GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,571
- 108,922
Leo GENTAMYCINE nawapigia ' Salute ' JF Members wote kwani mnafanya Kazi kubwa sana ya ' Kuibua ' mambo mazito na makubwa ya Kuisaidia nchi ya Tanzania huenda kuliko mnavyojua.
Nakumbuka huko nyuma miaka Miwili imepita niliwahi kusema hapa hapa kuwa kama kuna Mshauri Mkuu namba Moja wa Rais au Kiuongozi yoyote nchini Tanzania basi ni (atakuwa) JamiiForums (kama Mtandao)
Na ukiona tu ama unasemwa au unazungumzia hapa JamiiForums basi amini kuwa kwa 85% una ' Mapungufu ' hivyo basi yakupasa ujitafakari kwa Kina ama uombe radhi kwa Umma au Ujiuzuru mwenyewe au ' Uuchune ' kisha aliyekuteua aje ' Kukutumbua ' pasipo tarajia.
Ni hapa hapa JamiiForums aliyekuwa DC Ole Sabaya 'madudu' yake yaliibuliwa na ni hapa hapa pia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na akapelekwa Mwanza ' madudu ' yake yaliibuliwa na Wote hawa yamewakuta ya Kuwakuta.
Hii ni baadhi tu ya Mifano ya Nguvu ya ' Presha ' ya JamiiForums kwa Watendaji wa Serikali kwani najua ipo Mifano mingi tu huko nyuma ya jinsi Watendaji wa Serikalini katika Tawala (Awamu) zilizopita nao ' walivyonyooshwa ' na Nguvu ya Mtandao huu Bora kabisa Tanzania, Duniani na huenda hata Mbinguni vile vile.
Sasa leo nawaombeni wana JamiiForums wote kwa ' Presha ' yetu hii hii ambayo ina Nguvu, Tija na Matunda yake tunayaona halafu na hata Mama nae (Mheshimiwa Rais) ni ' Mdau ' wetu mkubwa hapa naomba sasa tuhamishie ' Makombora ' yetu kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda (Daudi Albert Bashite)
Huyu Mtu (Makonda) kwa Taarifa nilizonazo za Kuaninika tena kutoka kwa Watu ' ninaowaamini 100% zinasema ni Mtu ' Hatari ' sana na amefanya Mambo mengi mabaya ambayo hata Mkuu mwenyewe wa Mashetani Duniani alimshangaa na anaendelea bado kumshangaa.
Rais wangu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan Mwanao Mimi GENTAMYCINE sitochoka Kukuomba 'uviamuru' Vyombo vyako' vimkamate' upesi huyu Makonda ambaye nasikia unamuonea mno ' aibu ' Kuamuru hivyo sijui ni kwanini wakati hata Wewe Mwenyewe unayajua mengi mabaya kumhusu Yeye na alishawahi hata ' Kukuchongea ' maneno kwa ' Babaake ' aliyetwaliwa na mkawa ' mnanuniana ' na Kushirikiana na Kuchekeana ' Kinafiki ' tu.
Sina Chuki binafsi na Paul Christian Makonda (japo ni mwana Simba SC Mwenzangu), ila nina Chuki zaidi na Matendo yake mabaya ( maovu ) na ya ' Kiukatili ' aliyoyafanya hasa hasa alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Tunawapongeza kwa mnayoyafanya kwa Watu kama akina Ole Sabaya na najua hata hii 'tengua' ya Chalamila nae muda wowote tu ' atakamatwa ' kwa ' Madudu ' yake aliyoyafanya huko Mkoani Mbeya ila Watanzania tunataka Paul Christian Makonda nae ' akamatwe ' vinginevyo mtatufanya wenye Akili Kubwa tuanze Kuamini kuwa huenda Makonda ni mkubwa kuliko Tanzania.
Sitochoka Kumsagia Kunguni Makonda.
Nakumbuka huko nyuma miaka Miwili imepita niliwahi kusema hapa hapa kuwa kama kuna Mshauri Mkuu namba Moja wa Rais au Kiuongozi yoyote nchini Tanzania basi ni (atakuwa) JamiiForums (kama Mtandao)
Na ukiona tu ama unasemwa au unazungumzia hapa JamiiForums basi amini kuwa kwa 85% una ' Mapungufu ' hivyo basi yakupasa ujitafakari kwa Kina ama uombe radhi kwa Umma au Ujiuzuru mwenyewe au ' Uuchune ' kisha aliyekuteua aje ' Kukutumbua ' pasipo tarajia.
Ni hapa hapa JamiiForums aliyekuwa DC Ole Sabaya 'madudu' yake yaliibuliwa na ni hapa hapa pia aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na akapelekwa Mwanza ' madudu ' yake yaliibuliwa na Wote hawa yamewakuta ya Kuwakuta.
Hii ni baadhi tu ya Mifano ya Nguvu ya ' Presha ' ya JamiiForums kwa Watendaji wa Serikali kwani najua ipo Mifano mingi tu huko nyuma ya jinsi Watendaji wa Serikalini katika Tawala (Awamu) zilizopita nao ' walivyonyooshwa ' na Nguvu ya Mtandao huu Bora kabisa Tanzania, Duniani na huenda hata Mbinguni vile vile.
Sasa leo nawaombeni wana JamiiForums wote kwa ' Presha ' yetu hii hii ambayo ina Nguvu, Tija na Matunda yake tunayaona halafu na hata Mama nae (Mheshimiwa Rais) ni ' Mdau ' wetu mkubwa hapa naomba sasa tuhamishie ' Makombora ' yetu kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Christian Makonda (Daudi Albert Bashite)
Huyu Mtu (Makonda) kwa Taarifa nilizonazo za Kuaninika tena kutoka kwa Watu ' ninaowaamini 100% zinasema ni Mtu ' Hatari ' sana na amefanya Mambo mengi mabaya ambayo hata Mkuu mwenyewe wa Mashetani Duniani alimshangaa na anaendelea bado kumshangaa.
Rais wangu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan Mwanao Mimi GENTAMYCINE sitochoka Kukuomba 'uviamuru' Vyombo vyako' vimkamate' upesi huyu Makonda ambaye nasikia unamuonea mno ' aibu ' Kuamuru hivyo sijui ni kwanini wakati hata Wewe Mwenyewe unayajua mengi mabaya kumhusu Yeye na alishawahi hata ' Kukuchongea ' maneno kwa ' Babaake ' aliyetwaliwa na mkawa ' mnanuniana ' na Kushirikiana na Kuchekeana ' Kinafiki ' tu.
Sina Chuki binafsi na Paul Christian Makonda (japo ni mwana Simba SC Mwenzangu), ila nina Chuki zaidi na Matendo yake mabaya ( maovu ) na ya ' Kiukatili ' aliyoyafanya hasa hasa alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Tunawapongeza kwa mnayoyafanya kwa Watu kama akina Ole Sabaya na najua hata hii 'tengua' ya Chalamila nae muda wowote tu ' atakamatwa ' kwa ' Madudu ' yake aliyoyafanya huko Mkoani Mbeya ila Watanzania tunataka Paul Christian Makonda nae ' akamatwe ' vinginevyo mtatufanya wenye Akili Kubwa tuanze Kuamini kuwa huenda Makonda ni mkubwa kuliko Tanzania.
Sitochoka Kumsagia Kunguni Makonda.