Wana ndoa na sherehe za usiku......

Wana ndoa na sherehe za usiku......

yamoyoni mwangu

Senior Member
Joined
Oct 25, 2013
Posts
106
Reaction score
31
Oy wana jukwaa, leo kuna kitu nimejifunza kitu kutoka hapa ninapo ishi....

mama mwenye nyumba, amekwenda harusini na kumuacha mumewe..... harusi yenyewe ni ya usiku.... sasa me nikawa najiuliza kwa umri wetu kweli hili suala linawezekana.... binafsi mm cwez kumuacha wife aende mwenyewe wala yeye hawezi kukubali mm niende mwenyewe.... cjajua kwenu wadau wewe na mkeo/mumeo/ mchumba ako mnaweza kufanya hivi... kama alivyofanya jamaa....
 
watu kwa umbea ....nitatukana ukiniambia kuwa wewe ni mwanaume...alafu unafuatilia mambo ya watu hivi
 
Sijui uwezo wako wa kufikiri uko ktk upeo gani.Yaani unaloona ni tishio kwa wanandoa ni kutokuwepo pamoja ktk shughuli ya harusi tuu,je mmojawapo anaposafiri kikazi na asirudi labda wiki au zaidi hapo imekaaje hakuna hatari ya usaliti hapo?Je ikiwa kuna harusi 2 zinafanyika siku moja maeneo tofauti na woote ni wa-karibu yenu hamuwezi kugawana mahudhurio?
 
dah, bila shaka hata chooni huwa unaenda na mkeo,.

Hii ni kazi sana!!
 
Mtindo wa kushambulia mtoa thread na kuacha kuchangia mada sio vizuri,kwani alichotoa jamaa hamna wanaume/wanawake wana mawazo au lifestyle kama hiyo?
 
Jamani nadhani mtoa hoja hamjamwelewa vizuri, amesema mume kabaki NYUMBANI na sio vinginevyo.
Mi nadhani si halali kitendo hicho, kusafiri no inshu nyingine kabisa. Kwa hiyo jengeni hoja Na sio kumshambulia mtoa hoja
 
Dah mazee, huwa huna shughuli nyingine zaidi ya kusubiri harusi tuu, au mtoko wako na wife ni harusi za watu tu duh
 
Mtindo wa kushambulia mtoa thread na kuacha kuchangia mada sio vizuri,kwani alichotoa jamaa hamna wanaume/wanawake wana mawazo au lifestyle kama hiyo?

umeshachangia mkuu?

back to the topic: kwangu sio tatizo hata kidogo. kuwa cheated huweza kutokea wakati usiotarajia kabisa.
 
si kila sherehe ni lazima kwenda chalii, nyingine hazikuhusu
 
Hata saloon je tuambatane nao???? wivu mwingine bwana hata aibu, kwanza wote tayari nyie ni used tu acha na wengine wakamalizie kama una mashaka
 
ni kweli haipendezi kwani ye ametoa maoni yake na angependa kujua ya wengine pia.
Mtindo wa kushambulia mtoa thread na kuacha kuchangia mada sio vizuri,kwani alichotoa jamaa hamna wanaume/wanawake wana mawazo au lifestyle kama hiyo?
 
......hii sio ishu kabisa kabisa ndg zangu...hapo ni MAELEWANO tu ndio hutawala. Ushauri wa bure: FUATA YAKO NA ISHI UPENDAVYO USIFUATILIE YA WATU as HAYAKUHUSU WALA KUKUSAIDIA LOLOTE! pia huwezi kufanya kila mtu aishi KWA STAILI YAKO AU UIPENDAYO WEWE!!
 
Oy wana jukwaa, leo kuna kitu nimejifunza kitu kutoka hapa ninapo ishi....

mama mwenye nyumba, amekwenda harusini na kumuacha mumewe..... harusi yenyewe ni ya usiku.... sasa me nikawa najiuliza kwa umri wetu kweli hili suala linawezekana.... binafsi mm cwez kumuacha wife aende mwenyewe wala yeye hawezi kukubali mm niende mwenyewe.... cjajua kwenu wadau wewe na mkeo/mumeo/ mchumba ako mnaweza kufanya hivi... kama alivyofanya jamaa....
SABABU:
  1. Labda mmoja kachoka sana........
  2. labda mmoja anaumwa.......
  3. harusi nyingi cku hizi za kiswahili sana,unaambiwa inaanza saa 12.30 jioni lakini unakuta inaanza saa 2.30 usiku...
  4. mwaliko zaidi ya mmoja,,,,,,,,,
  5. gharama...ci unajua kuna single au double,sasa ili kuwaridhisha maharusi walau unatoa mchango wa mmoja tu...
  6. siku hizi kuna viwango vya kuja harusini,pengine upande wa kiume wanataka idadi ya wageni 15 tu toka kwa bibi harusi,,sasa katika kujibanabana ndio hivyo wengine inabidi mpigwe panga...
  7. nakadhalika,,,,,,,,,,,,,,,,,,
 
Hujaweka wazi hofu yako uliyonayo au hofu ya mkeo wewe kwenda kwenye sherehe peke yako usiku. Kuna kitu nyuma ya pazia. Labda hamuaminiani nyie wote vicheche.
 
Back
Top Bottom