Parabolic
JF-Expert Member
- Dec 3, 2013
- 2,870
- 3,146
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, John Heche amekutana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA Godbless Lema wakiwa na Makamu Mwenyekiti CHADEMA upande wa Zanzibar, Said Mzee; na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Dkt.Rugemeleza Nshala leo Septemba 17, 2026 jijini Dar es Salaam.
Kikao hicho kimefanyika wakati kukiwa na madai ya kutuhumiana na kurushiana maneno baina ya viongozi na wanachama wa chama hicho ambayo yamekuwa yakionekana katika majukwaa ya mitandao ya kijamii, madai ambayo yamewahusisha pia wanaharakati.
Kikao hicho kimetajwa kuwa sehemu ya jitihada za kuimarisha Umoja na mshikamano ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Soma pia: Lema, lengo lako kuhusu Heche ni nini hasa?