Kama uliangalia juzi ijumaa baada ya taarifa ya habari ya mbili, Star tv huwa kuna matangazo ya BBC, walimuhoji mtanzania mmoja alioko Marekani hususani eneo lilikotokea mauji hayo. Alisema hali ni mbaya kuliko inavyo ripotiwa aliongeza kuwa, huko marekani mengi sana yamekuwa yakitokea juu ya watu weusi na haya ripotiwi, mtu mweusi akitembea anaweza simamisha na askari hata mara tatu, ila mtu mweupe anapita tu au akasimamishwa mara moja tu au asisimamishwe kabisa. Tabia hii imewachosha wamarekani weusi kupelekea kuwapuuza polisi na ndipo mtiti unapoanzia hapo, akaulizwa kuhusu yeye, akasema kwa yeye na watanzania wenzake hamna tatizo kwa sababu Watanzania Wamezoe kuwaheshimu polisi, kwa wao wakisimamishwa huwa wanatii.