Mgirik
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 13,258
- 13,368
Kweli tupu, mwanamke unafanya kazi unarudi umechoka , bado majukumu ya nyumbani yanakusubiri ,dume unakuta limekaa tu kwenye tivii linasubiri kila kitu lifanyiwe na ukipanda tu kitandani linataka mzigo, ukifanya tofauti unaambiwa eti hujui majukumu yako, nichoke na kazi, nirudi nihudumie familia, na bado nikuhudumie wewe chakula cha usiku , nisipotoa chakula cha usiku vizuri kutokana na kuchoka utaniambia sijui mapenz, moyo huo utatoka wapi ikiwa wewe umekaa tu yaani hujitambui wala kujigeuza kwa lolote na bado unilaumu ,kwani ukinisaidia kazi utakufa, khaa nyie kwani wanawake maroboti? Mkiambiwa ukweli eti mwanamke msomi au mwenye kazi ni jeuri , kiukweli hamjitambui achaneni na mfumo dume wa kijinga!
huo ni uwongo mtupu. Wanawake wa siku hizi hasa nyinyi mnaojiita wasomi mnapika?
Na hg anafanya nn? Mnajifanya mpo busy na kaz kumbe mnagawa kwa mabos wenu maofisin.