Daudi Mchambuzi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 62,190
- 128,264
Hakuna namna nyingine zaidi ya kuisoma namba.
Acha kumuhusisha Mungu, walipewa nafasi wakaichezea. Hapa ni mbele kwa mbele wataisoma namba...
Waende ofisi za ccm wakaulize mkopo vipi
Sasa mnataka HESLB hiyo hela wainye? Msiwaonee bwana, tena kuna mimwanafunzi mingine ya chuo kikuu inashabikia sana ccm wacha yaisome namba!! Naiomba serikali fedha kidogo iliyobakia Hazina ielekezwe kwenye afya, huku wazazi wataweza tu kuwasomesha watoto wao!! HAPA KAZI TU!!HESLB inabidi wawajibike, inaoneka hawako makini !!.
Nafikiri njia rahisi ya demokrasia ya kweli ni kura ya wazi kwani haina utata wala matokeo hayachelewi kwani mtu wa mwisho anapohesabiwa tu na matokeo tayari na hakuna cha kulinda kura wala nini - sehemu ya kupangia mistari ni barabara za mitaa na kubwa.
Wala usipoteze muda kudhani serikali ya CCM ina mpango kabambe wa kushughulikia hii kitu. Magufuli na CCM kwenye kampeni zao walisema wazi kabisa Elimu ya bure mwisho ni Form Four, suala la Elimu ya Chuo kikuu sio agenda yao ya msingi na wala sio kipaumbele chao cha kwanza.Mimi ni mhanga na tayari nilisharipoti Mkwawa university Iringa, kwa kweli serikali isipolishughulikia swala hili, tutaumia sana na kukata tamaa na masomo ya elimu ya juu
Jamani kuweni wapole, mliletewa maembe nyie mkapenda malimao sasa kelele za nini? Baba zenu na mama zenu si ndo walikuwa wanashiriki kuimba zile nyimbo za "waacheni waandamane ehhhhheeeee ccm mbele kwa mbele?" Sasa mayowe ya nini? Kwanza serikali ya ccm haina sera ya elimu bure kwa chuo kikuu, hivyo kuweni wapole mpaka mwakani serikali itakapopata fedha. Kwa sasa hivi fedha nyingi imeenda kwenye kampeni za Magufuli, hivi mnafikri yale mat-shirt mliyokuwa mnavaa yamepatikana bure? In short hazina haina hela, hivyo anayeweza kuendelea kusubiri avute subira na asiyeweza kusubiri ahamie Rwanda.