Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,881
- 33,319
Tupo na jamaa zangu mitaa ya Mawasiliano Dar, kuna jamaa toka Mbande sijui iko wapi, amekuja jijini akiwa na zawadi kwaajili ya rafiki yake wa kike waliyekutana naye mtandaoni, wamewasiliana na huyo mwanamama akafika mpaka lodge alipofikia akiwa na bodaboda, akaingia ndani aliko mja wake, baada ya kama dakika mbili akatoka na zile zawadi akapanda bodaboda aliyekuja naye na kuondoka faster.
Muda kidogo jamaa anatoka anauliza huyo mama yuko wapi, tunamwambia amepanda bodaboda ameondoka, anabaki anashangaa, anasema huyo rafiki yake wa kike amefika chumbani akamwambia anaomba nauli amlipe bodaboda pamoja na zawadi ili bodaboda ampelekee nyumbani kwake kuepuka usumbufu kwenye daladala baadaye, amepewa, alivyotoka amezima simu hapatikani ametoweka.
Kila siku mbinu mpya za kuwaliza wanaume wajao toka bara. Wanaume wenzangu tuweni makini na viumbe hawa ipo siku watawaua, wanawake wa jiji walishatokwa na utu, hali siyo hali.
Muda kidogo jamaa anatoka anauliza huyo mama yuko wapi, tunamwambia amepanda bodaboda ameondoka, anabaki anashangaa, anasema huyo rafiki yake wa kike amefika chumbani akamwambia anaomba nauli amlipe bodaboda pamoja na zawadi ili bodaboda ampelekee nyumbani kwake kuepuka usumbufu kwenye daladala baadaye, amepewa, alivyotoka amezima simu hapatikani ametoweka.
Kila siku mbinu mpya za kuwaliza wanaume wajao toka bara. Wanaume wenzangu tuweni makini na viumbe hawa ipo siku watawaua, wanawake wa jiji walishatokwa na utu, hali siyo hali.