PreGE2025 Wananchi Arusha mjini watishia kususia kupiga kura uchaguzi mkuu 2025, 'Mbunge ametudanganya kama watoto, tumechoka'

PreGE2025 Wananchi Arusha mjini watishia kususia kupiga kura uchaguzi mkuu 2025, 'Mbunge ametudanganya kama watoto, tumechoka'

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Baadhi ya wananchi katika mtaa wa Muriet kata ya Skokoni one mkoani Arusha wametishia kususia kupiga kura huku wakimtuhumu diwani wa kata hiyo na Mbunge wa Arusha mjini kwa kushindwa kutekeleza ahadi ya kujenga kivuko kinachounganisha zaidi ya kata tatu ikiwemo kata ya Muriet Sokoni one pamoja na Lemara.

Wananchi hao wameongeza kuwa kivuko hicho kilichojengwa kwa nguvu za wananchi kimeanza kuoza hivyo kuhatarisha usalama wa watumiaji ambapo kinapitisha zaidi ya watu 2000 kwa siku ikiwemo wanafunzi 300 wanaokwenda shule.

Pia soma RC Makonda: Migogoro iliyopo inazungumzika tusisubiri tatizo likatokea, tukapiga kelele dunia ikajua, tunajiumiza kwa kutoonekana kuwa na hekima
 
Kazini kwa Gambo kuna KAZI.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Back
Top Bottom