kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,425
- 7,211
Watu walimchagua magufuli kwa kura asilimia 84.3. Bahati mbaya Mungu kamchukua Magufuli.
Mama umesema kwa kauli yako mwenyewe wewe na Magufuli ni kitu kimoja.
Tunategemea kuona nchi ikiendeshwa kwa msingi uleule wa kutetea maslahi ya umma. Kupiga vita ufisadi na uzandiki wa kila aina. Kujenga moyo wa kujitegemea taifa na kutumia mali asili zake kwa faida ya wananchi.
Wapinga maendeleo na wachumia tumbo tunataka kuona wanadhibitiwa. Wameonyesha nia ya kurejea ulingoni ili kudhibiti siasa na uchumi.
Wanamapinduzi wanapinga maoni na hila za kubinafsisha mashirika ya umma yaliyosalia ambayo ni mhimili wa uchumi wa taifa.
Kinachotakiwa kwenye mashirika hayo ni uongozi wenye weledi na uzalendo. Kuwaweka wafanya biashara wakubwa kwenye bodi na management za mashirika ya umma sio suluhisho maana kuna conflict of interest.
Wanamapinduzi ndani ya Chama cha Mapinduzi watahakikisha mama anabakia kwenye njia ya kimapinduzi ya Magufuli.
Alisema mwenyewe na Magufuli ni kitu kimoja.
Mama umesema kwa kauli yako mwenyewe wewe na Magufuli ni kitu kimoja.
Tunategemea kuona nchi ikiendeshwa kwa msingi uleule wa kutetea maslahi ya umma. Kupiga vita ufisadi na uzandiki wa kila aina. Kujenga moyo wa kujitegemea taifa na kutumia mali asili zake kwa faida ya wananchi.
Wapinga maendeleo na wachumia tumbo tunataka kuona wanadhibitiwa. Wameonyesha nia ya kurejea ulingoni ili kudhibiti siasa na uchumi.
Wanamapinduzi wanapinga maoni na hila za kubinafsisha mashirika ya umma yaliyosalia ambayo ni mhimili wa uchumi wa taifa.
Kinachotakiwa kwenye mashirika hayo ni uongozi wenye weledi na uzalendo. Kuwaweka wafanya biashara wakubwa kwenye bodi na management za mashirika ya umma sio suluhisho maana kuna conflict of interest.
Wanamapinduzi ndani ya Chama cha Mapinduzi watahakikisha mama anabakia kwenye njia ya kimapinduzi ya Magufuli.
Alisema mwenyewe na Magufuli ni kitu kimoja.