Tonge
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 695
- 12
Nimechoshwa na ubabaishaji wa wabunge waliopita na aliyepo wa CCM, Shekifu kawa mbunge kwa vipindi viwili lushoto lakini bado huduma kwa jamii kama maji, shule, zahanati na barabara sio nzuri na awamu hii yupo Mshangama nae hakuna analofanya zaidi ya kusinzia bungeni na kuiacha wilaya hii ambayo ina rasilimali nyingi kama utalii na misitu ikiendelea kuwa nyuma kimaendeleo.
Mfano, haiwezekani wilaya kama hii yenye kuzalisha matunda mengi haina hata kiwanda cha kusindika hayo matunda, si hivyo tu bali hakuna sekondari za kutosha kukidhi mahitaji ya wanafunzi wanaofaulu, swala la barabara na lenyewe halifai, tangu wajerumani waweke lami barabara toka mombo hadi lushoto mjini basi hakuna tena barabara ya lami kuelekea maeneo mengine kama mlalo na kwekanga tena yenye vivutio na uwekezaji kama hotel, utalii wa mazingira n.k.
Kwa haya na mengine mengi NATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA KWENYE JIMBO HILI ILI NIWEZE KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI WA LUSHOTO.
Naomba mniunge mkono wanaJF wenzangu. Aksanteni.
Mfano, haiwezekani wilaya kama hii yenye kuzalisha matunda mengi haina hata kiwanda cha kusindika hayo matunda, si hivyo tu bali hakuna sekondari za kutosha kukidhi mahitaji ya wanafunzi wanaofaulu, swala la barabara na lenyewe halifai, tangu wajerumani waweke lami barabara toka mombo hadi lushoto mjini basi hakuna tena barabara ya lami kuelekea maeneo mengine kama mlalo na kwekanga tena yenye vivutio na uwekezaji kama hotel, utalii wa mazingira n.k.
Kwa haya na mengine mengi NATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE KWA TIKETI YA CHADEMA KWENYE JIMBO HILI ILI NIWEZE KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI WA LUSHOTO.
Naomba mniunge mkono wanaJF wenzangu. Aksanteni.