Wananchi washangazwa na udikiteta unaofanywa na viongozi wa CHADEMA

Mie nimewasilisha kilio cha wananchi waliowengi wasioweza kufika hapa jamvini wadau!!!

5.Wananchama wa CDM na watanzania kwa

Kweli umejaliwa ujinga. Endelea kuwepo humu uelimishwe.

1. Ili kuzipa uzito hoja taarifa za kikao hicho cha wananchi zingeongeza thamani ya hoja yako.

2. Ulichoeleza ni ubakaji binafsi wa hali ya juu wa democrasia ambao unaonyesha upeo wako wa fikra na maslahi ya kilafi.

3. Hata chama wanautaratibu wa kuwaingiza mamluki kufanya unachokifanya

Kifupi jitahidi kuwa mkweli acha mapishi ya taarifa.
 
wanajamvi ni vyema tukajikita kwenye hoja za wananchi na tusipambane na mtoa mada.mimi nimewasilisha malalamiko ya wananchi ambao nimekuwanikisikia wakiyatoa dhidi ya chadema.nimekuwa nikiwasikia mitaani na kuyachukua nikayamwaga hapa jukwaani jinsi yalivyo.tusipuuze hoja zao kama tunakitakia mema chadema.
unaulizwa wanachi umekutana nao baa gani!?
 
Wewe unataka CDM iende kilege lege kama mgamba wenu? Lazima kuwe na mwelekeo na kamati kuu ndio final and conclusisive
 
Mkuu wangu FJM nimefurahi sana kwani umejibu hoja kikubwa na kwa usahihi kabisa, umeonyesha ukomavu wa CDM kwa kujibu fact nono zinazo pagusa kulekule kulipochokozwa. Ila naomba nami niongezee zege kidogo kwa ajili ya kufanya finishing ya majibu ya mada husika kupitia muongozo wa majibu yako makini kama ifuatavyo mkuu wangu:

1.Hapo Kwenye alama ya ***** Pia vijana walioenguliwa uchaguzi Bavicha ushahidi wa sababu za kuenguliwa ulishatolewa kupitia magazeti ukiainisha mchakato wote wa rushwa kupita Mpesa na Tigo uliofanywa na wahusika wote walioenguliwa.

2.Hapo kwenye alama ya ****** Ayo magenge yote ya story ya Arusha anayoyataja muandishi husika ndo wale watu 30 tu (na picha zilionyesha hapa JF) waliohudhuria shughuli ya kujipongeza kufanikisha muafaka feki yaani kale kashughuli kalichofanyika nje ya Ofisi ya Halmashauri ya Arusha mjini hivi majuzi???

3.Hapo kwenye alama ******* Sura za ya zamani inayopingwa ni Slaa kwa sababu amekua akionyesha matumaini mapya na imani kwa watanzania wengi wanaopenda haki. Sura hii ya Slaa(old wine in lattest bottle) inapingwa kwa sababu ni Mwiba kwa mafisadi ya nchi hii. Sera ya kujivua Gamba ni sera ya CCM haina nafasi CDM. Nape hafai kufananishwa na kijana yeyote ndani CDM kwani hasogei hata nukta moja, ukweli wake unajulikana na any reasonable man.

Daudi na kwa Wanajamvi,

Asante sana,Naomba sasa niweke record sawa...Mimi ni mmojawapo wa walioenguliwa Bavicha.Sina tuhuma na wala sijawahi kutoa wala kupokea rushwa katika mchakato ule.Kila mgombea alikuwa na tuhuma zake,lakini kuna kitu.....anyways ndiyo maana Mwanahalisi walipewa/walitoa habari ya kuwakashfu wagombea wote walioenguliwa ;Walitoka na heading Masalia ya Zitto yapukutishwa'. Hii sidhani kama ilikuwa bahati mbaya.Kwa bahati mbaya hilo halikuwazuia vijana kuwa na imani,na bado naendelea kuwa nao karibu kisiasa.wanajua kuchambua mambo kwa kina......hii ndiyo aina ya Demokrasia tuliyo nayo Tanzania na matumizi ya Media katika kuuwa demokrasia au kujenga Demokrasia,tutafakari.Nasizitiza sijawahi kuhusika kwenye Rushwa,Wengine siwezi kuwasemea.Kama ushahidi upo naomba sana niwajibishwe nipelekwe takukuru na hii itakuwa imetoa taswira nzuri kwa chama chetu na nitakuwa mfano na onyo lililo bora zaidi kwa wagombea wengine huko baadae ndani ya chama chetu.Nipo tayari kuwa mhanga wa hili ili chama changu kionyeshe dhamira ya dhati kabisa ya kupambana na ufisadi,rushwa kwa vitendo.

haya mambo ya kuchafuana kwenye media na majukwaa,tuyaache ni ulimbukeni wa kisiasa.Kila mmoja ana uwezo wa kwenda kwenye media,lakini ni kwa faida ya nani hasa?Hebu tuwe matured kidogo tuachane na hizi smearing campaign against each other,hii ni suicide pact,hii ni suicide attempt.Sitarudia tena.........

Hapo kwenye Red naona ni mwendelezo ule ule wa watu kutoa taarifa kwa ghiliba kwa madhumuni ya kuchafua watu tu.Ni mwendelezo wa udhaifu wa watu kuropoka hovyo na jitihada za kuhalalisha kinachofanyika.Nadhani hili nilishalieleza kwenye ile thread iliyoanzishwa baada ya kuenguliwa BAVICHA na nisingependa kuendelea kulijadili hapa ila sitavumilia kuona vijana na jamii ya watanzania wenye matumaini upinzani imara wakiendelea kupotoshwa aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya
 
nawaambia mnao - post humu chochote kile ambacho ni anti chadema; mnatafuta ugomvi jamvini.

Hapa wimbo ni kusifu chadema.

Ukisifu chadema; umeongea jema.

Ukikashifu ccm umeongea sawasawa.

Ila ukisifia/pongeza ccm au serikali na kubainisha changamoto za chadema; itakuwa unatafuta majibu ya kukosoa thinking yako.

In this forum.

Iq strong ni ile ya ku support chadema [hata kama itabainishwa changamoto; kufumbia moto changamoto hiyo na kukashifu ccm na serikali

iq dhaifu ni ile ya kusupport ccm na serikali na kubainisha changamoto za chadema.

Gr8 thinkers huwa wanapokea criticism na kutoa credit where necessary. If you cannot do that, then utajiita tu great thinker; kumbe tanker
ccm lekebisheni chama chenu kwanza mlikialibu wenyewe na sasa mnakazi ya kukitengeneza badala yake mnaharibu zaidi!
 
Shibuda katetea maslahi yapi ya wananchi? je umekusanya maoni ya wananchi wangapi ambao wanashangaa km unavyodai? usifanye hisia zako kuwa za wananchi wote!
 
Mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana CHADEMA, lakini tangu walivyomuua Chacha Wangwe moyo wangu umekasirika sana.

Acha mambo ya kivumi wewe; CDM waligeuka jini wakapindua gari au walifanyeje maana great thinker hatakiwi awe na imani za kishirikina kama wewe ndio maana tunatumia brain. Use your brain kufikiri acha mambo ya kimizizi!!!!!!!!!!!!
 
Mkuu wangu FJM nimefurahi sana kwani umejibu hoja kikubwa na kwa usahihi kabisa, umeonyesha ukomavu wa CDM kwa kujibu fact nono zinazo pagusa kulekule kulipochokozwa. Ila naomba nami niongezee zege kidogo kwa ajili ya kufanya finishing ya majibu ya mada husika kupitia muongozo wa majibu yako makini kama ifuatavyo mkuu wangu:

1.Hapo Kwenye alama ya ***** Pia vijana walioenguliwa uchaguzi Bavicha ushahidi wa sababu za kuenguliwa ulishatolewa kupitia magazeti ukiainisha mchakato wote wa rushwa kupita Mpesa na Tigo uliofanywa na wahusika wote walioenguliwa.

2.Hapo kwenye alama ya ****** Ayo magenge yote ya story ya Arusha anayoyataja muandishi husika ndo wale watu 30 tu (na picha zilionyesha hapa JF) waliohudhuria shughuli ya kujipongeza kufanikisha muafaka feki yaani kale kashughuli kalichofanyika nje ya Ofisi ya Halmashauri ya Arusha mjini hivi majuzi???

3.Hapo kwenye alama ******* Sura za ya zamani inayopingwa ni Slaa kwa sababu amekua akionyesha matumaini mapya na imani kwa watanzania wengi wanaopenda haki. Sura hii ya Slaa(old wine in lattest bottle) inapingwa kwa sababu ni Mwiba kwa mafisadi ya nchi hii. Sera ya kujivua Gamba ni sera ya CCM haina nafasi CDM. Nape hafai kufananishwa na kijana yeyote ndani CDM kwani hasogei hata nukta moja, ukweli wake unajulikana na any reasonable man.

NAOMBA NIKUITE BOSS,
Umeandika kirefu sana, lakini nikuulize swali, inawezekanaje mtu mwenye uwezo na bidii ya kuandika kirefu hivi akakosa uwezo na umakini wa kufuatilia jambo kiundani?
Pole sana, ningeweza kukusaidia tu namna ya kutoa taarifa hata kama ni za uzushi jitahidi uweke vitu vitakavyomfanya msomaji asumbuke sana kuvigundua kama sio vya kweli, lakini sio kama ulivyofanya, kukopy na kupaste mwanahalisi.
Mimi nilienguliwa saa chache kabla ya kupigiwa kura, je wajua kilichokuwa kinaendelea au unatamka kwa mujibu wa gazeti la mwanahalisi?
Usidhanie vijana wote tupo kwa ajili ya kuwafurahisha watu kwa dakika za uwanjani tu, ila gundua tupo kwa kuitafuta kesho ya jamii zaidi.
Nimekuwekea rangi ya kijani kwa kuwa chama fulani chenye rangi hiyo, kina aina hii ya matamshi na kutoa maneno yasiyofanyiwa utafiti, hivyo fuatilia ujue kwanza waliondolewa kila mmoja aliondolewa kwa sababu gani na waliobaki walibaki kwa sababu gani na walitajwa kwa tuhuma gani pia.
NIKUTAKIE SIKU NJEMA.
Ila ujue tu mimi sikujiunga chadema wakati wa kugombea bavicha, wala sijajiunga chadema baada ya kuona helkopita wala sijaitwa na mtu na vilevile sijakimbia ccm na kuja cdm.
Kwa hiyo ujue kabisa dhamira yangu ii wima na haitetereki kamwe!
Nilikwisha iahidi nafsi yangu kiapo, ni kiapo nisichoweza kukisaliti hadi niyalengayo yatimie ili nilipwe thawabu na Mungu na jamii inikumbuke kwayo.
 
Huku mitaani wananchi wameduwazwa na udikiteta unaoendelezwa na uongozi wa juu ndani ya chama hicho.Wamekuwa wakijiuliza iweje kila jambo viongozi watake kulitolea uamuzi?.Wananchi hapa mtaani wamekasirishwa na kitendo cha katibu wa CHADEMA kuonyesha usaliti wa demokrasia kwani amekuwa akihubiri kuwa serikali inahujumu demokrasia hapa nchini kumbe na yeye ndani ya chama chake hakuna demokrasia kabisa.Wananchi wamekuwa wakitolea mifano mambo kadhaa ambayo yamewahi kutokea ndani ya chama hicho na bado kikaendelea kuyafumbia macho huku suluhisho kikitoa vitisho vya kuwafukuza wanachama ambao wanaonekana kuhoji juu ya mwenendo ndani ya chama hicho.1.Wamekuwa wakikumbusha juu ya Zitto Kabwe alivyozuiwa na kikundi cha ati wazee wa chama asigombee uenyekiti na baadaye kuzushiwa mambo mbalimbali ikiwemo ati Zitto amenunuliwa na CCM nadhani tunayakumbuka haya kwani Zitto amepita katika kipindi kigumu mno.2.Pia, wananchi wamekuwa wakikumbushana juu ya lile tukio la Marehemu Chacha Wangwe alipohoji juu ya matumizi ya fedha za ruzuku ya chama kufaidisha watu wachache wa makao makuu huku ofisi za mawilayani na mikoa zikuwa katika hali mbaya kama sio taabani.Chacha Wangwe alizuliwa kashfa nyingi na kusema kwamba alikuwa amenunuliwa na CCM.Na alipotaka kutumia haki yake ya kidemokrasia kwa kutangaza kuwania uenyekiti ndani ya chama hicho mengi yalimkuta nadhani tunayakumbuka.3.Wananchi pamoja na wapenzi wa CDM wamekuwa wakizungumzia uchaguzi wa ndani ya chama hicho.Wanahoji iweje baadhi ya wagombea ambao hutoka katika mikoa isio ya Kilimanjaro na Arusha huenguliwa katika uchaguzi huo?.Wanatoa mfano wa kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea katika uchaguzi wa BAVICHA, wanasema udikiteta na upendeleo ndio ulitumika kuwaengua baadhi ya wagombea uenyekiti na kupitisha wale wasioweza kuhoji mwenendo wa mambo ndani ya chama hicho na si vinginevyo.Vijana wengi walidhani CDM ndio kimbilio lao kumbe wamebaini walipotea na sasa wameanza kusambaratika wengine juzijuzi tu wamejiunga na chama cha SAU na tumeona wamepewa ujumbe wa sekratirieti na wengine hivi karibuni tutawasikia NCCR-Mageuzi na CCM.4.Jambo lingine ambalo nimekuwa nikilisikia kwa wananchi mara kwa mara suala la Mh Shibuda.Hii kweli inaonesha kuwa no intra-party demokrasi CHADEMA.Yaani mbunge hapaswi kuwa na mawazo yake tofauti ndani ya Bunge.Hapaswi kupingana na wenzake hata kama wanazungumza pumba.Wananchi wamekuwa wakihoji iweje CDM imekuwa ikiponda CCM kuwa wabunge wake ni ndio mzee wakati wa kwao hawawapi fursa ya kutoa mawazo yao au kueleza bila kubughudhiwa na chama kile wananchoamini ni sahihi?.Hapa wananchi wengi wanaona CDM si mbadala wa CCM hata kidogo na mbadala hajazaliwa labda CCM yenyewe ipasuke vipande na hapo mbadala ndio utakuwepo na upinzani wa kweli sio wa Ze- Comedy utaonekana.Wanahoji hivi mbunge kutofautiana kidogo na msimamo wa chama chake ni dhambi?.Je mbunge alienda bungeni kusimamia maslahi ya chama au ya kwao wananchi?.Mimi mfanyabiashara hapa Arusha sina jibu labda wanachadema hasa viongozi wa juu wajitokeze na kujibu haya.5.Sasa jambo ambalo limetawala karibu magenge yote ya story hapa Arusha ni hili sakata la madiwani wa Arusha kukataa kupelekeshwa.Jambo hili limevuta hisia za watu wengi hapa na katika vyombo vya habari.Wananchi wamekasirishwa na kitendo cha viongozi wa CDM kuwatishatisha viongozi wao kwa kutaka kuwavua madaraka yao.Wananchi wengi sana hapa Arusha wanauliza hivi tulichagua viongozi hawa ikiwemo mbunge kutumikia chama au sisi wana Arusha?.Iweje chama kiwalazimishe madiwani wake kutanguliza maslahi ya chama badala ya maslahi yetu?.Sisi hatutaki vurugu kila kukicha ambazo zinapelekea kuuwawa kwa ndugu zetu.Wananchi wa Arusha wanataka amani ya kudumu sasa ili wajikite katika shughuli za maendeleo.Wananchi wengi wanaamini madiwani ambao wameshika vyeo hapa Arusha wakiongozwa na Naibu Meya Mh Estomih Mallah litakuwa suluhisho la mikwaruzo mingi ambayo imetokea hapa Arusha.Hivyo chama kuwalazimisha madiwani wavue vyeo walivyovipata kwa njia halali wakiongozwa na nia thabiti kabisa ya kujenga Arusha yetu ni kusaliti demokrasia na kuwasaliti wananchi waliowachagua kuungana na wale wa kutoka CCM ili kuleta maendeleo jijini.Hivyo, wananchi wanasema imefika wakati sasa kwa viongozi wa chadema kujivua gamba angalau ziwepo nyuso mpya zitakazoleta matumaini mapya.Na nyuso hizo ziwe za vijana atakaopambana na Nape wa CCM ambaye anaonekana kuwatishio sasa na viongozi waliopo sasa CDM wamezeeka na nguvu za kutawala jukwaa zinaisha.Pia, wanashauri utaratibu wa viongozi kupenda kuingilia mambo ya chini kama maamuzi yanayofikiwa na madiwani wao ukome kwani utakifanya chama kiondoke kwa wananchi na kubaki chini kuwa kampuni ya watu kama kilivyokuwa huko nyuma.Wanashauri structure ya chama ibadilishwa na maamuzi yawe yanafuata approach ya bottom-up badala ya sasa ya juu-chini.Wanasema utaratibu huu unalenga kuwatafutia umaarufu viongozi wa juu ili kila kitu waonekaneonekane na hawakotayari kuona mtu mwingine ndani ya chama akiibuka na kuwa maarufu zaidi yao.Wanasema udikiteta unakiua CHADEMA taratiiibu sawa na ugonjwa wa kansa kwa binadamu.Mie nimewasilisha kilio cha wananchi waliowengi wasioweza kufika hapa jamvini wadau!!!5.Wananchama wa CDM na watanzania kwa
Heko Siraji,unaonekana una upendo kuliko mshumaa kumulikia wengine!Lakin CDM hawaelewi na hawata elewa,kwani wamefungwa na minyororo ya msanii silaa na dj mbowe!! Hawatoki,werevu tu ndo watatoka kama siraji na mimi
 
Ujua maana ya udiketeta kweli, udikteta umejaa na kukithiri CCM na wala si CHADEMA
 
Kila wakati huwa tunamlalamikia Rais wetu kikwete kuto kutoa maamuzi mazito ambayo yamesababisha kambi mbalimbali ndani ya ccm. Chadema ipo imara ndiyo maana katibu anasimama na na kutoa maamuzi juu ya suala la arusha ili kuepusha ukwikwaji wa sheria na taratibu za chama.
 
Wewe mleta mada acha kukurupuka wewe eti wananchi ni wakina nani hao wananchi na wangapi??crap
 
Hujatueleza research yako uliifanya lini. Wakati unawasilisha mada kuhusu chama au taasisi yoyote ni bora upitie kwanza katiba na taratibu za uendeshaji, ngazi za mamlaka na maamuzi za tasisi na vyama husika.
 
Mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana CHADEMA, lakini tangu walivyomuua Chacha Wangwe moyo wangu umekasirika sana.
mimi mwenyewe nilikuwa naipenda sana ccm,lakini walivyo waua wale vijana pale nyamongo mgodini,moyo wangu umekasika sana tata.
 
Huku mitaani wananchi wameduwazwa na udikiteta unaoendelezwa na uongozi wa juu ndani ya chama hicho.Wamekuwa wakijiuliza iweje kila jambo viongozi watake kulitolea uamuzi?.Wananchi hapa mtaani wamekasirishwa na kitendo cha katibu wa CHADEMA kuonyesha usaliti wa demokrasia kwani amekuwa akihubiri kuwa serikali inahujumu demokrasia hapa nchini kumbe na yeye ndani ya chama chake hakuna demokrasia kabisa.Wananchi wamekuwa wakitolea mifano mambo kadhaa ambayo yamewahi kutokea ndani ya chama hicho na bado kikaendelea kuyafumbia macho huku suluhisho kikitoa vitisho vya kuwafukuza wanachama ambao wanaonekana kuhoji juu ya mwenendo ndani ya chama hicho.1.Wamekuwa wakikumbusha juu ya Zitto Kabwe alivyozuiwa na kikundi cha ati wazee wa chama asigombee uenyekiti na baadaye kuzushiwa mambo mbalimbali ikiwemo ati Zitto amenunuliwa na CCM nadhani tunayakumbuka haya kwani Zitto amepita katika kipindi kigumu mno.2.Pia, wananchi wamekuwa wakikumbushana juu ya lile tukio la Marehemu Chacha Wangwe alipohoji juu ya matumizi ya fedha za ruzuku ya chama kufaidisha watu wachache wa makao makuu huku ofisi za mawilayani na mikoa zikuwa katika hali mbaya kama sio taabani.Chacha Wangwe alizuliwa kashfa nyingi na kusema kwamba alikuwa amenunuliwa na CCM.Na alipotaka kutumia haki yake ya kidemokrasia kwa kutangaza kuwania uenyekiti ndani ya chama hicho mengi yalimkuta nadhani tunayakumbuka.3.Wananchi pamoja na wapenzi wa CDM wamekuwa wakizungumzia uchaguzi wa ndani ya chama hicho.Wanahoji iweje baadhi ya wagombea ambao hutoka katika mikoa isio ya Kilimanjaro na Arusha huenguliwa katika uchaguzi huo?.Wanatoa mfano wa kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea katika uchaguzi wa BAVICHA, wanasema udikiteta na upendeleo ndio ulitumika kuwaengua baadhi ya wagombea uenyekiti na kupitisha wale wasioweza kuhoji mwenendo wa mambo ndani ya chama hicho na si vinginevyo.Vijana wengi walidhani CDM ndio kimbilio lao kumbe wamebaini walipotea na sasa wameanza kusambaratika wengine juzijuzi tu wamejiunga na chama cha SAU na tumeona wamepewa ujumbe wa sekratirieti na wengine hivi karibuni tutawasikia NCCR-Mageuzi na CCM.4.Jambo lingine ambalo nimekuwa nikilisikia kwa wananchi mara kwa mara suala la Mh Shibuda.Hii kweli inaonesha kuwa no intra-party demokrasi CHADEMA.Yaani mbunge hapaswi kuwa na mawazo yake tofauti ndani ya Bunge.Hapaswi kupingana na wenzake hata kama wanazungumza pumba.Wananchi wamekuwa wakihoji iweje CDM imekuwa ikiponda CCM kuwa wabunge wake ni ndio mzee wakati wa kwao hawawapi fursa ya kutoa mawazo yao au kueleza bila kubughudhiwa na chama kile wananchoamini ni sahihi?.Hapa wananchi wengi wanaona CDM si mbadala wa CCM hata kidogo na mbadala hajazaliwa labda CCM yenyewe ipasuke vipande na hapo mbadala ndio utakuwepo na upinzani wa kweli sio wa Ze- Comedy utaonekana.Wanahoji hivi mbunge kutofautiana kidogo na msimamo wa chama chake ni dhambi?.Je mbunge alienda bungeni kusimamia maslahi ya chama au ya kwao wananchi?.Mimi mfanyabiashara hapa Arusha sina jibu labda wanachadema hasa viongozi wa juu wajitokeze na kujibu haya.5.Sasa jambo ambalo limetawala karibu magenge yote ya story hapa Arusha ni hili sakata la madiwani wa Arusha kukataa kupelekeshwa.Jambo hili limevuta hisia za watu wengi hapa na katika vyombo vya habari.Wananchi wamekasirishwa na kitendo cha viongozi wa CDM kuwatishatisha viongozi wao kwa kutaka kuwavua madaraka yao.Wananchi wengi sana hapa Arusha wanauliza hivi tulichagua viongozi hawa ikiwemo mbunge kutumikia chama au sisi wana Arusha?.Iweje chama kiwalazimishe madiwani wake kutanguliza maslahi ya chama badala ya maslahi yetu?.Sisi hatutaki vurugu kila kukicha ambazo zinapelekea kuuwawa kwa ndugu zetu.Wananchi wa Arusha wanataka amani ya kudumu sasa ili wajikite katika shughuli za maendeleo.Wananchi wengi wanaamini madiwani ambao wameshika vyeo hapa Arusha wakiongozwa na Naibu Meya Mh Estomih Mallah litakuwa suluhisho la mikwaruzo mingi ambayo imetokea hapa Arusha.Hivyo chama kuwalazimisha madiwani wavue vyeo walivyovipata kwa njia halali wakiongozwa na nia thabiti kabisa ya kujenga Arusha yetu ni kusaliti demokrasia na kuwasaliti wananchi waliowachagua kuungana na wale wa kutoka CCM ili kuleta maendeleo jijini.Hivyo, wananchi wanasema imefika wakati sasa kwa viongozi wa chadema kujivua gamba angalau ziwepo nyuso mpya zitakazoleta matumaini mapya.Na nyuso hizo ziwe za vijana atakaopambana na Nape wa CCM ambaye anaonekana kuwatishio sasa na viongozi waliopo sasa CDM wamezeeka na nguvu za kutawala jukwaa zinaisha.Pia, wanashauri utaratibu wa viongozi kupenda kuingilia mambo ya chini kama maamuzi yanayofikiwa na madiwani wao ukome kwani utakifanya chama kiondoke kwa wananchi na kubaki chini kuwa kampuni ya watu kama kilivyokuwa huko nyuma.Wanashauri structure ya chama ibadilishwa na maamuzi yawe yanafuata approach ya bottom-up badala ya sasa ya juu-chini.Wanasema utaratibu huu unalenga kuwatafutia umaarufu viongozi wa juu ili kila kitu waonekaneonekane na hawakotayari kuona mtu mwingine ndani ya chama akiibuka na kuwa maarufu zaidi yao.Wanasema udikiteta unakiua CHADEMA taratiiibu sawa na ugonjwa wa kansa kwa binadamu.Mie nimewasilisha kilio cha wananchi waliowengi wasioweza kufika hapa jamvini wadau!!!5.Wananchama wa CDM na watanzania kwa
Heko Siraji,unaonekana una upendo kuliko mshumaa kumulikia wengine!Lakin CDM hawaelewi na hawata elewa,kwani wamefungwa na minyororo ya msanii silaa na dj mbowe!! Hawatoki,werevu tu ndo watatoka kama siraji na mimi
 
Wanajamvi nimesubiri watu wa kujikita kwenye MADA amejitokeza mmoja tu.Wengi wao ni kuponda sasa nikirudi mtaani wananchi niwaambie nini zaidi ya kukitosa kabisa chama chao CHADEMA?.Udikiteta wanaozungumzia wananchi ndio naona umewatawala wapenzi wengi wa chama hiki ambacho namimi nilikuwa nakiamini lakini kwa menendo huu nami nakitosa.Hapa Arusha tuna matatizo mengi sana ya kimaendeleo.Tunachangamoto ya kudumisha heshima tuliopewa ya kuitwa JIJI (City) ndugu zangu hivyo itikadi za vyama tunakataa zisitutawale na kugawanywa na wanasiasa ambao inaonekana wanataka kututumia uwanja wa kujifunzia tunisianisation.Hatukubali nawaambia.Tumesubiri hatua ya kwanza ya CHADEMA kuwafukuza madiwani tuliowachagua sisi, hapo ndipo tutakapoanza kukifuta chama hicho mkoa wa Arusha.

TUNATAKA MAENDELEO ARUSHA NA SIO VURUGU NA MIGOGORO YA KISIASA.KAMA CHADEMA KINAHITAJI KUENDELEZA UTEMI HAPA A-TOWN BASI KITUHAKIKISHIE AMANI NA USTAWI MZURI WA MARIDHIANO NA SIO MIFARAKANO.

Bwana siraji, labda mimi sijakuelewa vyema unataka kusema wananchni wa Arusha walikutuma hapa JF? na kama hivyo ina maana Arusha hamna members wengine wa JF ni wewe peke yako tu!
 
Mimi mwenyewe nilikuwa napenda sana CHADEMA, lakini tangu walivyomuua Chacha Wangwe moyo wangu umekasirika sana.

We una akili kama ya Bwana mmoja anaitwa Steven Masatu Wassira a.k.a Tyson au ndio wewe Mkuu?

Wangwe aliuwawa na wale walioapa kuwa CCM nitakulinda mpaka kufa, walijuwa kuwa kifo cha wangwe kinge imaliza CDM lakini hawakujuwa kuwa bado wanaendeshwa na elimu ya zamani sana hawasomi na kuelimika kwenda na wakati na kuelekeza ulinzi wao kwa Taifa na hivyo kuapa Tanzania nitakulinda mpaka kufa, wakisha badili muelekeo wao kulinda Tanzania badala ya CCM then wanatakiwa pia kupata elimu ya kuelekeza mashambulizi yao katika akili na wala si roho wala mwili wa binadamu, hapo ndipo wanapokosea hadi sasa wanashambulia wrong target, "Philosophy never die".
 
Back
Top Bottom