TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,502
- 11,248
Wanajamii kuna kisa kimoja kimemtokea rafiki yangu na kwa kweli amebaki kuchanganyikiwa. Kisa chenyewe ni kuwa jamaa ni ana rafiki yake wa kike (raia wa nchi nyingine) ambaye wanasoma naye na wapo karibu sana ingwa siyo wapenzi na wala hawajahi kuwa wapenzi wala ku-do.Huyu binti ana boyfriend wake na wanafahamiana vyema na huyu rafiki yangu, tena maelezo ya binti ni kuwa anategemea kuolewa na huyo boyfriend wake kwa kuwa wanatokea nchi moja na wanapendana.
Sasa kilichomtokea jamaa kwa kuwa wanakaribia kumaliza masomo kisha kila mmoja arejee nchini kwake, binti amemfata jamaa na ombi la kumpatia zawadi ambayo itakuwa kumbukumbu na kwa mujibu wake zawadi ya mimba itamfaa zaidi kwa maelezo kuwa huyu rafiki yangu ni mtu mwema sana na ni kijana mtulivu asiye na makuu na pia ana akili za darasani na hata za maisha hivyo anataka apate mtoto ambaye atakuwa na sifa kama za jamaa ili iwe kumbukumbu yake ya kudumu manake wanaweza wasionane tena.
Huyu mtu ni caring sana kwa kweli kiasi kwamba inapotokea binti akikwaruzana na bwana wake kimbilio lake kubwa ni kwa huyu rafiki yangu na hata bwana wa binti mwenyewe anamuheshimu sana huyu jamaa. Ila kwa hili la mimba anajihisi kuchanganyikiwa na amekuja kwangu kuomba ushauri. Hivyo wadau naomba mawazo angalau nipate pa kuanzia ili kumsevu mwana jamii mwenzetu.
Sasa kilichomtokea jamaa kwa kuwa wanakaribia kumaliza masomo kisha kila mmoja arejee nchini kwake, binti amemfata jamaa na ombi la kumpatia zawadi ambayo itakuwa kumbukumbu na kwa mujibu wake zawadi ya mimba itamfaa zaidi kwa maelezo kuwa huyu rafiki yangu ni mtu mwema sana na ni kijana mtulivu asiye na makuu na pia ana akili za darasani na hata za maisha hivyo anataka apate mtoto ambaye atakuwa na sifa kama za jamaa ili iwe kumbukumbu yake ya kudumu manake wanaweza wasionane tena.
Huyu mtu ni caring sana kwa kweli kiasi kwamba inapotokea binti akikwaruzana na bwana wake kimbilio lake kubwa ni kwa huyu rafiki yangu na hata bwana wa binti mwenyewe anamuheshimu sana huyu jamaa. Ila kwa hili la mimba anajihisi kuchanganyikiwa na amekuja kwangu kuomba ushauri. Hivyo wadau naomba mawazo angalau nipate pa kuanzia ili kumsevu mwana jamii mwenzetu.