Wana CCM Iramba waja na Operation Chakaza Mkumbo(OCM)

Wana CCM Iramba waja na Operation Chakaza Mkumbo(OCM)

Hata kama.....Nyinyi kama chama tawala hampaswi kutumia nguvu kubwa kwenye majukwaa ya kisiasa baddala yake mnapaswa kutimiza ahadi mlizotoa na si vinginevyo.
Pamoja na kwamba mmeweka huo mkakati sijui operesheni lakini kama hamjatimiza ahadi mlizotoa ama wananchi hawajaona lolote la maendeleo tangu walipowapa madaraka, huo mkakati wenu hautafanikiwa na huyo mnayetaka kumchakaza ataendelea kung'ara na kupendwa.

MKAKATI WENU NI SAWA NA KUZIBA TUNDU LA PANYA KWA MKATE, mmechelewa!

Iramba political problem SOLVED.

Tunatumia majukwaa kufuta uongo unaotumiwa na viongozi wa upinzani kuwalaghai wananchi wasiojua kile kinachoendelea kisiasa. Tumefanya hivyo Iramba na Matokeo yake yako kwenye ofisi za tume ya uchaguzi kwa sasa.

Huwezi kutuchagulia njia na jinsi ya kufanya siasa wakati tuko tangu 1977 kwenye ulingo wa siasa. Tunafahamu kile tunachokifanya.
 
maisha haya yaani unanzisha post halafu unajijibu/mnajijibu .. MABADILIKO NI LAZIMA... kwa anayetaka na asiyetaka .. kujipa faraja si hatia endeleeni... ukweli CCM imechokwa namfahamu hilo endeleeni tu kuchafuana na harakati za ikulu ...
 
Iramba political problem SOLVED.

Tunatumia majukwaa kufuta uongo unaotumiwa na viongozi wa upinzani kuwalaghai wananchi wasiojua kile kinachoendelea kisiasa. Tumefanya hivyo Iramba na Matokeo yake yako kwenye ofisi za tume ya uchaguzi kwa sasa.

Huwezi kutuchagulia njia na jinsi ya kufanya siasa wakati tuko tangu 1977 kwenye ulingo wa siasa. Tunafahamu kile tunachokifanya.


Tambua kuwa wana-IRAMBA unaojaribu kuwasemea wana macho na uelewa wakutosha kujua zipi mbivu na mbichi......Hawahitaji watu kuwasemea ama kuwatazamia utekelezaji wa ahadi mlizotoa huko nyuma...
Hata kama kunawanao wanenea ya uongo wananchi wanauwezo wa kukataa propaganda zao.

Kikubwa ninachokiona kwako na chama chako ni kwamba uwezo wenu wakutatua matatizo ya wananchi umewaishia, na mpaka hivi sasa kuna mengi mliyoyaahidi kipindi lkilichopita hamjatekeleza na muda ndo unayoyoma kwa kasi.....Hivyo ili walau mfiche udhaifu wenu mmeamua kupambana na yeyote anayejitokeza kuwaelimisha wananchi namna ambavyo mmewatelekeza, na ambavy hamna tena uwezo wa kutekeleza....HII NI SAWA NA KUBEBA MAJI KWENYE PAKACHA!

Mnachopaswa kufanya sasa huko Iramba ni kuwaomba radhi wana -IRAMBA kwa kushindwa kutimiza ahadi zenu, na mkiri kuwa huo uwezo hamna......HILI NDO LITAKUWA LA BUSARA SANA , BADALA YA KUPAMBANA NA NIA TU YA DR MKUMBO
 
Na kama mnafikiri wanyiramba ni wepesi njooni wote mkae mwaka mzima muone,wanyiramba sio wepesi,mnajifanya mnakomboa watu,tuambieni tundu lisu amekomboa nini singida,msigwa amekomboa nini iringa,sugu amegkomboa nini mbeya,Lema amekomboa nini Arusha,Mnyika amekomboa nini Ubungo,wote wachumia tumbo

wameondoa fikra potofu kwa watanzania walio wengi hata wewe. Bila wao usingejua kuna EPA, Richmond na mengine. Huyo ndugu yako ana miaka mingapi bungeni na kawakomboa nini kama si kusubiria vijiweni awape hela vijana? Wananc

hi wengi majimbo ya CCM wamedumaa akili sabu bado wanajua rais wa nchi ni Nyerere. So iramba hatushangai.
 
Ni rahisi sana kuishinda Chadema waungwana kama kungekuwa na zahanati zenye madawa, visima vya maji vya kutosha , barabara nzuri , shule nzuri zenye kutoa elimu bora , mipango bora kwenye kilimo na ajira mbalimbali kwa vijana hapo Iramba mtagundua kwamba wanachama na wafuasi wa Chama cha Mapinduzi mngekuwa busy kwelikweli na wala hata msingepata muda wa kupambana na Dr Mkumbo kwakuwa angekosa cha kusema jukwaani na nyie mngekuwa mnapambana kwenye shughuli za maendeleo na wana Iramba.....hizo OPERATIONS na MOVEMENTS zote zinatia mashaka kwakweli
 
Chamdomo kimewauma sana na mmeumia sana. Nasikia katika uchaguzi huu mmetumia zaidi ya shs 120 million ati kupambana na Mwigulu
 
Iramba inaongoza kitaifa kwakuwa na huduma bora za Afya yani CHMCT. Pia no one kwa huduma bora zaCHF
 
Mikakati mikali ya kutokomeza element zote za Chadema aka Magwanda zimeanza kila kitongoji kwa wananchi wenye Mapenzi na Uzalendo na nchi hii kuhakikisha chadema na hasa Dr Kitila Mkumbo,kuhakikisha kuwa hawaruhusu jimbo hill linalokua kwa Kasi kimaendeleo halivurugwi na siasa za Fujo na chuki katika Iramba,

Wananchi kwa umoja wao wamedhamiria kuhalikisha Chadema haipati hata balozi ktk uongozi,tayari vitongoji wote wanapita nyumba kwa nyumba kulaani siasa za kuligawa taifa za chama hiki

We piga kelele tu hapa JF, lakini wenye akili hatudanganyiki na watu mnaochumia tumbo.

ei Jimbo linalokuwa kwa kasi kiuchumi?? Uchumi Gani watu hata maji ya kuoga inakuwa shida. Subiri dawa yenu M4C ije.mmekalia kuwahadaa watu eti Jimbo linakuwa kiuchumi tena wengi wenu hampo hata Iramba mko Dar mkingojea Bosi wenu mwigulu aje awagawie mabaki ya Bungeni kwa kazi ya keyboard mnayofanya hapa JF.
 
Iramba inaongoza kitaifa kwakuwa na huduma bora za Afya yani CHMCT. Pia no one kwa huduma bora zaCHF

Afya gani unayoongelea wakati watu wanashindwa hata kuswaki, hakuna maji. hio CHF ndio balaa juzi tu Kinampanda wazee walilalamika wanajiunga lakini wakienda hospitali dawa muhimu wanayoweza kupata ni panadol ya kuwatulizia maumivu na kuambiwa wakanunue dawa zingine. Hio Afya unayozungumza huku uko dar ni kudanganya akili yako mwenyewe wala hutamwokota mtu hapa. Wazee wapo wanataabika hakuna huduma, walilalamika mbele ya DC wewe unakuja na porojo hapa. Acheni kuwahadaa watu wa Iramba kwa mambo yasiokuwepo.
 
Inaelekea mieta uzi huu ni mbaguzi fulani hivi, na ubaguzi siyo sera ya ccm. Yeye anatoa wapi sera hiyo? Aache ubaguzi afanye siasa. Hiyo Iramba magharibi ni ngome ya ccm miaka yote iliyopita, je mbona bado ipo masikini hadi leo? Kwa hiyo cdm kupata asilmia 28 ndani ya ngome ya ccm ni jambo la kutia moyo wasilale wakaze buti kuendelea kutoa elimu zaidi, watu wataamka tu na wana cdm wataongezeka na kuleta mabadiliko.
 
Mikakati mikali ya kutokomeza element zote za Chadema aka Magwanda zimeanza kila kitongoji kwa wananchi wenye Mapenzi na Uzalendo na nchi hii kuhakikisha chadema na hasa Dr Kitila Mkumbo,kuhakikisha kuwa hawaruhusu jimbo hill linalokua kwa Kasi kimaendeleo halivurugwi na siasa za Fujo na chuki katika Iramba,

Wananchi kwa umoja wao wamedhamiria kuhalikisha Chadema haipati hata balozi ktk uongozi,tayari vitongoji wote wanapita nyumba kwa nyumba kulaani siasa za kuligawa taifa za chama hiki

Hii ni moja ya mambo ya kijinga kuwahi kutokea tanzania. Watu badala wakae wawajibu wapinzani wao kisiasa kwa kufanya shughuli za maendeleo na kisha wananchi wajionee wao wenyewe na pasiwe hata na haja ya wao kupiga kampeni wakati wa uchaguzi wanakaa kubwabwaja majukwaani na kwenye mitandao eti wana operation ya kumtokomeza Dr. Kitila. huu ni wehu, uchizi. kajipangeni upya.ccm na mawakala wake hamhitaji tena kuja kuwaambia wananchi chochote, ila waone wao wenyewe mkifanya maendeleo kama ilivyokuwa AHADI zenu.
 
Wanyiramba wengi bado tongotongo halijafutika,acha magamba waendelea kuwatumia mpaka wakome
 
Mtu yuko Dar es salaam anajifanya yuko Iramba...aacheni upuuzi leteni maendeleo kwa wananchi ukimchakaza Mkumbo halafu inakuwaje? Ye mbunge? Mnaacha kuwabana watendaji wenu walete maendeleo mnahangaika na watu wasiohusika...SWALI LA KUJIULIZA WEWE ni kwa nini sehemu ambazo viongozi wote ni wa CCM hakuna maendeleo tofauti na sehemu ambazo kuna hata madiwani wa UPINZANI? Ukiona sehemu wamechaguliwa viongozi wote kutoka chama kimoja iwe CCM au UPINZANI haitakiwi kushabikia maana hapo hamna wa kumfunga Paka kengele...Inasikitisha na kwa taarifa Iramba nimefika
 
Na kama mnafikiri wanyiramba ni wepesi njooni wote mkae mwaka mzima muone,wanyiramba sio wepesi,mnajifanya mnakomboa watu,tuambieni tundu lisu amekomboa nini singida,msigwa amekomboa nini iringa,sugu amegkomboa nini mbeya,Lema amekomboa nini Arusha,Mnyika amekomboa nini Ubungo,wote wachumia tumbo

Naona unapoandika vidole vinatetemeka
 
Iramba ni yawairamba na kwa hakika hata movement for chaga Iramba haiwezi kufua dafu. Mkumbo Hana chake namimi nipo kata ya Mtoa nikiratibu hii operation nikianzia nyumbani kwake Mkumbo hapa Mgela....hatulali wapenda Amani wapo kata zote 17. Mi ndio mratibu mkuu wa operation hii....viva CCM

kweli umewageuza wana iramba mazuzu ,huu uchaguzi mwigulu umeonyesha pakukazia wapi watu wanaenda kwa kujifunza kila mtu anajua Dodoma,Singida na Tabora mateja wa CCM lakini wameshaanza kuamka kwa hiyo vitisho vya kujimilikisha iramba kama kibwetele wa Uganda umekwisha ,ni somo kubwa sana kwamba book moja,mbili kwa wana iramba ni sawa na laki moja ,sasa acha kumchafua Dr Kitila kwa sababu Chadema ni taasisi sio mtu
 
Mtu yuko Dar es salaam anajifanya yuko Iramba...aacheni upuuzi leteni maendeleo kwa wananchi ukimchakaza Mkumbo halafu inakuwaje? Ye mbunge? Mnaacha kuwabana watendaji wenu walete maendeleo mnahangaika na watu wasiohusika...SWALI LA KUJIULIZA WEWE ni kwa nini sehemu ambazo viongozi wote ni wa CCM hakuna maendeleo tofauti na sehemu ambazo kuna hata madiwani wa UPINZANI? Ukiona sehemu wamechaguliwa viongozi wote kutoka chama kimoja iwe CCM au UPINZANI haitakiwi kushabikia maana hapo hamna wa kumfunga Paka kengele...Inasikitisha na kwa taarifa Iramba nimefika
maendeleo gani umeleta Iramba wewe hembu niambia,iguguno,tulya,shelui,kiomboi,kuna maendeleo gani pale ,tunakufahamu mwigulu umepatia pa kusema unawatenga wanyiramba,sio unaendekeza ukabila sio ndio siasa zenu tunakuangalia sana usidhani iramba ni baba yako subiri
 
Iramba inaongoza kitaifa kwakuwa na huduma bora za Afya yani CHMCT. Pia no one kwa huduma bora zaCHF
umewafuma hao wanyiramba wenzako ndio wadanganye hao hao bado kitambo kidogo wakiamua na kutoa matongotongo na kujua kwamba wewe ni kundi la wezi tu munaokula kwa mikono na m.a.ka,alio pale CCM na taifa watajijua kila mtu alijua wanyiramba ni watu wa mwisho kwa kujitambua kisiasa ,ni dezo ya CCM lakini ole wako watakapoamuka kikamilifu wameanza
 
maendeleo gani umeleta Iramba wewe hembu niambia,iguguno,tulya,shelui,kiomboi,kuna maendeleo gani pale ,tunakufahamu mwigulu umepatia pa kusema unawatenga wanyiramba,sio unaendekeza ukabila sio ndio siasa zenu tunakuangalia sana usidhani iramba ni baba yako subiri
Mkuu umenielewa nilichoandika kweli au umekurupuka? Tuliza akili rudia kusoma...halafu usinihusishe na watu nisiowafahamu
 
Wapiganapo mafahari wawili.....?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom