Waliosoma Tosamaganga High School

Waliosoma Tosamaganga High School

Tupia Jichoooo
Naikumbuka sana hiyo shule.Nilikomaa hapo miaka minne.CHUA walikuwa wakifika wanatushangaa sana jinsi Ma Olevel tulivyo adopt mazingira na kuyafurahia maisha ya Tosa.
Nyie ndo mlikuwa mnatuita CHUA sio?
 
Sisi tuliosoma enzi miaka ya 2001 kulikuwa na kitu kinaitwa E.M.O kuna mzee mmoja nadhani alikuwa mhasibu wa shule anaenda mjini postal bank anakuja na majina ya waliopata EMO yanabandikwa pale staff kwa nje aisee ukiona jina unafurahi sana. EMO kwa saaa ndio hizi MPESA, Tigo Pesa etc. kweli mambo yanaenda kasi.
Advance mwaka huo, hope tulikuwa pamoja
 
Kwa wale wa kitambo miaka ya 2000s na 90s hiyo picha ya juu hapo kati ni Mkwanga enzi hizo akiwa Mkuu wa Shule. Hapo anapiga stori za za ajabu na mikwara kibao. Utasikia wanaumee sasa pumzisheni vichwa vya chini mtumie vichwa vyenu vya juu...Hahaaa kitambo sana na memory inarudi kwa kasi nakumbuka mabanzi(bans) au maandazi ya ngano ile isiyochakatwa ya kwa masista wa Liharamo.
Mpiga picha design hiyo alikuwa ni SOLDIER
 
Back
Top Bottom