Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
Hapa JF kuna unafiki wa hali ya juu kabisa. .....
Hapa JF kuna unafiki wa hali ya juu kabisa. Kila leo watu mnasisitiza uhuru wa kujieleza / kutoa maoni nakadhalika. Leo vijana wameamua kujiunga na CCM, mnawasema vibaya kana kwamba nyie ndiyo mlioshika funguo za uhuru wao. Kwenda CCM siyo njaa ni matumizi ya uhuru wao kama vile nyie mnavyotumia uhuru wenu wa kujieleza.
Mkuu punda kunani kuipondea JF kila mtundiko wako?
Kwanza ulianza kwa kuhoji credibility yetu, leo unahoji unafiki, kulikoni? Watu tuna fikira anuwai hapa.
Huo uhuru wa kutoa na/ama kupokea mawazo/maoni unaousema hapo juu ndio huo wanaoutumia hao wanaowashangaa wanafunzi wa vyuo kujiunga na sisiemu, sasa kosa lao lipi? Wanasema yale yaliyo moyoni mwao bila kificho. Kama wana mtazamo tofauti na unavyofikiri wewe basi ni halali yao, JF inaruhusu, na kama haitoshi katiba ya nchi inaruhusu jambo hilo! Wewe unaishi dunia ipi mkuu?Ndio jambo forums ilivyo, ina watu wa kila namna.
Hebu soma vizuri masharti ya kujiunga na JF pale ukurasa wa mbele, huenda ukaelimika na kuelewa hiki ninachokiandika hapa, kwa sababu wamefafanua kwa undani sana.
Tuendelee kulumbana!
Kama ni kweli alishindwaje kuwasaidia wanafunzi waliokuwa Ukraine tayari na walianza kusoma baada ya mwaka moja akawatelekeza. AIBU HIYO JK, WEWE ULISOMESHWA KWA PESA YA WALIPA KODI.
Wangekuwa wamehamia upinzani hapo ingekuwa news au?
Anyway, wanafunzi wa vyuo vikuu huwa sielewi kabisa mambo yao.
Walivaa kijani na njano Diamond baada ya kufatwa na magari kutoka vyuoni, wakachukua kadi za ccm kibao, wiki iliyofuata walewale wakaandamana kwenda jangwani na kashfa kibao dhidi ya serikali kwa kushindwa kutekeleza habari yao ya mikopo.
Leo tena wanasifia na hapohapo anapouliza mtu asiyeridhishwa na mwenendo wa mikopo anashangiliwa, hiyo inatoa picha gani?
Na wao wameamua kuleta ushkaji na serikali ya kishkaji?
Acheni jamani wajiamulie.
CCM hoyeee! CCM juu juu juu zaidi!
if they keep beating you, why not join them?
bad news. we need a new technique to make these guys aware of themselves.
....njaa nyingine hii!
Hapa JF kuna unafiki wa hali ya juu kabisa. Kila leo watu mnasisitiza uhuru wa kujieleza / kutoa maoni nakadhalika. Leo vijana wameamua kujiunga na CCM, mnawasema vibaya kana kwamba nyie ndiyo mlioshika funguo za uhuru wao. Kwenda CCM siyo njaa ni matumizi ya uhuru wao kama vile nyie mnavyotumia uhuru wenu wa kujieleza.
Jamani tulieni kidogo, hivi mtu akiamua kujiunga na chama anachokipenda ni kwa sababu ya njaa?!!! mbona huko CCM wapo maprofessa wengi wamepelekwa na njaa? Je Professa Wangwe ana njaa yoyote?...
Wametimiza haki zao jamani, tuwaache hao!!! naona FD amefurahi... sibiri sunami 2010,,, Mnyika atakuwa Prof. Tayari
si 1000 tu,,, wengine sijui 50,000 si wako upinzani? sasa tatizo nini?
Unajua mkuu, kinachobishaniwa hapa ni kwamba, ni hivi majuzi tu hapa wanafunzi hawa hawa walikuwa wanaandamana kupinga serikali ya kishikaji na chama chake, ambavyo vimewasahau kwa kutowapa mikopo ambayo raisi aliahidi,leo ndio hao hao tena wanapokea kadi za chama ambacho walikiponda pamoja na serikali yake.Mgongano wa hoja na mawazo ndio unakuja hapa haswa. Kwamba, iweje hawahawa ndio waliponda chama majuzi na leo wanapokea kadi kwa chama hicho hicho? Nini kimewabadilisha mawazo ghafla?
Ugumu wa kufikiri unakuja hapa haswa mkuu.
Tuendelee kulumbana.
una uhakika wanafunzi wote waliprotest siku hiyo au ni baadhi ya wanafunzi ? unajuaje kama wanafunzi waliojiunga na ccm waliprotest ?
Nadhani ushauri kwenye Network yangu unafanya kazi.
Nimewaagiza vijana wasicheze mbali na system naona agizo langu linatekelezwa kwa vitendo.
Strategy za kupambana ni nyingi sana ndiyo maana ndani ya CIA kuna KGB na ndani ya KGB kuna CIA.
Hata kama sio wote walishiriki maandamano, lakini ni wote walisimamishwa masomo kwa kutokuingia darasani. Kwa hiyo basi, athari za wachache zinawakumba na wasiokuwemo.
lakini hapa sikumaanisha chochote juu ya WALIOSIMAMISHWA masomo, nilikuwa nikiongelea WALE WALIOJIUNGA NA CHAMA CHA MAPINDUZI !!