Ushauri mzuri tu
Hata hivyo, ushauri wako umeangalia upande mmoja tu wa sifa, kwamba wana qualifications za kuwafanya wakasomee diploma ya ualimu au fani zingine zozote
Upande wa pili ambao haukuuangalia ni;
1. Gharama za kwenda kusomea diploma ambazo zina range kati ya 1,000,000 hadi 3,000,000 kwa mwaka. Tukumbuke kuwa hii special diploma in education for science teachers kwa UDOM ilikuwa inafadhiliwa na serikali kwa kuwapa mikopo hawa vijana 100% na ndiyo maana kuna vijana wengine walishachaguliwa kwenda High Schools lakini kwa kuvutiwa na programu hii ambayo ilikuwa wakimaliza wana ajiriwa moja kwa moja waliacha na kuamua kujiunga nayo. Hawa walikuwa ndo wazalendo wa kweli!!
2. Uchache/uhaba wa nafasi katika vyuo vya serikali vinavyotoa Stashahada ya ualimu especially ktk masomo ya sayansi ambako huko ingalau hata watoto wa maskini walala hoi wanaweza kumudu gharama za kusomesha watoto wao.
Option pekee ya nafasi inabakia kwenye vyuo vya binafsi ambako ndiko kuliko na gharama unbearable kwa watoto wa maskini ya kati ya milioni moja hadi milioni tatu au hata zaidi!!
.....Ndo kusema kuwa hoja sio sifa na muda kuruhusu kufanya application bali vikwazo vikubwa ni hivyo hapo juu!!