Technician
JF-Expert Member
- Mar 30, 2010
- 841
- 222
na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango Dodoma, Chuo cha Maadili Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo Tengeru na Chuo cha Uhasibu Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.
NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango Dodoma, Chuo cha Maadili Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo Tengeru na Chuo cha Uhasibu Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.
NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.