweli). Kwa ajili tu ya kumpunguzia upweke na kumuabudu huyo mungu. Baadae auangamize na wachache wachaguliwe kuendelea na huo utumwa milele kwake, kusikojulikana. Hakuna anayepajua.
Ujinga mtupu!