Wanaenda shule saa ngapi hawa?

Wanaenda shule saa ngapi hawa?

Manyanza

Platinum Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
19,946
Reaction score
45,572
jamani wana JF!
kuna jambo linanitiza sana hapa, kuna maduka yanayouza nguo hapa Mwenge maarufu kwa Boutique ukiingia maduka haya utakutana na vijana wa kiume age yao ni miaka 14-17 wanauza nguo katika hayo maduka, ingawa mimi sio mkaaji sana wa dar es salaam lakini mara nyingi kila week end huwa nakuja Dar na ni lazima nipite angalau madukaa kadhaa kuangalia nguo, viatu na vitu vingine vinavyonifaa na katika maduka 7 utakayoingia maduka manne lazima utakuta hao machalii wanapiga business.. mara ya kwanza nilidhani ni week end tu, kumbe sivyo week hii nimefanya utafiti kuanzia jumatano mpaka ijumaa na kugundua hawa machalii wapo full time.
jamani hawa madogo wanasoma saa ngapi?
ina maana wenye maduka wameridhika na hiyo hali ya kuwaweka machalii katika maduka yao bila kuwapeleka shule?
jamani naomba hili tulitafakari sote kama watanzania tunaotaka kujikomboa kutoka katika ujinga.
 
Wakibosho hao shule kwao siyo muhimu pesa kwanza!
 
Ishauri serikali yako kwanza, irekebishe miuundo mbinu mashuleni na iweke walimu watoa elimu na c wauza maandazi na visheti., labda walau we mwenze2 ushauri wako unaweza kupata bahati ya kufanyiwa kazi.
 
Ishauri serikali yako kwanza, irekebishe miuundo mbinu mashuleni na iweke walimu watoa elimu na c wauza maandazi na visheti., labda walau we mwenze2 ushauri wako unaweza kupata bahati ya kufanyiwa kazi.
Mkuu!Serikali sio kwamba haisikii wala haioni, kuna mashirika na NGOs kama Haki Elimu zinafikisha ujumbe stahiki kwa serikali na wadau wote wa elimu, na nadhani wewe umetoka nje ya mada kabisa au na wewe ni mmliki wa yale maduka na umeajiri wale machalii?Kusema kweli inasikitisha sana kuona watoto wadogo kama wale wapo madukani badala ya mashuleni. Ingawa katika nchi yetu kuna watoto wengi ambao wapo mitaani lakini hawa wanaouza maduka pale Mwenge huwa wananisikitisha sana!
 
Angalieni na upande wa pili.umeshawahi kuwauliza hao madogo kwanini hawaendi shule?kuna madogo wameshindikana hata wapewe nini.wao wanaona kuwa na kahela kidogo mfukoni ni bora kuliko kukaa class
 
serikali iangalie hili,nilipita Moshi na Arusha hili lipo,vijana wa kipare wakimaliza shule kazi ya kwanza ni kuuza magazeti na shoeshine,na walivyo wafupi.....
 
jamani wana JF!
kuna jambo linanitiza sana hapa, kuna maduka yanayouza nguo hapa Mwenge maarufu kwa Boutique ukiingia maduka haya utakutana na vijana wa kiume age yao ni miaka 14-17 wanauza nguo katika hayo maduka, ingawa mimi sio mkaaji sana wa dar es salaam lakini mara nyingi kila week end huwa nakuja Dar na ni lazima nipite angalau madukaa kadhaa kuangalia nguo, viatu na vitu vingine vinavyonifaa na katika maduka 7 utakayoingia maduka manne lazima utakuta hao machalii wanapiga business.. mara ya kwanza nilidhani ni week end tu, kumbe sivyo week hii nimefanya utafiti kuanzia jumatano mpaka ijumaa na kugundua hawa machalii wapo full time.
jamani hawa madogo wanasoma saa ngapi?
ina maana wenye maduka wameridhika na hiyo hali ya kuwaweka machalii katika maduka yao bila kuwapeleka shule?
jamani naomba hili tulitafakari sote kama watanzania tunaotaka kujikomboa kutoka katika ujinga.


Labda hao wanaenda shule za usiku!
 
Mkuu!Serikali sio kwamba haisikii wala haioni, kuna mashirika na NGOs kama Haki Elimu zinafikisha ujumbe stahiki kwa serikali na wadau wote wa elimu, na nadhani wewe umetoka nje ya mada kabisa au na wewe ni mmliki wa yale maduka na umeajiri wale machalii?Kusema kweli inasikitisha sana kuona watoto wadogo kama wale wapo madukani badala ya mashuleni. Ingawa katika nchi yetu kuna watoto wengi ambao wapo mitaani lakini hawa wanaouza maduka pale Mwenge huwa wananisikitisha sana!
toka imeanza kufikishiwa habari ni lini mpaka leo na kilichofanyiwa kazi kina ukubwa gani? (namaanisha kasi yake ktk kutatua tatizo) Sana sana wakiwekewa jumbe zinazo wachoma wanaanza hadi kuzitishia hizo NGO's. Upande wapili nimeshikwa na mshituko!!! kuona unatoa masikitiko tena yenye huzuni kwa wenye nafuu.(hao walio mwenge) vp kuhusu watoto we2 na wadogo ze2 wanao lala kwenye mitaro na kuomba misaada barabarani? Vp wale wanao hudhuria masomo, madawati kwao ni mawe na vpande vya tofali, mwisho wasiku wakifeli ndo'wanakuja mwenge, we ndo'unaonesha kuumia kwa kuja kwao mjini huku ukisahau chanzo. Ubarikiwe kwa hisia zako uongozi wa nchi yako. Aimeen!
 
Labda hao wanaenda shule za usiku!
Yawezekana mkuu wanapiga evening Class, lakini jana nimezunguka madukani mpaka saa mbili usiku na bado walikuwa wanaendelea na business kama kawa!
 
toka imeanza kufikishiwa habari ni lini mpaka leo na kilichofanyiwa kazi kina ukubwa gani? (namaanisha kasi yake ktk kutatua tatizo) Sana sana wakiwekewa jumbe zinazo wachoma wanaanza hadi kuzitishia hizo NGO's. Upande wapili nimeshikwa na mshituko!!! kuona unatoa masikitiko tena yenye huzuni kwa wenye nafuu.(hao walio mwenge) vp kuhusu watoto we2 na wadogo ze2 wanao lala kwenye mitaro na kuomba misaada barabarani? Vp wale wanao hudhuria masomo, madawati kwao ni mawe na vpande vya tofali, mwisho wasiku wakifeli ndo'wanakuja mwenge, we ndo'unaonesha kuumia kwa kuja kwao mjini huku ukisahau chanzo. Ubarikiwe kwa hisia zako uongozi wa nchi yako. Aimeen!
Thanks mkuu!Najua moja ya matatizo sugu katika sekta ya elimu ni hayo uliyoainisha hapo juu na wakati mwingine mazingira ya shule zetu sio rafiki.Mimi kwa upande wangu nilikuwa nawasilisha mawazo na hisia zangu, lakini sina hatua zozote za kuchukua maana kama wadau katika sekta ya elimu wameshapiga sana kelele na serikali imeziba masikio....
 
kwa wamiliki wa hizo biashara ni faida maana hawana gharama sana ktk kuwalipa ujira wao ukizingatia hawana majukumu makubwa na wanakaa nao, hii inawafanya wamiliki kuwasaka hawa kwa udi na uvumba na ikiweka sheria kali itakayowabana waajiri na ikafuatiliwa kwa makini inaweza kupunguza hili.
 
serikali iangalie hili,nilipita Moshi na Arusha hili lipo,vijana wa kipare wakimaliza shule kazi ya kwanza ni kuuza magazeti na shoeshine,na walivyo wafupi.....

na wengine ndio wanakuja Dar kuuza maduka ya nguo, ama kweli mimi nashangaa serikali sijui inalichukuliaje hili suala maana watoto kama wale walipaswa kuwa shule lakini muda wao sasa wanautumia kufanya kazi.
viongozi wetu nao wanatoa kipaumbele kwenye kilimo badala ya elimu, kweli nchi hii ina safari ndefu katika kufikia maendeleo ya kweli.
 
Back
Top Bottom