Walioitwa Majipu kulipwa Tsh. Bilioni 2.2

Walioitwa Majipu kulipwa Tsh. Bilioni 2.2

Hayo yamesemwa na Mh Halima Mdee ambaye ni msemaji wa kambi ya upinzani wa wizara ya fedha na mipango , wakati akisoma maoni ya kambi hiyo kuhusu mapendekezo ya mpango wa Taifa wa Maendeleo kwa mwaka 2017/18.

" Tumeshuhudia serikali ya ccm ikijitapa kutumbua majipu iliyotengeneza yenyewe kwa mbwembwe , kumbe nyuma ya pazia serikali hiyo hiyo inayalipa majipu hayo mishahara pamoja na marupurupu mengine "

" septemba bil 2.2 zilitengwa kwa ajili ya kuwalipa viongozi waliotumbuliwa , ikiwemo tsh mil 198.8 kama POSHO YA USUMBUFU . "

Chanzo - Mwananchi .
Ndiyo hivyo tuliyataka wenyewe....kuna wajinga waliitikia "TUMBUA"...Kumbe pesa zinanyakuliwa
 
Je haya majipu mapya ya TRA nayo yataendelea kulipwa ?
 
Haya haya , mwingizeni na huyu wa leo kwenye hayo malipo .
 
Kwa hiyo akiongea Halima basi hakuna kuhoji? Maana naona vijimaneno tu. Mwambie awataje hao wanaolipwa izo bilioni 2.2. La sivyo ni siasa za maji taka na wewe unayeshabikia bila kuhoji majina ni akina nani unajizalilisha.
 
Kwa hiyo akiongea Halima basi hakuna kuhoji? Maana naona vijimaneno tu. Mwambie awataje hao wanaolipwa izo bilioni 2.2. La sivyo ni siasa za maji taka na wewe unayeshabikia bila kuhoji majina ni akina nani unajizalilisha.
Halafu pia wanalipwa na posho ya usumbufu .
 
Endeleeni kumwingiza na huyo mkidhani eti mtakwamisha juhudi za Rais wetu kulikwamua taifa hili kutoka kwenye utumishi wa ovyo.
 
Toka silaa ameondoka hawana hoja kabisa na Magu anawafanya waonekane hawapo duniani. Ndio maana wanatoka kula majani wanalipuka tu ili walau wasikike, hii tv live imearibu biashara ya wauza sura.
 
Hata jambo la Mramba lazima kama hilo. Maana nasikia Mramba amekuwa analipwa mshahara Mkubwa zaidi milioni 25 kwa mwezi(sina uhakika)
 
Hayo yamesemwa na Mh Halima Mdee ambaye ni msemaji wa kambi ya upinzani wa wizara ya fedha na mipango , wakati akisoma maoni ya kambi hiyo kuhusu mapendekezo ya mpango wa Taifa wa Maendeleo kwa mwaka 2017/18.

" Tumeshuhudia serikali ya CCM ikijitapa kutumbua majipu iliyotengeneza yenyewe kwa mbwembwe , kumbe nyuma ya pazia serikali hiyo hiyo inayalipa majipu hayo mishahara pamoja na marupurupu mengine "

" Septemba bil 2.2 zilitengwa kwa ajili ya kuwalipa viongozi waliotumbuliwa , ikiwemo tsh mil 198.8 kama POSHO YA USUMBUFU . "

Chanzo: Mwananchi .
Hah hah hayo yamesemwa na Halima Mdee,kazi ipo na kwa kuwa yamesemwa na Mdee jamaa wanashangilia utadhani wao ndio wanufaika,nadhani mngejisikia aibu kwanza .
 
Back
Top Bottom