Wanachuo 300 wajiunga CHADEMA

Technician

JF-Expert Member
Mar 30, 2010
841
222
na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango – Dodoma, Chuo cha Maadili –Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo – Tengeru na Chuo cha Uhasibu –Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.


NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.
 
na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango – Dodoma, Chuo cha Maadili –Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo – Tengeru na Chuo cha Uhasibu –Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.


NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.

kuna shule moja ya msingi vitoto vinalazimishwa kuvaa fulana za njano na scurf za kijani. CCM wanasahau kuwa hao ni watoto na wadogo zetu sisi tulioko vyuoni.
 
my MP lema,,, im proud ov u... Piga kazii,,, tafuta wanachama wa kutosha,,mabadiliko nchini tanzania yamabakia kuletwa na CHADEMA tu,, God Bless CHADEMA
 
naona CHADEMA inajaa wasomi, vizuri sana, hawa watumike kuelimisha jamii kwenye masuala tofauti, itasaidia kutukomboa kwenye umaskini, watu watafanya maamuzi kwa vitu wanavyo vijua na kuvielewa kwa undani, sio kuburuzwa tu!
 
CCM ndo washarikoroga yakhe! Zege ukishalichanganya haliwezi kurudi kuwa cement tena. Hicho ni kifo cha CCM na kaburi lao nawaandalia mimi mwenyewe ili siku ikifika tukawalaze mahali pabaya peponi.
 
Amina! I mean na iwe hivyo, CDM kaza uzi mpaka tuhakikishe ccm ikigusa uzi huo inajikata!! Kifo cha ccm kishakaribia, Heko kwa kijana wetu Lema na Nassari endeleeni na huo moto nasi tupo nyuma yenu kuchochea zaidi, tunataka chama kwanza kitishe kwa kuwa na wasomi zaidi. Naiona Tumaini Universities inakuja kwa kasi ya ajabu kutaka mapinduzi ya nchi hii, Sie Makamanda wa Makumira tushafungua tawi na karibu lina wanachama 500. Big up CDM!
 
CHADEMA endelezeni mashambulizi ili mafisadi wazidi kuchanganyikiwa zaidi...
 
Amina! I mean na iwe hivyo, CDM kaza uzi mpaka tuhakikishe ccm ikigusa uzi huo inajikata!! Kifo cha ccm kishakaribia, Heko kwa kijana wetu Lema na Nassari endeleeni na huo moto nasi tupo nyuma yenu kuchochea zaidi, tunataka chama kwanza kitishe kwa kuwa na wasomi zaidi. Naiona Tumaini Universities inakuja kwa kasi ya ajabu kutaka mapinduzi ya nchi hii, Sie Makamanda wa Makumira tushafungua tawi na karibu lina wanachama 500. Big up CDM!
namba nzuri sana ukizingatia limefunguliwa juzi juzi tu endeleeni kuhamasisha sijui kwanini wasomi kama nyie muendele kubaki CCM...
 
na bado. safari hii tutafika hadi secondary school. vijana wanatuhitaji sana huku. buriani ccm.
 
Ujumbe huu ni mahususi kwa wabunge wote wa CHADEMA bila kujali jinsia au njia walioingilia bungeni iwe ya kuchaguliwa au kuteuliwa.
Kila mbunge ahakikishe anapata wanachama wapya kwa ushawishi wa aina yeyote.
HII NDO KAZI YA MBUNGE
 
na Grace Macha, Lushoto
HARAKATI za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) za kujiwekea ngome kwenye vyuo vya elimu hapa nchini zimezidi kushika kasi baada ya wanachuo wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Sebastian Kolowa (SEKUCO) zaidi ya 310 kujiunga na chama hicho.
Wanachuo hao walikabidhiwa kadi za CHADEMA juzi na mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ambaye pia ni mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, wakati wa hafla ya uzinduzi wa tawi la chama hicho iliyofanyika eneo la Bondeni nje ya chuo hicho.
Katika hafla hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Katibu wa CHADEMA mkoani Tanga, Benson Mramba, mwenyekiti wa chama hicho wilayani Kinondoni, Henry Kilewo, na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Nasari Joshua, wakazi wa maeneo ya jirani waliomba nao kupatiwa kadi za chama hicho.
CHADEMA tayari imeshafungua matawi kwenye vyuo vikuu mbalimbali vikiwemo vile vya Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Chuo cha Mipango – Dodoma, Chuo cha Maadili –Dodoma, Chuo Kikuu cha Mt. Augustine (SAUT), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA) na wako mbioni kufungua matawi kwenye Chuo Kikuu cha Meru, Chuo cha Maendeleo – Tengeru na Chuo cha Uhasibu –Arusha ( IAA).
Lema aliwataka wanachuo hao kuhakikisha wanakuwa jasiri katika kudai haki zao pamoja na jamii inayowazunguka na wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote na badala yake wajenge tabia ya kuhoji pale wanapoona mambo hayaendi sawa.
Mbunge huyo wa Arusha Mjini aliwaeleza wanachuo hao kuwa watumie muda mwingi kuhamasishana kushiriki mijadala ya kisiasa na kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii kwenye maeneo mbalimbali nchini, jambo alilosema litasaidia kwa kiasi kikubwa kuwaamsha wananchi wengine.


NAUNGA MKONO KAZI NZURI YA KIJANA GODBLESS LEMA.
KAZA BUTI KITAELEWEKA TUU.

Ndiyo CDM!! kuna tetesi ambazo sio rasmi nimezisikia mahali nataka wana JF mwe makini kuzichunguza na kuzitafutia tiba iwapo na endapo kweli zitakuja kutimia. tetesi zenyewe ni juu ya matokeo ya mtihani wa kidato cha sita uliofanyika Februari 2011, inasemekana kuwa serikari ya CCM ina mpango wenye nia mbaya wa kupunguza ufaulu wa wanafunzi eitha kwa kuficha matokeo ama kuwafelisha wanafunzi kwa kiwango cha kutisha! Adhima na sababu iliyopo nyuma ya kusudi hili ni kwamba Vijana wengi wakijiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine moja kwa moja wanaenda kuongeza idadi ya wafuasi wa CDM ambapo upinzani wao dhidi ya CCM unakuwa ni upinzani uliopevuka kiakili na kifikra. Hivyo wana JF natoa tahadhari mapema ili endapo hii hali ikitokea tujue jinsi ya kuwatetea wadogo zetu na wenzetu wa CDM, sio taarifa rasmi lakini inaleta hisia ya kujiweka tayari kwa sababu CCM sa ivi imeamua kuingiza siasa katika maslahi yanayomhusu mwananchi moja kwa moja kama njia mojawapo ya kutaka kujitetea dhidi ya shubiri inayotolewa na CDM. Tusifikiri kwamba ccm wamenyamaza tu kuona vijana wengi vyuoni wakijiunga na CDM na bado matawi yakifunguliwa vyuoni kwa kasi hivi!! CDM tuwe makini!
 
Mwandishi alisahau kuwakumbusha kuwa Nasari Yoshua alishinda zikachakachuliwa! Hawa vijana wanafanya kazi nzuri sana! Waingie na mitaani na kwenye kila kata kufungua matawi ili kuimarisha chama. Baada ya 5yrs chama kiwe kimefika kila kijiji. Hiyo ndio kazi ya vijana siku zote. Kuimarisha chama! GOD BLESS CHADEMA
 
Wazazi nao wanawaangalia tu!!!hiyo shule inajikomba kwa chama tawala!
kuna shule moja ya msingi vitoto vinalazimishwa kuvaa fulana za njano na scurf za kijani. Ccm wanasahau kuwa hao ni watoto na wadogo zetu sisi tulioko vyuoni.
 
Waingie na mitaani na kwenye kila kata kufungua matawi ili kuimarisha chama..
Mbowe alisema hakuna kijiji ambacho hakitakuwa kimefikiwa na kiongozi wa juu yoyote wa Chadema kufika 2015 na jua CCM kuna sehemu hawajafika kwa zaidi ya miaka 20..
 
Ndiyo CDM!! kuna tetesi ambazo sio rasmi nimezisikia mahali nataka wana JF mwe makini kuzichunguza na kuzitafutia tiba iwapo na endapo kweli zitakuja kutimia. tetesi zenyewe ni juu ya matokeo ya mtihani wa kidato cha sita uliofanyika Februari 2011, inasemekana kuwa serikari ya CCM ina mpango wenye nia mbaya wa kupunguza ufaulu wa wanafunzi eitha kwa kuficha matokeo ama kuwafelisha wanafunzi kwa kiwango cha kutisha! Adhima na sababu iliyopo nyuma ya kusudi hili ni kwamba Vijana wengi wakijiunga na vyuo vikuu na vyuo vingine moja kwa moja wanaenda kuongeza idadi ya wafuasi wa CDM ambapo upinzani wao dhidi ya CCM unakuwa ni upinzani uliopevuka kiakili na kifikra. Hivyo wana JF natoa tahadhari mapema ili endapo hii hali ikitokea tujue jinsi ya kuwatetea wadogo zetu na wenzetu wa CDM, sio taarifa rasmi lakini inaleta hisia ya kujiweka tayari kwa sababu CCM sa ivi imeamua kuingiza siasa katika maslahi yanayomhusu mwananchi moja kwa moja kama njia mojawapo ya kutaka kujitetea dhidi ya shubiri inayotolewa na CDM. Tusifikiri kwamba ccm wamenyamaza tu kuona vijana wengi vyuoni wakijiunga na CDM na bado matawi yakifunguliwa vyuoni kwa kasi hivi!! CDM tuwe makini!


Duh another smell of sad story from CCM...yaani kama hii inshu ni kweli basi nawashauri CHADEMA msifunguie matawi kwenye mashule ya sekondari, bora hukohuko vyuoni coz ikitokea CCM wakajua kwamba kuna sekondari ina tawi la CDM nadhani madent watafanya kusikia tu abt University, sidhani kama kuna pua itagusa chuo.
 
Back
Top Bottom