Nakumbuka za mani kulikuwa na Yale mawe meusi unachanja then unabandika linanasa mpaka sumu ikiisha linadondoka, asubuhi unalidumbukiza kwenye maziwa fresh kutoa sumu then linakuwa ready kwa Matumizi mengine. Hebu tuelezane first aid jamani seriously wengi tumehamia makazi mapya. Mkojo ni tiba? Sometimes distance to the hospital plus traffic can be very challenging
Mkuu hilo la mkojo sijawahi kulisikia kwenye huduma ya kwanza kwa mtu aliyengatwa na nyoka.
katika ulimwengu wa sasa uliojaa magonjwa,unaweza kusababisha tatizo kubwa wakati unajaribu kutatua tatizo dogo.
Asilimia kubwa ya nyoka hawana sumu,ila nao wanagonga.wenye sumu wakigonga huacha alama za meno mawili yaliyotoboa,ie utakuta panatoa damu.
na hao wenye sumu,wako makundi matatu(sumu inayoingia kwenye nyama,sumu inayoingia au kusafiri kwenye damu na sumu inayosafiri kwenye nerve system(akina na black/green mamba))
wale wa kundi la kwanza sumu yao huwa inatend kuozesha sehemu iliyoathiriwa(nyama/misuri);kundi la pili ndo hao sumu inatembea kwenye damu na kundi la tatu hawa sumu yao inaua haraka sana yaani ndani ya madakika lakini hawa mara nyingi wapo maporini siyo mjini.
Huduma ya kwanza ni kumfanya mgonjwa asipanic(assurance) hii inazuia kama ni sumu inayotembea kwenye damu,basi moyo wa mtu aliyepanic huenda mbio na hivyo damu hukimbia haraka na hivyo kusambaza damu/sumu haraka. Usifunge kiungo kilichoathiriwa na endapo utafunga,basi uwe unafungua kila baada ya dakika walau 30. ili kufanya damu ifike na kupeleka oksijeni kwenye kiungo hicho.kama kiungo kilichogongwa ni mkono uninginize ili damu inayorudi kwenye moyo iwe na resistance ya kupanda badala ya kuuinua juu.kama ni mguu kaa endelea kuuninginiza.
Lakini hizi ni huduma ya kwanza tu,lazima utaratibu wa haraka wa kumpeleka mgonjwa hospitalini unafanywa au fanya hayo huku mgonjwa akiwa kwenye chombo cha usafiri kumpeleka hospitalini.Jitahidi kupata usafiri badala ya kwenda hospitali kwa mguu au mgonjwa abebwe.Kama ulivyotaja kijiwe unaweza kitumia lakini nacho kama huduma ya kwanza huku unampeleka mgonjwa hospitalini.
haya ndio ninayoyajua tuendelee kuchangia.