Wanajamvi nimeng'atwa na nyoka

Wanajamvi nimeng'atwa na nyoka

Nipo hospitali nimehudumiwa na kupatiwa kitanda nimetundikiwa maji baada ya sindano mbili. Nilikua nmevaa sandals usiku huu natoka kupaki gari jirani tu na napokaa. Naendelea vyema

Pole sana mkuu,tunashauriwa kutokuwa na vichaka majumbani kwetu..Hata kama kuna maua jitahidi kupluni mara kwa mara,Sasa kama hujamuona maana yake ni kwamba anaishi maeneo ya hap!Pole sana
 
Duh...! Kijana pole sana, kumbe mitaa ile kuna nyoka?

Aisee yaani kaniotea natoka kupark gari palepale pa cku ile akanikong'oli,ikabidi nirudie gari kuwahi hospital ndo nipo bado namalizia drip ya mwisho,nadhani mida ya sa 6 ndo inaisha nirudi hm
 
Pole sana mkuu,tunashauriwa kutokuwa na vichaka majumbani kwetu..Hata kama kuna maua jitahidi kupluni mara kwa mara,Sasa kama hujamuona maana yake ni kwamba anaishi maeneo ya hap!Pole sana

Ni kweli mkuu sema nimeng'atwa mbali kidogo na hm ni barabarani tu sema pembeni kweli kuna vichaka kidogo nadhani ndo alikokimbilia
 
Wanajamvi nimeruhusiwa ndio natoka hospital mda huu saa 7 dak 5 hivi..nawashukuru sana kwa maombezi yenu na faraja zenu. God bless u all abundanly
 
  • Thanks
Reactions: Paw
Pole sema inategemeana na aina ya nyoka, kuna wengine wskisha kuuma optional pekee ni kukatwa either mguu
 
nyoka wakubwa hawang'ati unyayo wala kisigino ,wanapiga kuanzia magotini kwenda juu,pole mkuu

Hawa sasa watakuwa wanakiuka masharti waliyopewa Enzi za Adam name eva!!!kwamba sie tuwatifue za utosi na wao watafune visigino!!! .....i
Ugua pole mkuu
 
Wanajamvi nimeruhusiwa ndio natoka hospital mda huu saa 7 dak 5 hivi..nawashukuru sana kwa maombezi yenu na faraja zenu. God bless u all abundanly
Pole sana. Inabidi mumsake huyo nyoka asije akaleta madhara zaidi.
 
Pole sema inategemeana na aina ya nyoka, kuna wengine wskisha kuuma optional pekee ni kukatwa either mguu
Duh ni kweli especially ukichelewa sana matibabu,halafu dokta jana pia aliniambia kufunga kamba sehem ulong'atwa pia ni hatari eti ndio inaweza kupelekea mguu kukatwa akashauri ni vyema mtu ukakimbilia matibabu mapema,mi mguu umevimba sana nadhani sababu ya kufunga ili sumu isisambae ile baada ya kung'atwa
 
Pole sana mkuu, natumaini wamekudunga sindano ya anti venom. Pia kila wakati endelea kunywa mkojo wako, ni tiba nzuri sana ya kuondoa sumu. Kunywa maji mengi sana ili ukojoe mara kwa mara, inasaidia. Sema ni kwa vile ilikuwa ni usiku, kama ni mchana make sure unajua rangi ya nyoka i.e kuweza kuelezea maumbile yake. Kuna lile jiwe la nyoka hivi wanauza wapi DSM? Dr. MziziMkavu njoo huku uje utoe tiba ushauri kwa mtu aliyeumwa na Nyoka.
 
Back
Top Bottom