Wanaoomuamini Mungu, wana nini cha kujivunia?

Wanaoomuamini Mungu, wana nini cha kujivunia?

Sasa mtu anayeamini Mungu wake ni wa kweli 100% na anamuongoza atamsikiliza vipi binadamu tu kwa kuwa binadamu tuna mipaka ya maarifa?

Kwa nini unataja mipaka ya maarifa ya binadamu wakati mwenzako anaamini 100% anamtegemea Mungu na hamtegemei binadamu?
Kutambua kuwa binadamu tuna mipaka ya maarifa hakumaanishi ninamtegemea binadamu kuliko Mungu , bali ni unyenyekevu wa kutambua kwamba hata ufahamu wa Mungu tunaupokea kwa kipimo, si kwa ukamilifu wote.

Hivyo, kumsikiliza binadamu si kusaliti imani, bali ni njia ya hekima ya kuchuja, kuthibitisha, na hata kuimarisha kile unachoamini. Mungu humtumia pia binadamu mwingine kuonesha ukweli wake, kama alivyowatumia manabii na mitume.
 
Kutambua kuwa binadamu tuna mipaka ya maarifa hakumaanishi ninamtegemea binadamu kuliko Mungu , bali ni unyenyekevu wa kutambua kwamba hata ufahamu wa Mungu tunaupokea kwa kipimo, si kwa ukamilifu wote.

Hivyo, kumsikiliza binadamu si kusaliti imani, bali ni njia ya hekima ya kuchuja, kuthibitisha, na hata kuimarisha kile unachoamini. Mungu humtumia pia binadamu mwingine kuonesha ukweli wake, kama alivyowatumia manabii na mitume.
Kama unamuamini Mungu wako 100% , Mungu ambaye uwezo wake hauna mipaka, kwa nini uone umuhimu wa kumsikiliza binadamu mwenzio ambaye ushajua maarifa yake yana mipaka?

Huoni kwamba ukishaanza kumsikikiza binadamu mwenzako umeshaweka uwezekano kwamba huyo Mungu wako hakuongozi vizuri 100% na jivyo unahitaji kumsikikiza huyo binadamu mwenzako akijazie pale ambapo Mungu hajakuongoza?
 
Kumwamini Yesu ni mengi ya kujivunia, aliyemwamini Yesu ni mshindi wa mengi
 
Kama unamuamini Mungu wako 100% , Mungu ambaye uwezo wake hauna mipaka, kwa nini uone umuhimu wa kumsikiliza binadamu mwenzio ambaye ushajua maarifa yake yana mipaka?

Huoni kwamba ukishaanza kumsikikiza binadamu mwenzako umeshaweka uwezekano kwamba huyo Mungu wako hakuongozi vizuri 100% na jivyo unahitaji kumsikikiza huyo binadamu mwenzako akijazie pale ambapo Mungu hajakuongoza?
Kumsikiliza binadamu si dalili ya kushuku uongozi wa Mungu, bali ni kutambua kuwa Mungu anaweza kuzungumza kupitia wengine. Imani ya kweli haikufungi masikio, bali inapima kila jambo kwa hekima .
 
Kumsikiliza binadamu si dalili ya kushuku uongozi wa Mungu, bali ni kutambua kuwa Mungu anaweza kuzungumza kupitia wengine. Imani ya kweli haikufungi masikio, bali inapima kila jambo kwa hekima .
Ukishaanza kuamini Mungu anaweza kuzungumza kupitia wengine maana yake imani yako kuwa Mungu ana uwezo wa kuzungumza nawe moja kw amoja imepungua.

Utajuaje Mungu anazungumza kupitia wengine na hayo si maneno ya watu tu?
 
Kakataza majadiliano na militant atheists.

Majadiliano yanaruhusiwa kwa wenye muelekeo wa kutaka kujua ukweli sio kwa waliokataa na sasa wanatafuta mabishano.

Mkristo hakai kubishana. Wapo waliomuona kwa macho walimkataa. Na wapo bado hatujamuona kwa macho na tumemkubali. Kazi zake tunaziona! !

Namna hiyo.

PRAISE THE LORD JESUS.
Dini ni utapeli that's why china na baadhi ya nchi za Asia Wana miungu Yao na wanamafanikio kuliko nchi ambazo zinazo muamini Yesu na Muhammad

Dini ni zao la elimu ya kiroho elimu ambayo ndani yake inahusika na kuutumikisha ulimwengu wa kiza kuwa connected na ulimwengu wa kiroho na Nyama( kimwili)

So inapotokea ukawa unafanya maombi Fulani Ambayo kimsingi waasisi wa maombi hayo ndio wanajua chanzo chake basi hayo maombi ni lazima yatakupa matokeo chanya cuz Kuna energy unakuwa unaipata Toka direct Kwa baina ya ulimwengu wa giza na ulimwengu wa roho kuja ktk ulimwengu wa nyama

So Called Yesu /Muhammad/ na mitume as mwamposa and the likes wanahiyo elimu ya kuutumikisha Ulimwengu wa kiroho na ulimwengu wa giza ili uweze kuleta matokeo chanya ktk ulimwengu wa nyama

Baada ya wao kuweza kumaster hiyo elimu ya ulimwengu ninao kueleza hapo juu ndio Waka form Taasisi za kidini ili wapate wafuasi ambao watakapo kuwa wanazitumikia Dini hizo baada ya wao kupewa maagano ya ulimwengu wa kiza na kiroho --- kuwa endapo mkitufanyia hivi na hivi Basi na sisi tuta wapa power ,

In short ni mambo yanayo husu kupata spiritual power Toka Kwa mizimu na majini lakini Kwa kuwa hauwezi kumwambia mtu kuwa chanzo Cha dini hizi ni mizimu na majini ndio wakaja na Jina la Mungu Kwa Lengo la kuwa pumbaza watu ili waweze kuamini Kwa wepesi

Kisha baada ya kuform dini hizo ndio wakaziundia Sheria na kanuni Kwa waumini wake, Awali Dini zilikuwa na Lengo Hilo lakini zilipo fika mikononi Kwa wanasiasa wakazigeuza kuwa Psychology weapon ya kuweza kuwasaidia kupata madaraka kuendelea kuwatawala watu Kwa wepesi Kwa kuwa brain wash na kuwatawala Kwa kuwa devide and rule Wananchi Kwa kutumia Imani zao

That's why Leo hii tunaona Kila muumini wa dini yake lazima amuone muumini wa dini nyingine kuwa ni mtu aliye potea anayefaa kutengwa and the likes, So Kwa mfano ikitokea nchi Fulani ikapata Kiongozi anaye taka kuupush agenda zake ili ziweze kukubalika haraka ni lazima ataangalia nchi hiyo Ina idadi kubwa ya Wananchi wanao amini ktk Dini Gani Kisha Alisha jua Dini ipi yenye idadi kubwa ya waumini na Dini ipi yenye waumini wengi wenye exposure au power ya kiuchumi Au dini ipi Ina wajinga wengi basi mwanasiasa husika ana weza kuyatumia hayo makundi Tajwa hapo juu ktk kuweza kupata Millage ya kisiasa

Na kuendelea kubaki madarakani Dini hizi Kuna wakati huwa zinatumika kama the way ukabila unavyo tumika ktk baadhi ya mataifa katika kuwa chonganisha Wananchi na serikali kisiasa au katika Kuinufaisha serikali kisiasa ,

Na muanzilishi wa hiyo system ni Ibrahim ,

Hakuna masuala ya Mungu + Peponi Wala nini hayo yote ni utapeli , Yale mambo unayo yaona ya waumini wa kiislam kwenda Hijja Maka na Wa Cristian kwenda Hijja Israel Yale ni matambiko but yame fanyiwa propaganda ili watu waamini kuwa ndio formula ya dini inavyo taka ,Yale ni matambiko maana ukienda makka utaenda kuzuru makaburi na kulizunguka jiwe ukienda Israel utaenda kuzuru makaburi pia , so kwaajili yako ya kawaida Kuna tofauti Gani hapo na waafrica wanao kwenda kuzuru makaburi ya mababu zao na kusali kwenye mawe makubwa au miti mikubwa !??

Yale ni matambiko Yaliyo fanyiwa PR ili watu waweze kuya catch Kwa wepesi na kuyaamini that's why Huwa USA ili kuwa Ina peleka macelebrity Makka like kina Michael Jackson ili wawe kama influencer wakuya fanyiwa promotion cuz macelebrity Wana ushawishi mkubwa ktk jamii wakifanya jambo ni rahisi jambo Hilo kukubalika


Jiulize Why china wanaimani zao za kitamaduni before ya ukristo na uislam na Taifa lao Lina fanya Maendeleo makubwa kuliko wale wenye Imani ya Muhammad na Yesu , so kama Mungu wa Yesu/ Muhammad ndiye mungu wa haki na wa halali na mwenye power Authority Inakuwaje ana muacha Mungu wa china awe na uwezo mkubwa wa kuwa saidia wa china ktk kuwafanya waweze kutimiza malengo Yao na kuwa super power kuliko mataifa mengine yanayo muamini mungu wa Yesu na Muhammad!?? Kwa mantiki hiyo it means mungu wa Yesu / Muhammad Hana nguvu mbele ya Mungu wa china !?? 😁😁😁

Halafu kitu kingine Cha kuchekesha Sasa Kwa nyinyi waumini wa hizi dini mbili ni pale Tunapo ona USA ambalo baadhi ya watu wengi huamini kuwa ndio taifa la shetani USA hao hao ndio wanao tumika kuyalinda mataifa takatifu ya Mungu Israel/ Saudi Arabia Yaani mataifa ya Mungu haya wezi kujilinda yenyewe mpaka yapewe msaada wa ulinzi na Taifa la shetani!!! WTF 😂😂😂🙌😂

Dini ni uchizi , Walau Onyesheni kujitambua basi nyie wafia dini , Dini hazina nafasi katika Karne hii maana zimejaa Utapeli + Ujinga ,
 
Hivi, kwa nini watu wanaomuamini Mungu wakisoma posts za wasioamini katika uwepo wake, wanaumia na kuona kama kuna viumbe hawana akili.

Wakati huo huo, wasiomuamini huyo Mungu, wanawaona wenzao kama kawaida, wenye haki ya kuamini wanachokitaka, bila kejeri na matusi kama ya wana wa Mungu?


Mungu wa wanaomuamini yawezekana hana heshima na yeye ndo wanajifunza huko!!!!

Wakati huo huo, wasioamini wengine wana maisha mazuri kuliko wanaoamini na kuabudu, wenzetu wanaoamini, Mungu wao kama mbaguzi na anawajali wasiomuamini, iweje waandame wasioamini? Si hiari yao?
Umeongea kimyume, wasioamini ndo huwaona waamini wameshikwa akili. Wanaoamini huwaona wasioamini kama wakosaji wanaosubiri hukumu.

Kama huamini, kutana na mlokole wewe ukiwa na mwanamke huku mmelewa na yeye yupo na biblia kisha mzungumze.

Wewe utamuona mjinga na yeye atakuona umepotea utachomwa.
 
Ndo hapo sasa. Je, kwa ninin mimi nisieamini, nisiwaone nyie mnaoamini mmepotea njia? Hili swali lina mabishano hakika. Swali lilikuwa kwa nini sasa, muwaone wamepotea njia, na wao wakiwaona nyie, wanaona ni kawaida, hawajishughulishi na kuwaconvice musiamini? Af wanaoamini, wanataka waonekane wao ndo wako sahihi
Wanaoamini wamepewa wajibu wa kuwafanya wasioamiamini waamini, hawawezi kutulia, aliye ndani yao anawasukuma kufanya hivyo.
 
Ukishaanza kuamini Mungu anaweza kuzungumza kupitia wengine maana yake imani yako kuwa Mungu ana uwezo wa kuzungumza nawe moja kw amoja imepungua.

Utajuaje Mungu anazungumza kupitia wengine na hayo si maneno ya watu tu?
Sauti ya Mungu haibadiliki kwa njia anayotumia, kuamini anaweza kuzungumza kupitia wengine si kupunguza imani, bali ni kuikubali hekima yake ya kutumia njia mbalimbali. Tunatambua sauti yake kwa kupatana na Neno lake, amani ya moyoni pamoja , na uthibitisho wa Roho Mtakatifu.
 
Sauti ya Mungu haibadiliki kwa njia anayotumia, kuamini anaweza kuzungumza kupitia wengine si kupunguza imani, bali ni kuikubali hekima yake ya kutumia njia mbalimbali. Tunatambua sauti yake kwa kupatana na Neno lake, amani ya moyoni pamoja , na uthibitisho wa Roho Mtakatifu.
Ujishaamini dini tofauti na yako, inayopingana na yako, inaweza kuwa kweli, Mungu tofauti na wako, anayepingana na wako, anaweza kuwa wa kweli, hapo maana yake umeamini Mungu wako anaweza kuwa si wa kweli.

It is that simple.
 
Ujishaamini dini tofauti na yako, inayopingana na yako, inaweza kuwa kweli, Mungu tofauti na wako, anayepingana na wako, anaweza kuwa wa kweli, hapo maana yake umeamini Mungu wako anaweza kuwa si wa kweli.

It is that simple.
Kuamini Mungu wangu ndiye wa kweli hakuhitaji nikatae kuwepo kwa imani tofauti , bali natambua kuwa ukweli hauko kwenye wingi wa mitazamo, bali kwenye msingi thabiti wa ufunuo wa kweli.

Easy!
 
Kuna mama dr,aliniambia hivyo vifilosofi mnasoma vinawaharibu kuwafanya msiamini katika Mungu

Nilimuuliza hivi
According to the bible shetani ameshushwa tupo nae duniani kwahiyo inakiaje Mungu mwenye upendo kwa wanadamu,atumix na shetwani muovu,

Nilitumia mfano rahisi sana na mwepesi maana yule mama alikuwa mweupe sana kichwani ulokole umemjaa,hakujibu swali zaidi alienda mbali na kuniambia nahitaju therapy

Nikamuuliza kwanini,

Sababu huamini Mungu

Hakika nilimuacha haende zake uku hakisikitika sana,
Kwa hiyo na wewe ukajiona bonge moja la mtu, kwamba huyo mama ni mweupe, wewe umejaa nondo..kwa hiyo hilo swali lako ndo kipimo cha Mungu yupo au hayupo na wote wakishindwa..una conclude Mungu hayupo..??Duuuh...
Hayo mambo ya Mungu yupo ama hayupo tafuteni majibu wenyewe, msitafute VALIDATION kutoka kwa watu waunge mkono mnachoamini, waacheni kama kweli hayupo ipo siku watakua enlighted kama nyinyi mnavojiona, WAO PIA wawaache - kila mtu ashinde mechi zake..
 
Kuamini Mungu wangu ndiye wa kweli hakuhitaji nikatae kuwepo kwa imani tofauti , bali natambua kuwa ukweli hauko kwenye wingi wa mitazamo, bali kwenye msingi thabiti wa ufunuo wa kweli.

Easy!
Suala si kukataa kuwapo kwa imani tofauti.

Suala ni, je, hizo imani tofauti ni za kweli?

Ukishaamini Yesu ndiye njia pekee ya kufikia kwenye uzima wa milele mbinguni utasemaje tena kuwa hata bila Yesu, Buddha naye anaweza kukufikisha mbinguni?

Huoni kuwa hapo kutakuwa na contradiction?
 
Suala si kukataa kuwapo kwa imani tofauti.

Suala ni, je, hizo imani tofauti ni za kweli?

Ukishaamini Yesu ndiye njia pekee ya kufikia kwenye uzima wa milele mbinguni utasemaje tena kuwa hata bila Yesu, Buddha naye anaweza kukufikisha mbinguni?

Huoni kuwa hapo kutakuwa na contradiction?
Hakuna contradiction kama unaelewa kuwa watu wanaweza kuwa kwenye safari tofauti kuelekea kwa Mungu mmoja, lakini kupitia neema yake, si kwa juhudi zao.

Kuamini Yesu ni njia pekee haimaanishi lazima umpokee kwa jina hilo hilo duniani , Mungu anaweza kujifunua kwa kila mtu kwa namna tofauti kulingana na maarifa na mazingira yao. Ukweli uko kwa Yesu, lakini watu wanaweza kumfikia kwa njia tofauti, siyo lazima iwe hii hii ninayo amini mimi.
 
Hakuna contradiction kama unaelewa kuwa watu wanaweza kuwa kwenye safari tofauti kuelekea kwa Mungu mmoja, lakini kupitia neema yake, si kwa juhudi zao.

Kuamini Yesu ni njia pekee haimaanishi lazima umpokee kwa jina hilo hilo duniani , Mungu anaweza kujifunua kwa kila mtu kwa namna tofauti kulingana na maarifa na mazingira yao. Ukweli uko kwa Yesu, lakini watu wanaweza kumfikia kwa njia tofauti, siyo lazima iwe hii hii ninayo amini mimi.
Ukienda hivyo, umejiruhusu hata kumkanusha huyo Mungu na kumkataa kuwa atheist na kusema atheist naye anaweza kufika mbinguni bila kumkubali Yesu wala Mungu.
 
Ukienda hivyo, umejiruhusu hata kumkanusha huyo Mungu na kumkataa kuwa atheist na kusema atheist naye anaweza kufika mbinguni bila kumkubali Yesu wala Mungu.
Mungu hamwokoi mtu kwa kutoamini, bali kwa kumfunulia ukweli hata katika ujinga wake.

Atheist haokolewi kwa kutokuwa na imani, bali kwa kubadilishwa na Mungu hadi amkiri. Hivyo, bado Yesu ndiye njia , Mungu ndiye anayemvuta mtu kwa wakati wake, na siyo sisi kwa mipaka yetu.
 
Mungu hamwokoi mtu kwa kutoamini, bali kwa kumfunulia ukweli hata katika ujinga wake.

Atheist haokolewi kwa kutokuwa na imani, bali kwa kubadilishwa na Mungu hadi amkiri. Hivyo, bado Yesu ndiye njia , Mungu ndiye anayemvuta mtu kwa wakati wake, na siyo sisi kwa mipaka yetu.
Huyo Mungu mwenyewe huwezi kuthibitisha yupo.

Kama unabisha, thibitisha yupo.
 
Back
Top Bottom