Walioishi kabla ya Yesu na Muhammad wamepotea ?

Walioishi kabla ya Yesu na Muhammad wamepotea ?

Mwenyezi mungu ni muadilifu. Kwenye Quran ameahidi hatomuadhibu mtu ambaye kaishi hadi kufa hajawahi kusikia habari za mitume .Qur-an 17:15 9"Wala Sisi hatukuwa wenye kuadhibu mpaka tuwapelekee Mtume." Hapo kundi la msamaha wanaingia vichaa, watoto na watu waloishi bila kusikia habari za Muumba.
Sasa huoni ilikuwa busara zaidi kutoleta mitume kabisa ili wasiwepo watu wa kukaata na binadamu wote waingie mbinguni?
 
Acha zako kule ndipo ustaarabu umeanzia , wazungu hawana historia ni watoto wa juzi ..Ukiinza hata uingereza ni ya juzi hapa tena baada ya kuanzishwa kwa Aglican , kule USA walikuwa jamii kama red indian .

Katika uislamu , unatumbua kipind cha ujahili(watu kabla ya kustaarabik) , uislamu unaenda mbali kwa kuonyesha watu walifikiwa na ujumbe kwa wale ambao hakuwafikiwa basi hawana kosa . Dini ni ustaarbu ndiyo maana kulikuwa na muendelezo wa manabii kuja kuwajuza watu ...America , Europe za juzi tu kihistoria kama mwafrika, wengi wamepata nguvu kipind cha utumwa na mapinduzi ya viwanda .​
Kama nia ni wengi waende mbinguni , kutoeneza ujumbe haliwezi kua jambo jema kweli, maana no ujumbe no makosa?
 
Mwenyezi mungu ni muadilifu. Kwenye Quran ameahidi hatomuadhibu mtu ambaye kaishi hadi kufa hajawahi kusikia habari za mitume .Qur-an 17:15 9"Wala Sisi hatukuwa wenye kuadhibu mpaka tuwapelekee Mtume." Hapo kundi la msamaha wanaingia vichaa, watoto na watu waloishi bila kusikia habari za Muumba.
"tuwapelekee Mtume." Ina maanisha nini
 
Dini ipi imeeneza utumwa ? Hakuna dini ambayo imeenzea utumwa bali jamii ilikuwa katika enzi za utumwa , mitume ilikuwa dhalili . Nitajie mtume mmoja aliyekuwa ana miliki watumwa ?

Hakuna vita ya dini hata siku , vita ipo katika watu kujilinda , dini hailindwi kwa mujibu wa kiislamu ila watu kama wanasimamia haki wanaweza kupigana dhidi ya dhulma mpaka hao madhulmat waijue haki ..Dini hailindwi hata siku moja wlaa haipiganiwi .

Ubaguzi ni stori za miaka na miaka , ubaguzi ni kinyume cha dini .
Yule jamaa aliekuwa na wake 1000 na utajiri wa kutisha alikuwa na watumwa kibao
 
Hapana mkuu!

Kwa upande wa ukristo!
YESU alikuwa anawakilishwa na dhabihu za wanyama, ambapo mtu akitenda dhambi alitakiwa kutoa kafara ya mnyama!

kwa sababu mshahara wa dhambi ni mauti, kwa hiyo mnyama ndiye alichukua hatia ya dhambi na kufa!!

Baada ya YESU kuja ndiye alilipa deni la dhambi, kwa hiyo kila mwanadamu anaye mwamini, atasamehewe kupitia kumwamini YESU!
Kama ulikwepo vile kumbe ni story tu
 
Ujumbe utakufikia kwa sababu kuna wajumbe .
Kama nia ni wengi waende mbinguni ujumbe wa Muhammad na Yesu hautakiwi kuenezwa maana watu wasiposikia hakuna shida na mungu ila wakiusikia ujumbe lazima waamini vinginevyo wakiutaa wanapotea, kwa hiyo ni bora zaidi wasiusikie ujumbe maana ndio wanakuwa upande salama zaidi wa kutohukumiwa.
 
Yule jamaa aliekuwa na wake 1000 na utajiri wa kutisha alikuwa na watumwa kibao
Sema watumwa kwa mujibu ya kitabu gani , onesha kwamba alimili watumwa , mimi ni mtumishi wa umma inwezekana nikawa mtumwa kwa aliyeniajiri ila nataka kuona watumwa wa kufungwa nyoror .
 
  • Kicheko
Reactions: Lax
Kama nia ni wengi waende mbinguni ujumbe wa Muhammad na Yesu hautakiwi kuenezwa maana watu wasiposikia hakuna shida na mungu ila wakiusikia ujumbe lazima waamini vinginevyo wakiutaa wanapotea, kwa hiyo ni bora zaidi wasiusikie ujumbe maana ndio wanakuwa upande salama zaidi wa kutohukumiwa.
Ni maoni yako ila ona leo kila kona umefika , aliypanga ni muweza ...Unachotakiwa kujua haki inafundishwa hapo , hiki kibaya na hiki kizuri .

Lazima upotee unapoktaa , kwani kwa jambo dogo mbona hataa nchi ina sheria za mambo ya kufuata na ukienda kinyume umefnya kosa ..Basi njia ya haki lazima itangazwe.
 
Hivi vitabu viliandikwa zamani sana. Viliendana na uwezo wa kufikiri wa watu wa enzi hizo. Leo yaliyoandikwa mule mengi haya make sense hata kwa logic ndogo sana. We unaambiwa mungu ni muweza wa yote lakini ili awasamehe viumbe wake ni mpaka wamuombe tena kupitia mitume wake sasa kwanini asituumbe katika hali ambayo kiasili tu huwezi kumkosea.
 
Kama hawajapotea na wataenda mbinguni kulikuwa na haja gani ya Yesu Kristo kuja kufa kwa ajili ya dhambi za binadamu na Muhammad kuja na Quran yake ?

Maisha si yangeweza kuendelea tu kama kawaida bila wao?!
Yesu alivokufa alishuka kuzimu kutangaza habari njema. Muhammad ni mtume wa uongo alijitungia tu mambo, ameoza anasubiri kufufuliwa na Yesu.
 
Sema watumwa kwa mujibu ya kitabu gani , onesha kwamba alimili watumwa , mimi ni mtumishi wa umma inwezekana nikawa mtumwa kwa aliyeniajiri ila nataka kuona watumwa wa kufungwa nyoror .
Kufungwa minyororo ndio kigezo Cha utumwa? Hata hapa Africa walikuwa wakifungwa chains wakat wa kuwasafirisha tu wakifika eneo husika wanakuwa free mana hawana pa kukimbilia. Lete hoja nyingine
 
Yesu alivokufa alishuka kuzimu kutangaza habari njema. Muhammad ni mtume wa uongo alijitungia tu mambo, ameoza anasubiri kufufuliwa na Yesu.
Kwa nini hakusubiria binadamu wote wafe waende kuzimu kisha ndipo aje mwisho wa dunia kabisa asulubiwe ashuke kuzimu kuwapa msamaha ?
 
  • Thanks
Reactions: Lax
Yesu alivokufa alishuka kuzimu kutangaza habari njema. Muhammad ni mtume wa uongo alijitungia tu mambo, ameoza anasubiri kufufuliwa na Yesu.
Anachukua jukumu gani ikiwa kuna billions of suvh followers kwa sasa
 
Kufungwa minyororo ndio kigezo Cha utumwa? Hata hapa Africa walikuwa wakifungwa chains wakat wa kuwasafirisha tu wakifika eneo husika wanakuwa free mana hawana pa kukimbilia. Lete hoja nyingine
Nioneshe huyu nabii alikuwa na mtumwa , kama ni wafanyakazi hata mimi nimeajiriwa na serikali basi ni mtumwa.🙂🙂
 
Kwa mtazamo wa Ukristo.

Watu walioishi kabla ya Yesu hawakuwa wamepotea wote moja kwa moja. Biblia inaonyesha kwamba Mungu aliwahukumu kwa kile walichojua na kwa imani yao kwa Mungu.

Lakini kwa Ukristo, kifo cha Yesu kilikuwa na umuhimu kwa sababu Yesu alikuja kufanya kile ambacho dhabihu za zamani hazikukamilisha yaani upatanisho wa dhambi kwa njia ya mwisho na kamili.

Kwa mtazamo wa Uislamu.

Muhammad hakuchukuliwa kuwa ndiye aliyeanzisha njia mpya ya wokovu. Uislamu unaamini manabii wengi walikuja kabla yake Adam, Nuhu, Ibrahim, Musa, Isa n.k. wakiwa na ujumbe wa msingi wa kumwabudu Mungu mmoja.
Muhammad anachukuliwa kuwa mjumbe wa mwisho, na Qur'an kuwa ufunuo wa mwisho uliothibitisha/kukamilisha ujumbe huo.

Majibu ya kidini huwa kwamba hawakuja kwa sababu Mungu alishindwa kuwaokoa watu bila wao, bali kwa sababu Mungu alichagua njia hiyo ya kujifunua na kuwaongoza wanadamu.
 
Kabla ya wao kulikua na manabii kwa upande wa uislam Muhammad ndo wa mwisho hakutakuja Mtume mwengine ila kwa upande mwengine wapo hao akina mwamposa na manabii wengine.
TUnaye mtume mwamposa na wengine kibao,wapi walisema mudi ndio awe wamwisho acha kukaza fuvu pokea wokovu na unapatikana bure.
 
Back
Top Bottom