Wanaojua mawasiliano ya TAMISEMI au Wizara ya Elimu nina shida muhimu sana

Yuyo Ahumile Shamalendi

JF-Expert Member
Mar 10, 2018
993
782
Wakuu habari, kama nilivozungumzia kwenye kichwa cha habari.

Nina shida na mawasiliano ya TAMISEMI kwa anayeelewa niingieje kwenye website yao au email yao, vilevile sina email yao wala website yao, naombeni anayefahamu mawasiliano yao anisaidie.

Bila kujali ngoja niwaeleze tatizo linalonituma niwatafute hao.

Nina watoto wawili ambao majina yao yalikosewa shuleni, na sasa hivi wapo sekondari, mmoja yuko form four na mwingine yuko form one.
Nataka nifuatilie kama kuna uwezekano wa majina yao kurekebishwa, maana nimekuja kugundua hicho kitu baada ya kwenda kuwakatia vyeti vya kuzaliwa, wale watumishi wa ofisi ya usajili wa vizazi na vifo waliniambia niende shuleni kwao nikachukue majina yao ndipo niwapelekee.

Sasa baada ya kwenda shuleni kwao nikakuta naandikiwa majina ambayo yana makosa ya baadhi ya herufi, huyu wa form four jina la tatu limekosewa ni herufi moja tu ndo iko sahihi, na huyu wa form one jina la pili limekosewa herufi mbili na la tatu limekosewa kabisa.

Naombeni wakuu mwenye uelewa wa hivi vitu anieleweshe nifanyeje ili kurekebisha haya majina, maana hawa wa usajili wa vizazi na vifo walinishauri niende ofisi za elimu sekondari wilaya lakini baado maelezo walionipa hayakua ya kunisaidia.

Na ni lazima watoto niwakatie vyeti vya kuzaliwa.

Karibu kwa ushauri wenu na msaada pia wa mawasiliano ya TAMISEMI.
 
Wakuu habari, kama nilivozungumzia kwenye kichwa cha habari.

Nina shida na mawasiliano ya TAMISEMI kwa anayeelewa niingieje kwenye website yao au email yao, vilevile sina email yao wala website yao, naombeni anayefahamu mawasiliano yao anisaidie.

Bila kujali ngoja niwaeleze tatizo linalonituma niwatafute hao.

Nina watoto wawili ambao majina yao yalikosewa shuleni, na sasa hivi wapo sekondari, mmoja yuko form four na mwingine yuko form one.
Nataka nifuatilie kama kuna uwezekano wa majina yao kurekebishwa, maana nimekuja kugundua hicho kitu baada ya kwenda kuwakatia vyeti vya kuzaliwa, wale watumishi wa ofisi ya usajili wa vizazi na vifo waliniambia niende shuleni kwao nikachukue majina yao ndipo niwapelekee.

Sasa baada ya kwenda shuleni kwao nikakuta naandikiwa majina ambayo yana makosa ya baadhi ya herufi, huyu wa form four jina la tatu limekosewa ni herufi moja tu ndo iko sahihi, na huyu wa form one jina la pili limekosewa herufi mbili na la tatu limekosewa kabisa.

Naombeni wakuu mwenye uelewa wa hivi vitu anieleweshe nifanyeje ili kurekebisha haya majina, maana hawa wa usajili wa vizazi na vifo walinishauri niende ofisi za elimu sekondari wilaya lakini baado maelezo walionipa hayakua ya kunisaidia.

Na ni lazima watoto niwakatie vyeti vya kuzaliwa.

Karibu kwa ushauri wenu na msaada pia wa mawasiliano ya TAMISEMI.
Huyo was form four muache atumie hivyo hivyo kwa sababu ashasajiliwa tayar
 
Huyo was form four muache atumie hivyo hivyo kwa sababu ashasajiliwa tayar
Mkuu kuhusu huyo nilielekezwa hivo hivo nikawaelewa ofisi ya sekondari Wilaya.

Shida ni kwamba akifaulu kwenda form five atatakiwa awe na cheti cha kuzaliwa, na cheti cha kuzaliwa hawawezi kutengeneza majina tofauti na ya mzazi hasa jina la tatu, maana huyu wa form four jina la kwanza liko vizuri na la pili liko vizuri, shida ipo kwenye hili la tatu.

Hili la tatu lililo halisi ambalo nalitumia hata mimi lina herufi sita, lakini wao wameweka herufi nne na katika hizo herufi nne moja tu ambayo ni ya kwanza ni sahihi, hizi nyingine zote siyo sahihi.
 
Potezea tu, demu wangu kwao anaita Mariette, walimu wakamuandika Malta, mpaka sasa amekuwa OCS hajahojiwa popote
 
Samahani mkuu,

Pole na tatizo linalokukumba
Ingia google search www.tamisemi.com.tz itakuja web site yao ingia nenda chini kabisa Utapata mawasiliano.

Pia wizara ya elimu search www.wizara ya elimu.com.tz fuata utalatibu wa apo juu

Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom