Mie ni Mmiliki.
Naungana na mleta hoja hapo juu,hii biashara lazima uwe na akili ya kuona mbali,sio hizi za kusema akupe elfu kumi then iwe yake.So,what next,inaamana wewe kila mwaka unatakiwa kubadilisha Driver mpya?hii sio akili ya kibiashara kabisaaa,na waoga wa biashara ndio wanaitumia.
Kama unakimbia changamoto za bodaboda basi sikufichi kwenye Gari ndio usisogee kabisaa,utakuafa,nakuambia kwa uzoefu
Mie hutumia hivi:-
-Hesabu yangu mie ni kwa Wiki Tsh:50,000
-Na kila baada ya miezi sita tu nauza Chombo nanunua kingine,na huwa nanunua kwanza kisha nampa Driver halafu ndio nakiuza ili asikose kazi hata siku moja.Unless kuwe na jambo katikati.
Na kwenye kuuza huwa baada ya kuuza nampa Driver kama zawadi ya pesa kwa kutunza Chombo vizuri in percentage,so hii hufanya na wao kuwa makini na chombo
-Driver akiwa na Msiba au ugonjwa wowote katika familia au Msiba wa Driver mwenzao,basi huleta pikipiki nyumbani au mdogo wangu anaenda kuichukua,na akipona anakuja kuichukua,hii huwa siangalii muda gani,hata kama ni mwezi.Ila ukizidi mwezi huwa nakuwa na option ya kumtafuta Day worker ili apige kwa muda then akipona ndio namrejeshea chombo chake,na huyo Day worker namuomba mwenyewe amtafute.
-Akiwa na dharura ya kifamilia au maafa,au ugonjwa,basi hutoa kiasi cha pesa ili kumsaidia kama sehem ya familia,tusiangalie pesa tu.
Halafu kama unapesa ya mawazo na Bodaboda moja,basi wasiwasi ndio anakuwa rafiki yako muda woote.Ila kwa mie mwenye more than one,huwa hainipi saana presha.Na thanks Allah kwamba Drivers wangu woote ni watu safi sana.Kuanzia wa Bodaboda hadi kwenye Carry.
Hakua kazi isiyo na stresses,lazima uwe na wazo endelevu kwamba leo unamiliki bodaboda moja basi kuna siku utamiliki zaidi ya moja,na baadae utamilimiku hadi gari.Sasa akili lazima uiandae kwa changamoto na sio kuzikimbia kwa kufanyakazi kwa hofu au kubahatisha kama hao wa Mkataba eti akimaliza inakuwa yake.Kinachofuata hapo unakuwa akili yako ipo limited.
Uwezo wa kujua changamoto za biashara hii inakupa uwezo mkubwa saana wa kuelewa,na ndio maana wale wenye kutaka wepesi wengi wao wameachia kazi hizi.Kuna siku nimeenda TRA kusajili nikamkuta kuna mdada anamiliki bodaboda 21,na hesabu ya wiki na hakuna mkataba wa kusema kwamba mali ni ya Driver ndani ya mwaka.vyombo vyote ni mali yake.Na anaenda vizuri na Drivers wake,leo hii wanaume ndio wanakimbia changamoto,aiseee.Kuna siku Dar itakuwa mji fulani wa wategea maisha.
Ndoto yangu ni kuunda Kampuni ya usafiri Dar,bila kujali gari aina gani.Nasuburi itimie idadi ya gari kadhaa then ni unde Kampuni ili nile vitenda vidogo vidogo,Idea ya website tayari inafanyiwa kazi Nairobi.
Na pia Drivers wangu wawili wa Carry wote walitoka kwenye Bodaboda wakaomba kama nikileta Carry niwashift,na ndio nilivyofanya na hadi leo wanaenda vizuri.Na mmoja yupo kwene option ya Noah ndio nasubiria kuipakia Dubai ili niilete.Although pia Carry zinapoteza soko inabidi nibadilike niingie kwenye Townace au liteace Tani moja ambazo zinasoko zuri sana kibiashara na demand kwa wateja ni kubwa,hii ni kutokana na Drivers wangu.
Biashara akili,ukikimbia changamoto basi kaa pembeni usubirie siku za mwisho wa ujana wako uanze kulaumu watu.
Mtoto wa Kitaa wazo lako na Plan yako aisee nimeipenda saaana,endelea nayo na usikatishwe tamaa,biashara ni mbuni na akili ya ubunifu.Na pia hesabu hizi zinategemea maeneo gani ya Biashara ndio maana hutofautiana kidogo.
Ushauri kwako pia,katika hizi siku unazowaachia za free,basi tenga muda kama nusu saa hivi ukagua chombo chako,ili kama kunatatizo dogo basi uweze kulifix kabla halijawa kubwa.