Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Wanaopinga uwepo wa Mungu ni wakaidi

Kutengenezwa pia inawezekana. Sheria haziruhusu bado duniani kote. Hakujakuwa na hitaji la kutengeza. Dunia haina uhaba wa watu, tena unaweza sema tumezidi kuliko fursa za maisha zilizopo. Watu wanazaa zaidi kuliko kuzalisha mali!
Weka ushahidi mwana sayansi gani duniani aliyewwza kutengeneza mbegu za kiume na mayai ya mwanamke ili apatikane binaadam

Mpaka sasa hakuna mwanasayansi yoyoye anayeweza

1)kutengeneza shahawa na mayai ya mwanamke ili azaliwe binaadam

2) Kumfanya binaadam asizeeke na aishi milele

3) kumfufua mtu aliyekufa

Kama yupo mwanasayansi anayeweza kufanya mojawapo au yote hayo 3 weka ushahidi hapa tuone
 
Weka ushahidi mwana sayansi gani duniani aliyewwza kutengeneza mbegu za kiume na mayai ya mwanamke ili apatikane binaadam

Mpaka sasa hakuna mwanasayansi yoyoye anayeweza

1)kutengeneza shahawa na mayai ya mwanamke ili azaliwe binaadam

2) Kumfanya binaadam asizeeke na aishi milele

3) kumfufua mtu aliyekufa

Kama yupo mwanasayansi anayeweza kufanya mojawapo au yote hayo 3 weka ushahidi hapa tuone
Kuna taaluma nyingi za kuunda viumbe hai kwa kukuza chembe za dna. Cloning. Hakuna serikali iliyokubali kwa sababu za kutohitaji hiyo tech. Mifumo inayotumika ni kama ile ya mabadiliko asili ya viumbe hai. Unaweza kufatilia kwa muda wako. Kasome. Utaelewa. Mjadala uendelee.

Kwahyo kwa hoja ya vile hakuna anayeweza kuzalisha binadamu maabara( inawezekana) inahusiana vipi na imani za uwepo wa miungu?

Bado sio ushahidi. Huwezi kutoka kwenye uwepo wa kushindikana kurudia jambo fulani ukahitimisha kuwa jambo hilo limetokana na kitu kingine usichokijua. Unaunganisha vipi?

Yaani unaanza tu, "hakuna anayeweza kuumba uhai. Hii ni ishara mungu yupo". Uko tayari kubadili mtazamo utakapogundua inawezekana kuunda viumbe hai? Maana kusema mungu yupo kwa sababu kuna vitu haviwezekani unajiweka katika nafasi ya kuhamisha hoja kila jambo linapofikiwa na maendeleo ya uelewa wa vitu duniani.

Wewe hapo ulipo ni kama mungu hajakuumba. Umezaliwa. Wewe hapo ni kopi. Narudia tena. Kama uwepo wako wewe, nakala ya vizazi vya nyuma, ni hoja ya uwepo wa mungu basi wote wanaoweza kufyatua kopi za binadamu(cloning), na wapo sana tu, nao ni miungu pia. Mungu wako bana upekee unaompa. Tunaishi miongoni mwa miungu. Hoja dhaifu sana.
 
Weka ushahidi mwana sayansi gani duniani aliyewwza kutengeneza mbegu za kiume na mayai ya mwanamke ili apatikane binaadam

Mpaka sasa hakuna mwanasayansi yoyoye anayeweza

1)kutengeneza shahawa na mayai ya mwanamke ili azaliwe binaadam

2) Kumfanya binaadam asizeeke na aishi milele

3) kumfufua mtu aliyekufa

Kama yupo mwanasayansi anayeweza kufanya mojawapo au yote hayo 3 weka ushahidi hapa tuone
Suala la kutozeeka, kutibu magonjwa sugu na yanayoathiri wengi kama kansa linakwamishwa na mambo mengi. Kuna tafiti nyingi kama zike za human stem cell zinapingwa kwa sababu za kijinga. Chanzo cha sababu ni hizo imani zenu. Ukifatilia kutoka hapa utaelewa naongelea nn.... mfano kukuza cells, tissue au organs kwenye maabara kusiaidia watu na shida za uzee kunategemea sana hii tafiti. Tatizo ni imani za wanasiasz walio wengi wanapinga kutokana na ujinga wa iman zao kwamba sayansi hii inaingilia uumbaji wa mungu!

Hao hao wanaruhusu gmo ifanyike kwenye vyakula tunakula mimea na mifugo iliyobadilishwa sana. Yote ili kurahisisha maisha. Tutafika muda ukiruhusu.

Kufufua watu kila siku inafanyika sehemu huko duniani. Ukiona mtu moyo umesimama na kuwa kitabibu ni mfu unadhani kinachofanyika pale ni nn? Kama sio defibrillator na cpr unakufa! Mungu anashangaa tu muda huo. Upasuaji kuokoa wanawake na vichanga ni tendo la kuokoa uhai. Imetokea fetal distress hata uombe vipi mtoto anakufa na pengne mama nae atapata hatari ya kupoteza maisha. Mungu yu wapi. Kuna wajinga hingiza hoja ya hao wanaotibu wanawezeshwa na mungu. Wanakuwa mawakala wa mungu. Hoja ingne dhaifu. Mungu wa mizunguko. Anajivuta taratibu kusubiri watu wasome, wafanye tafiti, wapate uelewa halafu isemwe tu amewawezesha.

Hakuna nafasi ya uwepo wa mungu kwenye maisha ya binadamu. Tunalazimisha uwepo wake. Hayupo. Sio kwa hizi hoja zilizopo. Ndio pekee kilichopo, bila hoja(porojo, hadithi, imani n.k.) hakuna ushahidi mwingne!
 
yan unamaanisha kila kilichoumbwa kwa uwezo wa kipekee bas kina muumba wake!kwahyo hapo unakubali kabisa kuwa sisi viumbe wa dunian tunamuumba wetu ! Lakin hakuna formula ya kuwa kila kinachoumba kitu complex bas nae lazma aumbwe na mwingne coz hata sisi binadamu mbona tunashindwa kuumba viumbe vingne? Kwahyo sio lazma Mungu awe ameumbwa ila yeye ni alfa na omega,alikuwepo na atakuwepo daima
Unajuaje Mungu ni alfa na omega kweli na hiyo si story uliyokaririshwa tu?

Unaweza ku prove Mungu yupo?
 
Unajuaje Mungu ni alfa na omega kweli na hiyo si story uliyokaririshwa tu?

Unaweza ku prove Mungu yupo?
Ndio nimekuthibitishia kutoka maelezo yangu ya hapo juu,lakini pia mi nimesoma theories mbali mbali za wanasayansi wasioamin Mungu,ni theories za 'Origin of life' lakin bado kuna critics nying sana,,,Ndugu yangu amin tu mwenyez Mungu yupo
 
Kijana huwa nakwambia hivi, usijibu hoja zangu kama hujazielewa. Unakumbuka nilikwambia nini ile siku ? Nilikwambia unatakiwa ukijue unachokijadili.

Pili, sijawahi kukimbia hoja, sababu unapokosoa hoja ina maana unajua unachokisimamia. Sasa nakuuliza swali ambalo ni lazima ujibu unaniuliza tena mimi ? Sasa kwanini unajenga hoja kwa jambo usilo lijua ? Maana yake unajadili ili kupotezea watu muda, ndiyo maana unauliza maswali ya kijinga ambayo laiti kama ungesoma nilichokiandika usinge uliza maswali hayo. Haya huwa nakwambia mara chungu mbovu.

Sasa usilete lawama za uongo na kijinga baada ya wewe kushindwa hoja, unachotakiwa ni ujibu hoja siyo unakimbia hoja.

Unajua katika maswali yote niliyo kuuliza ni swali moja tu ndiyo umejaribu kujibu ? Sasa huu utoto ndiyo huwa naukataa kila siku.
We uniambie nini cha kujadili, hiyo sio kazi yako

Kama hujawahi kukimbia hoja nambie hapa ulifanya nini
1648719881637.png


Nina sababu nyingi za kuonesha kwanini umekuwa ukikimbia mjadala kwa mbinu tofautitofauti halafu unakuwa wakwanza kulaumu

Leo sikupi mwanya huo tena kama ilivyo kwa siku ile, ni eidha ukubali hujui au utoe majibu ya kile ulichokileta ili tuendelee na mjadala vinginevyo hatuwezi kuendelea zaidi
 
Rejea kuanzia post namba 139 kisha uniambie pale ulitakiwa kujibu swali nililo kuuliza au kuuliza swali ? Muda huo ambao jibu kwa swali halijakidhi vigezo ?

Kisha ufike kwenye post namba 155. Post ile ilikuwa inajibu swali kwa kile ulichokiandika. Nilikuuliza unaijua hatima yako ? Kabla yake niliuliza tena kwanini ufanye mabaya ? Unakumbuka hili ? Kama hauko makini katika mjadala au unakumbukumbi ndogo achana na mijadala hii
Unani point kwenye post yako #139 kuwa kuna swali uliniuliza sijakujibu wakati jukumu la post yako hiyo ilikuwa ni kujibu hoja zangu za post #125?
 
Mimi nipo kijana, sababu nina kijua nachokijadili. Jibu maswali ninayo kuuliza kisha tuendelee.

Nipo, huna hoja ya kunifanya nikimbie, na kwanini nikimbie ?
Mambo yaliyo nje na uwezo wetu ni yapi?
 
Ndio nimekuthibitishia kutoka maelezo yangu ya hapo juu,lakini pia mi nimesoma theories mbali mbali za wanasayansi wasioamin Mungu,ni theories za 'Origin of life' lakin bado kuna critics nying sana,,,Ndugu yangu amin tu mwenyez Mungu yupo
Niamini tu au nikubali kwa sababu umethibitisha?

Unaelewa vitu hivi ni tofauti?

Kama umethibitisha, kwa nini niamini tu?

Wapi umethibitisha Mungu yupo?
 
Bado unatoa majibu ya kihuni

Uhuru wa huyo mtu uko wapi kama amezuliwa kufanya jambo fulani?

Mtoto namba 1 anafungiwa ndani na mzazi wake kwa kuzuiwa kwenda kucheza na wenzake.

Na pia kuna mtoto namba 2 ambaye wazazi wake wammpa uhuru wa kwenda kucheza na wenzake pale atapojiskia

Ni mtoto namba ngapi mwenye uhuru wa kuchagua leo nikacheze na wezangu au nisiende na ikawezekana?
Soma hivyo vitabu ndugu vina majibu ya maswali yako, ni vema wakati unavisoma ungepata ufafanuzi kutoka kwa watu wenye maarifa zaidi ya dini ya UISLAMU yaliyo sambamba na huo ufahamu mfano: ABU RASLAAN MUSSA KILONGOZI, ABU FADHIL QASSIM MAFUTA, ABU ABDI-SALAAM MUJAAHID, ABU UMAYR ADAM MANDHUMATUL na wengine wengi, visome hali ya kuwa moyo wako upo huru - ruhusu kupokea haki ijapokuwa ladha yake si tamu

Hii ni moja ya mada ngumu sana 'FREE WILL & DIVINE DECREE' kuwahi kuwepo kwenye ulimwengu wa imani na wanazuoni wakubwa wanakiri juu ya hilo hadi kufikia kuonya waumini kufikiri sana na kuhoji sana juu ya masuala yanayohusiana na haya kwa kuchelea wengi ni wenye maarifa madogo wanaweza wakatatizika na wakatoka kwenye mstari, mambo mengi ya imani hayapimwi kwa hoja za falsafa, mantiki au akili, ulimwengu wa imani ni ulimwengu wa yakini, hivyo kwenye ulimwengu huu baadhi ya mambo yamewekewa mipaka na tahadhari, baadhi ya mambo yanahitaji mapokeo na kuyaitakidi tu kama yalivyokuja - si kila jambo ni la kutafakari kwa 100% au kuhoji sana mfano: MWENYEZI MUNGU asili yake ni nini? ametokana na nini? yeye ni wa kwanza na mwisho, wa kwanza kwa maana gani? chanzo chake ni nini? haya ni baadhi tu ya maswali ambayo si salama kujiuliza kwa waumini wa imani mbalimbali, hivyo inashauriwa watu wayapokee kwa uchache wake na yanawakinaishe

Sisi ambao ni waumini wa imani mbalimbali, tunafahamu na tunaheshimu nafasi za wasiosadikisha uwepo wa MUNGU kwa hoja mbalimbali, kila mtu ana uhuru wa kuamini anachoamini na haifai kuwalazimisha wala kuwashurutisha waamini vile tunavyoamini, wanadamu hatufanani kwa hali zote - si kifikra tu hata uwezo wa kupambanua mambo, na kamwe hamna jambo ambalo wanadamu wote tutakuja kuwa na ufahamu mmoja, haitakuja kutokea na haijawahi kutokea, kwa hali hii ni vema kila mmoja aheshimu msimamo wa mwenzake pasina kubezana, bali kueleweshana tu kwa nia njema na kwa lugha nzuri

Suala jingine: waumini wa imani mbalimbali mfano: WAYAHUDI, WAKRISTO, WAISLAMU, WABAHAI, WAHINDU na wengine mnatakiwa mfahamu kwamba, unapojadiliana na wapagani au watu wasioamini uwepo wa MUNGU mara nyingi hatuhitaji kutumia maandiko ya vitabu vitakatifu au vyanzo vingine vya maandiko ya kiroho kama marejeo yetu, wao hawaviamini - si rahisi andiko likawakinaisha hata liwe na tija kwenye imani zetu isipokuwa mara chache sana - hususani wanapofanya mifananisho au wanapokuwa wameuliza swali linalohitajia jibu la kiakili kutoka kwenye vitabu, wao sanasana wanatumia ELIMU ZA MANTIKI, SAYANSI, FALSAFA na HISTORIA, hivyo unapojadiliana nao hakikisha nawe upo njema kwenye hizo fani na unajua kujenga hoja mfano: anaweza akawa anapinga uwepo wa MUNGU kwa hoja ya kutokuonekana kwake, kwa hoja yake hiyohiyo waweza kumuuliza: mbona hapingi uwepo na maumivu na hali hayaonekani? hivyo ndivyo mijadala yetu dhidi yao inavyoendeshwa, na baadhi ya nyakati ni kwa kumpatia marejeo au andiko linalofafanua mada inayomtatiza kwa lengo la kuongeza maarifa yatakayomsaidia kumuondoa kwenye mabanoView attachment Shaykh muhammad ibn saleeh AL-UTHAYMEEN - QADAR.pdfView attachment 2170226
 
We uniambie nini cha kujadili, hiyo sio kazi yako

Kama hujawahi kukimbia hoja nambie hapa ulifanya nini
View attachment 2170237

Nina sababu nyingi za kuonesha kwanini umekuwa ukikimbia mjadala kwa mbinu tofautitofauti halafu unakuwa wakwanza kulaumu

Leo sikupi mwanya huo tena kama ilivyo kwa siku ile, ni eidha ukubali hujui au utoe majibu ya kile ulichokileta ili tuendelee na mjadala vinginevyo hatuwezi kuendelea zaidi
Hujaonyesha baada ya hapo nilijibu nini.
 
Unani point kwenye post yako #139 kuwa kuna swali uliniuliza sijakujibu wakati jukumu la post yako hiyo ilikuwa ni kujibu hoja zangu za post #125?
Kwani unaandika uongo. Anzia hapo kwenye post 139 kwenda mbele.
 
Unani point kwenye post yako #139 kuwa kuna swali uliniuliza sijakujibu wakati jukumu la post yako hiyo ilikuwa ni kujibu hoja zangu za post #125?
Shida nyingine unasahau sana kijana, swali gani katika post yangu namba 121 ulijibu ? Ndiyo maana nikasema hujibugi maswali yangu.
 
Kuna taaluma nyingi za kuunda viumbe hai kwa kukuza chembe za dna. Cloning. Hakuna serikali iliyokubali kwa sababu za kutohitaji hiyo tech. Mifumo inayotumika ni kama ile ya mabadiliko asili ya viumbe hai. Unaweza kufatilia kwa muda wako. Kasome. Utaelewa. Mjadala uendelee.

Kwahyo kwa hoja ya vile hakuna anayeweza kuzalisha binadamu maabara( inawezekana) inahusiana vipi na imani za uwepo wa miungu?

Bado sio ushahidi. Huwezi kutoka kwenye uwepo wa kushindikana kurudia jambo fulani ukahitimisha kuwa jambo hilo limetokana na kitu kingine usichokijua. Unaunganisha vipi?

Yaani unaanza tu, "hakuna anayeweza kuumba uhai. Hii ni ishara mungu yupo". Uko tayari kubadili mtazamo utakapogundua inawezekana kuunda viumbe hai? Maana kusema mungu yupo kwa sababu kuna vitu haviwezekani unajiweka katika nafasi ya kuhamisha hoja kila jambo linapofikiwa na maendeleo ya uelewa wa vitu duniani.

Wewe hapo ulipo ni kama mungu hajakuumba. Umezaliwa. Wewe hapo ni kopi. Narudia tena. Kama uwepo wako wewe, nakala ya vizazi vya nyuma, ni hoja ya uwepo wa mungu basi wote wanaoweza kufyatua kopi za binadamu(cloning), na wapo sana tu, nao ni miungu pia. Mungu wako bana upekee unaompa. Tunaishi miongoni mwa miungu. Hoja dhaifu sana.
Weka ushahidi mwana sayansi gani duniani aliyewwza kutengeneza mbegu za kiume na mayai ya mwanamke ili apatikane binaadam

Mpaka sasa hakuna mwanasayansi yoyoye anayeweza

1)kutengeneza shahawa na mayai ya mwanamke ili azaliwe binaadam

2) Kumfanya binaadam asizeeke na aishi milele

3) kumfufua mtu aliyekufa


Niliweka hizo hoja kwa sababu hizo hoja 3 hapo zinabeba uwezo wa Mungu

Kwa bahati mbaya hujajibu hata moja nilijua utaweka link za makala mbalimbali kuthibitisha hao banadamu wenzako wenye uwezo wa kuumba binadamu wengine kama wewe

Katika Qurani Mungu ametumbia hakuna yoyote anaeweza kuumba hata Inzi zaidi yake yeye Mwenyezi Mungu

Unaongea vitu kana kwamba tunaishi dunia totauti wakati wote tunaishi dunia moja na dunia ni kama Kijiji

Hao wanasansi wako ambao ndio unataka wakutanyie prove kuwa hakuna Mungu sio tu kuumba binaadam hata uwezo wa kuumba organs za binaadam hawana

Hawezi kuumba FIGO
Hawawezi kuumba Moyo
Hawawezi kuumba Ini

Juzi kati kuna mtu walimuwekea organ ya Nguruwe kama sio ini basi ni moyo au figo na wamefeli jamaa ameshindwa kuishi amefariki

Mtabaki tu kudanganyana na kujazana ujinga

Nahata kama ungekuwepo huyo mwanasansi anayetengeneza viumbe hai
Watu kama sisi tungemuliza hayo material aliyoyatumia amepata wapi maana inabidi atoke nje ya universe akatafute hayo material kwa sababu material yaliopo hapa duniani yote ni Mungu hivyo angekuwa hajafanya kitu
 
Mambo yaliyo nje na uwezo wetu ni yapi?
Jibu hoja yangu kabla, inakuwaje unajadili mambo usigo yajua na kujidai unajua ? Hili swali ulitakiwa uulize pale tu nilipo anza na jambo hili. Lakini hauko makini kijana, jambo hili nililiashiria.
 
Je naye Mungu ana wish binadamu wafanye mazuri ya kumpendeza ili asiwachome moto lakini hana option ya kuwafanya wawe hivyo anavyotaka?
Mungu ameumba free wills kwa Mwanadamu!!,,,lkn akampa Sheria zake kuwa aishi ivi, hutaki atakuadhibu! nakuwa mwanadamu amuabudu tu baasi!! ndo alivo taka! hakuna kuhoji!.... Mfano Mama/Baba yako lazima umuheshimu!!...ufanye anayo taka!!

lkn pia una uhuru wa kuto muheshimu!!...na usipo muheshimu Mzazi wako kuna adhabu utaipata maarufu hapo Bongo!! hii inaitwa Laana!...km huijui jaribu tu!

yaani hata unaweza kumtukana, kumpiga,kumfanya hata kijakazi wako....kumfungia nje, hata kumpiga mpaka uka muua,,,,lkn nikuulize tu....Matokeo yake ni Mazuriii??......hata Mtu mpita njia ! anae lingana Umri na Baba yako utamheshimu sana!!

Kama utafanya Mabaya kwa Wazazi wako Duniani humu iko shida km hutaoa!! wala kuolewa!! ajabu sasa waolewaji nani aliwaambia kuwa ulifanyia wazazi wako hayooo hadi wakukatae???!....hata km utaoa ukazaa kwa kujibana saaana....kipigo watakacho kupa hao wanao, siyo cha Dunia hii!!

Uzuri ni kwamba unaweza ukajaribu tu!! uone matokeo.... mwishoni hii itakuonyesha kuwa Mungu yupo!...hao wazazi ndo miungu wako wa kwanza kabisa Duniani!.....Kinyume chake wapende uwaheshimu!! uone utakavyo tusua..kmau zaidi ya Diamond!

Jiwe alidharau Machozi ya Mamake mwandishi Kabendera tena yule mama akalia kuwa mwanae ndo nguzo!! uhai wake unamtegemea mpaka yule Mama kafa.......haya Jiwe yuko wapi leo???.... Na kabendera alimpenda na kumuheshimu Mama yake fika!!

Leo kabendera anatusua majuu!! kuku kwa Mrija na Mbinguni ataenda!! je Jiwe wako yuko wapi?? kwanza hata hakupata mda wa kutubu! Na Jiwe alikuwa mdogo sana kwa yule Mama! lkn jiwe halikumheshimu wala kusikiliza ! sababu ya kiburi cha uzima eti Rais!

Na jiwe kafa kwa ugonjwa uleule ulio muua yule Mama!! pamoja na kulindwa juu na chini, pamoja na Madaktrai wooote kumtibia lkn hawakuona dawa!!...jiwe akadharaulika Duniani mara dufu....akaogopa hata kusafiri!! akafia humu!!

Kabendera ni Muandishi..
 
Soma hivyo vitabu ndugu vina majibu ya maswali yako, ni vema wakati unavisoma ungepata ufafanuzi kutoka kwa watu wenye maarifa zaidi ya dini ya UISLAMU yaliyo sambamba na huo ufahamu mfano: ABU RASLAAN MUSSA KILONGOZI, ABU FADHIL QASSIM MAFUTA, ABU ABDI-SALAAM MUJAAHID, ABU UMAYR ADAM MANDHUMATUL na wengine wengi, visome hali ya kuwa moyo wako upo huru - ruhusu kupokea haki ijapokuwa ladha yake ni chungu, hivyo ndivyo mambo yalivyo

Hii ni moja ya mada ngumu sana kuwahi kuwepo kwenye ulimwengu wa imani na wanazuoni wakubwa wa UISLAMU wanakiri juu ya hilo hadi kufikia kuonya waumini kufikiri sana na kuhoji sana juu ya masuala yanayohusiana na haya kwa kuchelea wengi ni wenye maarifa madogo wanaweza wakatatizika na wakatoka kwenye mstari, masaili mengi ya kidini hayapimwi kwa hoja za kiakili, mantiki wala falsafa, ulimwengu wa imani ni ulimwengu wa yakini, hivyo kwenye ulimwengu huu baadhi ya mambo yamewekewa mipaka na tahadhari, baadhi ya mambo yanahitaji mapokeo na kuyaitakidi tu kama yalivyokuja - si kila jambo ni la kutafakari kwa 100% au kuhoji sana mfano: MWENYEZI MUNGU asili yake ni nini? ametokana na nini? yeye ni wa kwanza na mwisho, wa kwanza kwa maana gani? chanzo chake ni nini? haya ni baadhi tu ya maswali ambayo si salama kujiuliza kwa waumini wa imani mbalimbali, hivyo inashauriwa watu wayapokee kwa uchache wake na yanawakinaishe

Sisi ambao ni waumini wa imani mbalimbali, tunafahamu na tunaheshimu nafasi za wasiosadikisha uwepo wa MUNGU kwa hoja mbalimbali, kila mtu ana uhuru wa kuamini anachoamini na haifai kuwalazimisha wala kuwashurutisha waamini vile tunavyoamini, wanadamu hatufanani kwa hali zote - si kifikra tu na uwezo wa kupambanua mambo, na kamwe hamna jambo ambalo wanadamu wote tutakuja kuwa na ufahamu mmoja, haitakuja kutokea na haijawahi kutokea, kwa hali hii ni vema kila mmoja aheshimu msimamo wa mwenzake pasina kubezana, bali kueleweshana tu kwa nia njema na kwa lugha nzuri

Suala jingine: waumini wa imani mbalimbali mfano: WAYAHUDI, WAKRISTO, WAISLAMU, WABAHAI, WAHINDU na wengine mnatakiwa mfahamu kwamba, unapojadiliana na wapagani au watu wasioamini uwepo wa MUNGU mara nyingi hatuhitaji kutumia maandiko ya vitabu vitakatifu au vyanzo vingine vya maandiko ya kiroho kama marejeo yetu, wao hawaviamini - si rahisi andiko likawakinaisha hata liwe na tija kwenye imani zetu isipokuwa mara chache sana - hususani wanapofanya mifananisho au wanapokuwa wameuliza swali linalohitajia jibu la kiakili kutoka kwenye vitabu, wao sanasana wanatumia ELIMU ZA MANTIKI, SAYANSI, FALSAFA na HISTORIA, hivyo unapojadiliana nao hakikisha nawe upo njema kwenye mambo hayo na unajua kujenga hoja mfano: anaweza akawa anapinga uwepo wa MUNGU kwa hoja ya kutokuonekana kwake, kwa hoja yake hiyohiyo waweza kumuuliza: mbona hapingi uwepo na maumivu na hali hayaonekani? hivyo ndivyo mijadala yetu dhidi yao inavyoendeshwa, na baadhi ya nyakati ni kwa kumpatia marejeo au andiko linalofafanua mada inayomtatiza kwa lengo la kuongeza maarifa yatakayomsaidia kumuondoa kwenye mabanoView attachment 2170227View attachment 2170226
Mkuu kwa ulivyosema tu kuwa haya mambo hayatakiwi kutumia akili kwa mtazamo wako, hiyo ni hoja yenye ushawishi?

Ebu geuza kibao chukulia hayo maneno ndio yamesemwa na mkristo katika harakati za kukutaka kukuonesha jinsi Ukristo ndio imani sahihi na Uislamu ni upotofu, utayakubali maelezo hayo?

Umesema haipaswi kuuliza baafhi ya maswali mfano kuuliza Mungu alitoka wapi

Kama unaweka kizuizi kwa maswali ya msingi ambauo unaelewa mtu yeyote ambaye haamini Mungu hilo litakuwa swali lake muhimu, unategemea nani atakubaliana na maelezo yako kuwa ni yakweli?
 
Kwani unaandika uongo. Anzia hapo kwenye post 139 kwenda mbele.
Kwani post #125 iko mbele au nyuma?

Kama iko nyuma niambie ulijibu?

Kama hukuijibu kwanini tuanzie mbele wakati huku nyuma nako kuna vilaka uliviacha?
 
Shida nyingine unasahau sana kijana, swali gani katika post yangu namba 121 ulijibu ? Ndiyo maana nikasema hujibugi maswali yangu.
Hiyo #121 si ulikuwa ume quote post yangu ya #119?

Sasa post #119 si ilikuwa na maswali?

Au hujui huu mjadala nimeuanza mimi kwa kukuuliza swali ambalo ulilikimbia kwa mdau kwa kile ulichokidai kuwa mpaka ajibu maswali yako?
 
Back
Top Bottom