Waliochagua kubaki kupiga box majuu waliona mbali

Mkuu, unachosema ni sahihi na naona hoja yako ni ya msingi kabisa. Hata hivyo, inabidi ujiulize huo mkataba utakaoufunga na serikali utafungwa kwa kutumia sheria ipi? Hakuna mkataba bila sheria. Ndio maana nikasema ipitie sheria ya manunuzi ya mwaka 2004.

Pamoja na uwepo wa sheria ya manunuzi, sheria hiyo imezingatia tenda zinazotangwazwa na serikali, lakini upo mwanya pia wa raia ye yote kuomba idhini ya serikali kushughulikia kile ambacho serikali haijatangaza. Kwa utaratibu huo, ombi la mhusika hufikishwa kwenye vikao husika. Vikao vikikubaliana na ombi hilo, serikali itatoa tangazo kwenye gazeti la serikali kwa muda muafaka kuona kama kuna pingamizi la kisheria. Kusipotokea pingamizi la kisheria lenye kuweka zuio la ajenda hiyo, basi serikali itakuwa imejiridhisha kumpa mkataba mhusika.

Ulichosema wewe ni sawa, lakini umebana zaidi kwenye sheria ya manunuzi inayotangazwa na serikali, ila katika sheria hiyo haijaweka kipengela cha hoja aliyosema Njele.

Kuna baraza la madiwani ambalo mara nyingi ndilo linaloweza kutoa baraka wakiona jambo hilo ni la manufaa kwa umma. Binafsi ningeshauri Mdau Njele kuongea na ofisi ya Madiwani wa eneo husika, hao mara nyingi wapo karibu ya wananchi na wanajali masilahi ya wananchi na wanaweza kumsaidia kufikia malengo yenye manufaa kwa wananchi.
 
Pamoja na uwepo wa sheria ya manunuzi, sheria hiyo imezingatia tenda zinazotangwazwa na serikali, lakini upo mwanya pia wa raia ye yote kuomba idhini ya serikali kushughulikia kile ambacho serikali haijatangaza. Kwa utaratibu huo, ombi la mhusika hufikishwa kwenye vikao husika. Vikao vikikubaliana na ombi hilo, serikali itatoa tangazo kwenye gazeti la serikali kwa muda muafaka kuona kama kuna pingamizi la kisheria. Kusipotokea pingamizi la kisheria lenye kuweka zuio la ajenda hiyo, basi serikali itakuwa imejiridhisha kumpa mkataba mhusika.

Ulichosema wewe ni sawa, lakini umebana zaidi kwenye sheria ya manunuzi inayotangazwa na serikali, ila katika sheria hiyo haijaweka kipengela cha hoja aliyosema Njele.

Kuna baraza la madiwani ambalo mara nyingi ndilo linaloweza kutoa baraka wakiona jambo hilo ni la manufaa kwa umma. Binafsi ningeshauri Mdau Njele kuongea na ofisi ya Madiwani wa eneo husika, hao mara nyingi wapo karibu ya wananchi na wanajali masilahi ya wananchi na wanaweza kumsaidia kufikia malengo yenye manufaa kwa wananchi.
Unachosema ni sahihi kwa asilimia 100. Nakumbuka kuna bwana mmoja aliwahi kuiconvince halmashauri ya mji wa Kibaha kuipa huduma ya kukusanya kodi za majengo. Utaratibu unaousema hapa ukafuatwa na yule bwana akapewa kazi. Alikuwa na idea innovative ya kuwa proactive katika kukusanya kodi za majengo kuliko ilivyo sasa kwamba mlipa kodi anasubiriwa mpaka aje kulipa mwenyewe. Hata hivyo, yule bwana alikutana na vikwazo vingi toka kwa wenye majengo akakimbia.
Ushauri wa kudeal na wabunge ni mzuri. Labda mdau Njele atuambie ni sehemu gani ya nchia anayotaka kufanya shughuli yake. Anaweza kupata mtu akamuunganisha na wafanya maamuzi. Hii ni dunia ya connections and networking...
 
Last edited by a moderator:
Unachosema ni sahihi kwa asilimia 100. Nakumbuka kuna bwana mmoja aliwahi kuiconvince halmashauri ya mji wa Kibaha kuipa huduma ya kukusanya kodi za majengo. Utaratibu unaousema hapa ukafuatwa na yule bwana akapewa kazi. Alikuwa na idea innovative ya kuwa proactive katika kukusanya kodi za majengo kuliko ilivyo sasa kwamba mlipa kodi anasubiriwa mpaka aje kulipa mwenyewe. Hata hivyo, yule bwana alikutana na vikwazo vingi toka kwa wenye majengo akakimbia.
Ushauri wa kudeal na wabunge ni mzuri. Labda mdau Njele atuambie ni sehemu gani ya nchia anayotaka kufanya shughuli yake. Anaweza kupata mtu akamuunganisha na wafanya maamuzi. Hii ni dunia ya connections and networking...

Nashukuru sana kwa mawazo yenu ZeMarcopolo, Candid Scope, nnna wadau wengine hapa JF, kwani nazidi kuhakikishiwa hapa ndipo Jukwaa huru la great thinkers kama ilivyokuwa kilima cha Aleopago kule Ugiriki kwa mababu wa falsafa.

Naanza kufunguka, maana mambo ya nchi yetu hayako katika mkondo ulionyoka, unashtukia njia za kawaida ambazo zipo na zinaeleweka mtu unajikuta ukijibamiza ukutani tu kama huna akili timamu vile, kumbe wenyewe wanazijua njia za kuuzunguka ukuta huo.

Nimejitahidi kuwa na subira, na hata michango ambayo ilionekana kuwa kinyume cha matarajio kwangu imekuwa ni challenge ya kunisaidia kuongeza kasi ya kupanda mlima ninaokusudia ufika kileleni kusimamisha alama ya ukombozi wetu wa uhuru wa kujitegemea.
 
Wazo la kuanzisha sehemu za kupumzikia na kuchezea ni zuri sana ila mdau usisahau kuwa TZ ni dunia ya tatu, huo utamduni hatuna, sie tunafikiria mahitaki mengine tofauti kabisa kama afya, elimu, nishati na makazi.

TZ inatia huruma, mbaya zaidi ukitoka nje ya bongo halafu ukarudi unaweza hata kulia jinsi watz wanavyoishi maisha duni, hasa wale wa vijijini unaweza sema wanaigiza dah.
 
Wazo la kuanzisha sehemu za kupumzikia na kuchezea ni zuri sana ila mdau usisahau kuwa TZ ni dunia ya tatu, huo utamduni hatuna, sie tunafikiria mahitaki mengine tofauti kabisa kama afya, elimu, nishati na makazi.

TZ inatia huruma, mbaya zaidi ukitoka nje ya bongo halafu ukarudi unaweza hata kulia jinsi watz wanavyoishi maisha duni, hasa wale wa vijijini unaweza sema wanaigiza dah.

Nimekupata vizuri tu Leornado, lakini fikiria majuzi tu kule bungeni waziri Mwakiembe alitahadharisha magari ya abiria kutosimama barabarani kuruhusu abiria kwenda kuchimba dawa porini.

Hoja ya Mwakiembe haina mantiki kwa vile huwezi kuzuia jambo hilo wakati serikali haijajenga vituo vya kupumzika kando ya barabara kuu kila baada ya mwendo wa urefu unaokubalika ambapo vituo hivyo vingekuwa na sehemu za kujisaidia. Hata hilo kama atajitokeza mmoja kutaka kuwekeza utaniambia bado kwa sasa Tanzania hatuhitaji?
 
hahahahaha kupunzika bongo. hiyo foleni yenyewe ya kwenye daladala ukiwa unatoka kazini ni mapunziko tosha . unafika nyumbani usiku umechoka unafikia kujitupa kitandani uamke mapema kesho saa kumi usiku. (WATANZANIA HAWAHITAJI GARDEN ZAKUPUNZIKIA WALA VIWANJA VYA MICHEZO) utapunzika vipi wakati unaishi kwa dhiki na mawazo

Kwangu hizo foleni za magari mjini dar ni uzembe wa kutengeneza miundo mbinu inayoendana na wakati ikiwa ni pamoja na kupanua barabara, kuongeza barabara na kuhakikisha sehemu zote zinazokaliwa na watu kunakuwa na barabara za kupitika.

Tanzania hatuna magari ya kuwa na msongamano kama unavyoonekana wakati wamiliki wa magari jiji la Dar ni sawa na 1/8 na pengine pungufu ya hapo ya wakazi wa jiji hili, tofauti na nchi zilizoendelea wastani wa kila familia ni magari mawili. Je, Tanzania tukifikia wastani wa robo ya wakati mijini wawe wanamiliki gari hali itakuwaje?

Fikiria unakoishi na unakofanya kazi, njia ambayo unatumia kufika kazini ni ya mzunguko usio muhimu, lakini barabara zote zenye uwezekano wa wewe kufika kazini kama zengetengenezwa kwa kiwango husika huoni kama msongamano barabara ile unayopita usingekuwepo na pengine ungekuwa na alternative ya kupita kusiko na msongamano?
 
Mkuu naomba kukuuliza swali kidogo, kwa sasa una kazi au bishara yoyote ambayo inakuingizia kazi hapa bongo? Kama ni ndio au hapana achana na hiyo habari ya kurudi kwenye kupiga box! Kutokana na maelezo yako inaonekana kuna vitu viwili vinakupa changamoto, kwanza ni inawezekana hauja "settle" kimaisha toka uliporudi bongo (ndio maaana unafikiria kurudi kupiga box) na ya pili ni kuhusu hiyo project yako ambayo ukitulia na kwenda nayo taratibu utaweza kufanikasha kama wadau wengi walivyochangia.

Mimi binafsi niko kwenye situation kama ya kwako na nina project ya kuanzisha "Sport Academy" na challenges unazokutana nazo nami pia ninakutana nazo sana. Mawazo yaliyotolewa hapa ni bab kubwa, hakuna kurudi utumwani!
 
Nimekupata vizuri tu Leornado, lakini fikiria majuzi tu kule bungeni waziri Mwakiembe alitahadharisha magari ya abiria kutosimama barabarani kuruhusu abiria kwenda kuchimba dawa porini.

Hoja ya Mwakiembe haina mantiki kwa vile huwezi kuzuia jambo hilo wakati serikali haijajenga vituo vya kupumzika kando ya barabara kuu kila baada ya mwendo wa urefu unaokubalika ambapo vituo hivyo vingekuwa na sehemu za kujisaidia. Hata hilo kama atajitokeza mmoja kutaka kuwekeza utaniambia bado kwa sasa Tanzania hatuhitaji?

Wazo ni zuri ila kwa Tanzania baado sana sana. Usisahau kuwa una mawazo from first world wakati Tanzania ni zero maisha yetu ni as if tunecheza mchezo wa watoto wa kujipikilisha usio na maana.
Ukitaka kujua asilimia 70% ya watanzania ni maskini wa kutupwa wasio hata na nyumba za bati temebelea vijijini, nilitembelea mikoa mitano ya tz mwaka huu hadi leo najisikia vibaya sana kuwa kuna watu bado karne hii wanaishi vile na serikali tunayo sema serikali yetu imejikita mjini na kusahau wenzetu wa vijijini.

Hii ya kuchimba dada haitekelezeki bila kuwa na vyoo mbadala.
 
Nilijitutumua kuingia mpaka office ya Mkurugenzi wa maendeleo Mkoa wa Dar kumshauri kuhusu tatizo la msongamano wa magari kwamba ni shida inayowezekana kuondokana katika muda mfupi iwapo tu watafanya yafuatayo:
  1. Kujenga belt-way (park way) ambayo itaanzia Mbezi beach kupitia Mbezi Juu, Pugu, Mbagala hadi kuunganisha kule Mji Mwema kwa Abdu Jumbe na kuishia Kivukoni kwa kiwango cha express high way.
  2. Kujenga barabara kadhaa ambazo zitaunganisha na hiyo belt-way (park way) kuunganisha na maeneo mengine, na kubuni barabara nyingi mitaani zinazounganika na barabara kubwa kama Kilwa Road, Bagamoyo Road, Morogoro Road, Pugu Road.
  3. Kuhakikisha barabara zote za mitaani ni nzuri na zinapitika wakati wote ili watu wawe na alternative ya kuchagua njia.
  4. Kuruhusu commuter bus zenye kuchukua watu kuanzia 45 sitters badala ya madogo ambayo huongeza msongamano kwa wingi wake.
  5. Kuwepo na usafiri wa train kwa baadhi ya maendo ambayo yana msongamano msongamano zaidi. Mfano Gongolamboto kuna reli imepita pale, kama kungekuwa na train ingerahisisha kupunguza watu kudandia kupitia madirishani.

Ushauri wangu huo ulijikita katika maana ya kwamba miji mkubwa daima njia zinatengenezwa kwa kichocheo cha kuvutia watu kupita nje kidogo ya mji ili kupunguza msongamano, la sivyo kujanga fly overs katikati ya jiji kwa sasa hivi maana yake ni kuendelea kuweka vivutio vya magari kujaa mjini ambako hakuna sababu, ampapo magari yanayoenda mjini yangekuwa ni yale yanayohitaji kwenda huko tu.

Pole sana Mkuu......mawazo yako ni mazuri......kuna mawazo mazuri mengi sana yalikwishatolewa na wataalamu mbalimbali awali (through tafiti and proposals).....sasa kama yanafanyiwa kazi au lah hilo ni suala jingine......

Je ulimuuliza wana mipango gani?....na alikujibu nini?.....nina imani mazungumza yako hayakuwa one way traffic.......sidhani kwamba alikusikiliza tu....tuambie alisema nini juu ya mawazo yako na wao wanafanya nini sasa hivi.........mipango mingi ya maendeleo na maboresho inahitaji pesa......sasa kinachotakiwa ni priorities ili kuweza kutimiza yale yaliyopo na uwezo wa kifedha zilizotengwa.....

......mfano....... PPP models zina apply sehemu nyingi tu kwa maendeleo ya Mji wa DSM........lakini unakuta wapuuzi na mafisadi wanahujumu ili kujinufausha wao.......hebu angalia mfano Kituo cha mabasi Ubungo.......hivi kuna maboresho gani pale......yaani akina Kinje wamekula pesa weee.....na sasa wamehamia kwneye biashara zingine.........
 
Kama mtu yuko majuu anapiga boksi halafu anajenga nyumbani siwezi kumlaumu sana. Tatizo wengi wamekaa nchi za watu lakini hawana maendeleo yoyote. Nyumbani hata banda la nyasi hana. Hana vitega uchumi vya aina yoyote ile. Akirudi anaenda kukaa nyumbani kwa mama au sijui kwa shemeji yake. Yaani wanajipotezea muda halafu maisha ni mafupi. Unapiga boksi, mvi na upara vinaota lakini huna mbele wala nyuma kimaisha. Hizo nguvu za boksi unafikiri utakuwa nazo milele? Ukichoka jee utakuwa mgeni wa gani?
 
Mungu awe nanyi katika mipango yenu, binafsi imenifungua masikio.
Thanks a lot.
 
Back
Top Bottom