ARCHBISHOP
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 271
- 488
Tokea nikiwa mdogo nimekuwa niksikia kuhusu uzi ndoa za mkeka, na niliambiwa hizi ufungishwa kwa razima pale unapofumaniwa na binti wa watu basi unawekwa chini ya ulinzi na shekhe anaitwa na ndoa inafungwa, uwe unataka au hutaki!
Binafsi nimekuwa nikipinga jambo hili na ninajiuliza ni muda gani hati za ndoa upatikana ghlafla ivi? Na je? Tangazo la ndoa linakuwa limetoka?
Je akitokea muweka pingamizi atasikilizwa? Na mwanaume akiamua kukataa atafanywa nini pale?
Vipi kuhusu wazazi wa mwanaume, hawana haki yakumfumania binti na kijana wao wakawapiga pingu za maisha?
Kwenye sheria za ndoa ndoa hii ni batili lakini nashangaa bado serikali haitaki kuzipiga marufuku kabisa maana vibinti vya uswahilini vinavizia vijana wenye mwelekeo, vinajitongozesha nakujileta geto, kumbe vimeshaandaa wajomba, mashangazi mpaka mababu. Tazama sheria ya ndoa hapa chini!
******************
MAANA YA NDOA
Kwa mujibu wa kifungu cha 9(1), cha Sheria ya Ndoa, sura ya 29
ya sheria za Tanzania, ndoa ni muungano wa hiari kati ya
mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu kwa muda wa
maisha yao yote.
Hata hivyo, muungano huo ili uweze kukamilika kisheria ni lazima
mambo ya msingi yafuatayo yazingatiwe, nayo ni:
2.1 Hiari
Kifungu cha 16 kinaeleza kuwa muungano huo lazima uwe wa hiari.
Udanganyifu au ulaghai, kurubuniwa kwa aina yoyote unafanya
muungano usiwe wa hiari. Kama itathibitika kwamba hakukuwa na
hiari basi muungano huo hauwezi kufikia hadhi ya kuwa ndoa.
Watoto wa kike kuchaguliwa wanaume na wazazi/walezi wao au
ndoa zinazoitwa za mkeka si ndoa kwa mujibu wa sheria hii ya ndoa.
Binafsi nimekuwa nikipinga jambo hili na ninajiuliza ni muda gani hati za ndoa upatikana ghlafla ivi? Na je? Tangazo la ndoa linakuwa limetoka?
Je akitokea muweka pingamizi atasikilizwa? Na mwanaume akiamua kukataa atafanywa nini pale?
Vipi kuhusu wazazi wa mwanaume, hawana haki yakumfumania binti na kijana wao wakawapiga pingu za maisha?
Kwenye sheria za ndoa ndoa hii ni batili lakini nashangaa bado serikali haitaki kuzipiga marufuku kabisa maana vibinti vya uswahilini vinavizia vijana wenye mwelekeo, vinajitongozesha nakujileta geto, kumbe vimeshaandaa wajomba, mashangazi mpaka mababu. Tazama sheria ya ndoa hapa chini!
******************
MAANA YA NDOA
Kwa mujibu wa kifungu cha 9(1), cha Sheria ya Ndoa, sura ya 29
ya sheria za Tanzania, ndoa ni muungano wa hiari kati ya
mwanaume na mwanamke unaokusudiwa kudumu kwa muda wa
maisha yao yote.
Hata hivyo, muungano huo ili uweze kukamilika kisheria ni lazima
mambo ya msingi yafuatayo yazingatiwe, nayo ni:
2.1 Hiari
Kifungu cha 16 kinaeleza kuwa muungano huo lazima uwe wa hiari.
Udanganyifu au ulaghai, kurubuniwa kwa aina yoyote unafanya
muungano usiwe wa hiari. Kama itathibitika kwamba hakukuwa na
hiari basi muungano huo hauwezi kufikia hadhi ya kuwa ndoa.
Watoto wa kike kuchaguliwa wanaume na wazazi/walezi wao au
ndoa zinazoitwa za mkeka si ndoa kwa mujibu wa sheria hii ya ndoa.