Waliojipatia Milioni 280 kwa njia ya Mtandao watozwa Faini ya Laki Tano

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewahukumu Amiry Luwiso na Ashirafu Awadh waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo ya kuongoza genge la uhalifu kwa njia ya mtandao na kujipatia zaidi ya Sh milioni 280 kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya Sh 500,000 kila mmoja baada ya kukiri mashtaka yanayowakabili.

Hukumu hiyo iitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo baada ya washtakiwa hao kutimiza masharti ya makubaliano ya kukiri kosa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Akiwasomea hukumu hiyo, Hakimu Mazengo alisema mahakama imetoa hukumu hiyo kwa kuzingatia kitendo cha washtakiwa hao kukiri mashtaka yao bila kuisumbua mahakamani na kwa kuzingatia makubaliano kati yao na DPP.

Chanzo: Habari Leo
 
Mtu akikamatwa anachoma mkaa au kuuza anakula mvua za kutosha na faini km onyo kwa wengine ila mwizi wa mabilion ya fedha na ufisadi faini yake huwa ni ndogo sana.
Hukumu iliyotolewa ndiyo uhalisia wa nchi yetu ilivyo hata kwa viongozi.
Gharama ya kutengeneza treni used au meli inazidi bei ya treni au meli mpya na hakuna atakayemshitaki.
CCM oyeeee!
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewahukumu Amiry Luwiso na Ashirafu Awadh waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo ya kuongoza genge la uhalifu kwa njia ya mtandao na kujipatia zaidi ya Sh milioni 280 kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya Sh 500,000 kila mmoja baada ya kukiri mashtaka yanayowakabili.

Hukumu hiyo iLItolewa juzi na Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo baada ya washtakiwa hao kutimiza masharti ya makubaliano ya kukiri kosa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Akiwasomea hukumu hiyo, Hakimu Mazengo alisema mahakama imetoa hukumu hiyo kwa kuzingatia kitendo cha washtakiwa hao kukiri mashtaka yao bila kuisumbua mahakamani na kwa kuzingatia makubaliano kati yao na DPP.

Chanzo: Habari Leo
Hukumu hizi, unashindwa hata kushangaa.
 
Nadhani hapo adhabu sio hiyo laki 5 wala miezi 6, adhabu kamili iko kwenye makubaliano na DPP.

Kinachoonekana ni kwamba walishakubaliana na DPP kama ni kulipa ama kurudisha pesa.

Hapo ilitakiwa yasomwe makubaliano ya hao jamaa na DPP ndio tuelewe adhabu kamili ni ipi.

Maana ukishakubaliana na DPP kinachofuata ni kupunguziwa adhabu tu.
 
Nadhani hapo adhabu sio hiyo laki 5 wala miezi 6, adhabu kamili iko kwenye makubaliano na DPP.

Kinachoonekana ni kwamba walishakubaliana na DPP kama ni kulipa ama kurudisha pesa.

Hapo ilitakiwa yasomwe makubaliano ya hao jamaa na DPP ndio tuelewe adhabu kamili ni ipi.

Maana ukishakubaliana na DPP kinachofuata ni kupunguziwa adhabu tu.
Anachosema hakimu pale mbele ya mahakama ndicho kinachofanyika, hakuna kitakachofanyika pembeni kama maamuzi afu asikisema mbele ya mahakama. Hata hivyo sio mara ya kwanza Tz kuwa na upumbavu na namna hiyo
 
Aise
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewahukumu Amiry Luwiso na Ashirafu Awadh waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka mawili ikiwemo ya kuongoza genge la uhalifu kwa njia ya mtandao na kujipatia zaidi ya Sh milioni 280 kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya Sh 500,000 kila mmoja baada ya kukiri mashtaka yanayowakabili.

Hukumu hiyo iitolewa juzi na Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo baada ya washtakiwa hao kutimiza masharti ya makubaliano ya kukiri kosa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Akiwasomea hukumu hiyo, Hakimu Mazengo alisema mahakama imetoa hukumu hiyo kwa kuzingatia kitendo cha washtakiwa hao kukiri mashtaka yao bila kuisumbua mahakamani na kwa kuzingatia makubaliano kati yao na DPP.

Chanzo: Habari Leo
Eeeh
 
IMG_0178.jpg

FYI
 
Nadhani hapo adhabu sio hiyo laki 5 wala miezi 6, adhabu kamili iko kwenye makubaliano na DPP.

Kinachoonekana ni kwamba walishakubaliana na DPP kama ni kulipa ama kurudisha pesa.

Hapo ilitakiwa yasomwe makubaliano ya hao jamaa na DPP ndio tuelewe adhabu kamili ni ipi.

Maana ukishakubaliana na DPP kinachofuata ni kupunguziwa adhabu tu.
Kumbe sasa kuna umuhimu wa kuwekwa wazi makubaliano.
 
Ashirafu Awadh na Amiry Luwiso waliokua wakikabiliwa na mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu kwa njia ya mtandao na kujipatia zaidi ya Tsh. Milioni 280 wamehukumiwa kwenda jela miezi 6 au kulipa faini ya Tsh. 500,000 kila mmoja baada ya kukiri mashtaka

Hukumu imetolewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Pamela Mazengo baada ya washtakiwa kutimiza masharti ya makubaliano ya kukiri kosa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)

Soma Waliojipatia Milioni 280 kwa njia ya Mtandao watozwa Faini ya Laki Tano

#JFMatukio #Justice #JamiiForums
FB_IMG_1697385601335.jpg
 
Back
Top Bottom