Waliochagua kubaki kupiga box majuu waliona mbali

Pole sana ndugu. Nakuelewa sana unachomaanisha. Ila kwa bahati mbaya mtu ukshakuwa nje ya nchi unarudi na mtazamo na uelewa ambao kiukweli kama mtu hajawahi kufika hata hapo Kenya ni ngumu sana kuelewa. Kuna swala laku supply kulingana na demand ila pia kuna possibility zaku create demand ili uweze kusuply. Tz bado sana! Unajua mtu ukiwa hapo Tz unafurahia kusema mi mnyakyusa, mpare, mchaga n.k. Ila siku ukitoka nje ya Tz ndiyo unaelewa nikwajinsi gani utanzania unakuhusu na jinsi hali ya nchi inavyoweza kukufanya ukafeel guilty kama vile wewe ndiyo rais wa nchi. Still we have a long way to go for people to understand the meaning, value and worth of being Tanzanian
Kwa kweli umesema kila kitu! mara nyingi hata hili ulilozungumza hapa la kujisikia guilty pale watu wanapokuuliza iwapo rahisi wa nchi yako amesoma kidogo economics au " what is his profession" watz waliowengi ambao ndo hawajatoka nje hawatakaa walione kamwe! mtu anaweza kuku embarass kwa vitu ambavyo ukiwa bongo unaona ni sawa tu kwa vile kila kitu tunasubiri waje wageni hata wakenya na waganda ndo wafanye kuliko sisi kuanzisha! bado ni safari ndefu na itaendelea kutudhalilisha
 
Hali ya mazingira ya kukatisha tamaa kwa watanzania kutokana na serikali kutojali maisha ya watumishi wa umma na wananchi, nabadili mawazo na kuwa waliobahatika kuwa huko majuu na kupata nafasi ya kupiga box waliona mbali kuliko tulioamua kurudi kwani tumepoteza hata mafao tuliopigia box. Inakatisha tamaa mambo yasiyvyoleta matumaini na kwa kuwa sikutupa jongoo na mti wake naamua kuridi kupiga box ughaibuni pamoja na kwamba nako maisha magumu yanawafungua macho wazungu waliozoea kutupa hifadhi katika nchi zao.

Nimejitahidi kuishawishi serikali katika mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka kuchukua maeneo ya wazi kimkataba ambayo yalitengwa kwa ajili ya michezo na burudani mbalimbali ili niyaendeleze kwa malengo yayo hayo kuwa viwanja vizuri vya michezo na bustani za mapumziko, nimeishiwa kutishiwa mambo ambayo sikutegemea. Kitu kama hicho ndicho kinachofanyika katika nchi nilikokuwa napiga box na mtu anayejitolea kufanya hivyo anaonekana yupo kwenye chanda cha dhahabu ndani ya kisahani lakini bongo unaonekana usiyefaa na wa kutaka kujineemesha wakati sitahitaji pesa toka serikalini na maeneo hayo yanazidi kutia aibu kila kukicha. Kuna mengi ila sipendi kuyatapika hapa.

Ndugu yangu naomba utambue kuwa wanaobaki au kuamua kurudi nyumbani wamefanyahivyo kama kujitoa muhanga. Kama bado hujakata tiketi nakushauri ueendelee kidogo kuvuta muda hapo usaidie kuleta mabadiliko walau kidogo. Please be aware that everything in Dar is de minimis, so patience and politeness are needed to transform this country, you may add other 2 Ps (persistence and perseverance) into the equations also. Please be advised that those system guys who you managed to talk to understand you very well but they're always looking for themselves first, yaani...if you have to upgrade those community plots to public parks, they (themselves) they are not going to benefit because the project will be fully private funded and chances of kick backs are low. If say, you get a politician to help you get government funding to upgrade those plots, for sure you will have close to 99.99% of their support. Same analogy applies to your suggestions on decongestion of the City of Dar es Salaam. If you want to understand what I am talking about please find a way to be employed in the government even in short term basis and at least look for at least a deputy director position............
 
Kila jambo na wakati.

Huwezi fanya jambo kabla ya wakati.


Huu ni wakati wa ubinfasi.
Siku itafika tutakapo taka huduma ya kijamii.

Vipanya ni tatizo Dar lakini ndo nafuu ya watu kadhaa.

Mji mkubwa kama Dar ahauwezi kuhudimiwa na panya ni Wazimu.

Mifereji ya maji machafu common sewage system ni muhimu.
Dar kila mtu achimba shimo lake mwenyewe vinyesi kila kona.
Ni unafuu wa watu kadhaa na kiraha ya wengi

hakuna open space, zimekwenda wapi??

Wakuu wamegawana wamejenga nyumba zao na za mahawala zao.

Master plan ya jiji kule wizarani bado inaonyesha open space.
siku ikifika NYUNDO tu.

Sioni haja ya kumlaumu mleta mada.

Mambo ya Bongo mengi ni ya kienyeji na yanaudhi.

Kule Rwanda ujinga kama huu wa Bongo umefutika kabisa.
Tena ni marufuku hata kujitamburisha kwa Utusi na Uhutu.

Mleta mada nimekuelewa vizuri.
Nakuomba usife moyo endelea mbele,
Wako wengi wanawaza kama wewe na zaidi,
wanasubiri wakati MWAFAKA.
Mawazo yako yaweke katika maandishi siku si nyingi utaya hitaji kivitendo.
 
Umefunua kitu ambacho huenda wengi hawakijui kuhusu Public Procurement Act ya Mwaka 2004, ungajaribu kutufafanulia kwani kuna wengi wanaotaka kuijua zaidi ya huyu Njele.

Shukurani.

Hii Act ni pana, nakumbuka nishamuwekea Mkandara hapa katika thread moja niliyokuwa namcharaza Mhando wa TANESCO kwa ufedhuli wake. Nilimpa Mkandara kipengele cha kuanzia.

Ingesaidia zaidi kama kuna uelewa zaidi unaoweza kutoa majibu zaidi na uliosababisha sheria hii ikawekwa hapa, tupewe uelewa huu kama mtoa document anavyoelewa. Au hata tupewe kurasa/ ibara husika.

La, shukrani kwa homework.
 
Hali ya mazingira ya kukatisha tamaa kwa watanzania kutokana na serikali kutojali maisha ya watumishi wa umma na wananchi, nabadili mawazo na kuwa waliobahatika kuwa huko majuu na kupata nafasi ya kupiga box waliona mbali kuliko tulioamua kurudi kwani tumepoteza hata mafao tuliopigia box. Inakatisha tamaa mambo yasiyvyoleta matumaini na kwa kuwa sikutupa jongoo na mti wake naamua kuridi kupiga box ughaibuni pamoja na kwamba nako maisha magumu yanawafungua macho wazungu waliozoea kutupa hifadhi katika nchi zao.

Nimejitahidi kuishawishi serikali katika mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka kuchukua maeneo ya wazi kimkataba ambayo yalitengwa kwa ajili ya michezo na burudani mbalimbali ili niyaendeleze kwa malengo yayo hayo kuwa viwanja vizuri vya michezo na bustani za mapumziko, nimeishiwa kutishiwa mambo ambayo sikutegemea. Kitu kama hicho ndicho kinachofanyika katika nchi nilikokuwa napiga box na mtu anayejitolea kufanya hivyo anaonekana yupo kwenye chanda cha dhahabu ndani ya kisahani lakini bongo unaonekana usiyefaa na wa kutaka kujineemesha wakati sitahitaji pesa toka serikalini na maeneo hayo yanazidi kutia aibu kila kukicha. Kuna mengi ila sipendi kuyatapika hapa.
Kwa pale Bongo usishangae kusikia kuna mtu kigogo/jamaa wa kigogo ambae anachukua fungu la pesa toka serikalini kwa ajili ya kuviendeleza hivyo viwanja na pesa anfanyia matumizi binafsi. Sidhani kama City wao hawaoni hali halisi ya hivyo viwanja.
Karibu kwa kila tatizo unaloliona bongo, yupo ambae ananufaika nalo. Watu wanatakiwa wabadilike.
 
Asiwadanganye mtu maisha ya kubeba box sio maisha kabisa.. Bora hata bongo unaweza kua na kajibiashara kako au kama umesoma ukapata kazi na kujiendeleza... Ulaya hujiendelezi kabisa unaishi kama mtumwa huyu mtoa mada ana frustrations tu za maisha mbona wazungu wanakimbia nchi zao si wangebaki wabebe mabox?
 
Wamisionari walipokuwa walikuja kutalii kuangalia kama waafrika tunahitaji dini?
Wakoloni walipokuja kututawala tulishakuwa na watawala wetu na waliingia kwa nguvu ya magobole, kwani waafrika tulihitaji hawa wazungu waje kututawala au vipi?

Hitaji lipo, utakuwa watu wanavyofurahia bustani za Mnazimmoja, pale St. Joseph, kule kwenye mchezo wa golf nk.
  • Ni hakika bustani zinahitajika
  • Ni hakika vijana wanahitaji viwanja vizuri vya kuchezea michezo
  • Ni hakika watoto wanataka maeneo mazuri ya kuchezea, leo Idd tazama walivyojazana ufukwe wa Bahari au kile kitega uchumi Mbagala, ila wakuu wetu hawafunguki.

Inawezekana huyu Njele alishaona wazo lake linapokeleka, na hajalalamika kwamba wananchi walimkatisha tamaa, bali anasema viongozi wa serikali ndo waliomtisha na kumkatisha tamaa. Tutetee mambo kwa misingi ya ukweli katika mazingira ya leo.
Hahaha! Sikukuu ya Iddi watoto wa Manzese wote tunaishia juu ya daraja la Manzese. Njele uko sahihi zaidi ya correct. Sijuwi hao wapumbavu wanatetea nini. Wamejenga eneo la wazi nini!!!?. Wachunguzwe.
 
acha kutetea ujinga...sehemu za kupumzikia ni muhimu vilevile so unataka watu wawe wanakaa kama vile pale Coco na kula mihogo na harufu ya kinyesi kwenye vile vichaka pale?......na hiyo Haki Elimu unayoisema wanaofaidi labda wale walioajiriwa sana sana ni mchongo wa kupata funds tu toka kwa Donors....maana eti inatoa taarifa za seka ya elimu Tanzania..wakati nani asiyejua kwamba system ya elimu Tanzania kwa ujumla ni mbovu.
 
Kijakazi una mtazamo mzuri kwa maana kuwa una sisistiza kwamba ungekuwa wewe ungejua kuwa hilo wazo haliwezekani hapa tz. lakini napenda kutofautiana na wewe kwa mambo mengi lkn hapa nitazungumza kifupi tu. kiukweli kabisa, ni wajibu wetu kuleta new ideas ambazo zinaongeza tija na zenye less competition kwa sababu zinaongeza diversification badala ya kubaki na idea za kuuza juice au kufuga kuku wa nyama na mayai kama ilivyozoeleka kwa kila mkasiriamali. Wengi wetu humu tumeishi ng'ambo na tungetamani kuona vitu vizuri vyenye kuonyesha ubunifu ktk mazingira ya Afrika ukileta manufaa kwetu na faraja. Tatizo ninaloona mimi and correct me if Im wrong, ni kwamba kuna long term target ya watu fulani (wakubwa) kuvichukua hivyo viwanja na hivyo kuifanya idea nzima kushindikana maana itakuwa vigumu wahusika kuviomba kiujanja wakati tayari vimeshagawiwa kwa mtu mwingine. kama alivyoeleza hapo juu Njele, ni kweli wazungu na wahindi wanafanya kile tunachoita "ukila na kipofu usimguse mkono" wanahakikisha wanajifanya wako ktk level sawa na sisi na kutimiza "business as usual" lkn kimsingi wanakuwa na malengo yao yaliyojificha. Endapo tutashindwa kuona point ndani ya hii observation ya Njele basi tutakuwa kama vipofu na huenda kwa miaka hii watanzania wataungana na wale wa west Africa ambao wakifika ulaya hawataki kusikia jina la nchi yao tena kwa kisingizio kuwa hakuna social security na uonevu ni mkubwa maana bado serikali ziko barbaric. TUFUNGUE MACHO TUSISUBIRI WACHINA, WAHINDI NA WAZUNGU KUANZISHA VITU VYOTE VIPYA NA KUTUFANYA SISI TUWE WATU WA KUFUATA TU BILA HATA KUULIZA.

Sawa kabisa hakuna sehemu mimi nilipopinga maendeleo ila kinachoniudhi ni pale mtu anapokuja kutoka nje na kutaka mambo yaende kama anavyotaka yeye au kama huko alikotoka wakati yeye alizaliwa hapa kakulia hapa kasoma hapa sia ajabu hata yeye asingepata nafasi ya kwenda huko nje na yeye angekuwa na mtazamo kama wa watz wengi.

Kama una wazo jipya ni lazima ulipiginie bila hivyo haiwezekani na hiyo nafikiri ni kila mahali kama inabidi uhonge ili ufanikiwe so be It, lakini kuja hapa na kufikiri kwamba unaweza ukabadilisha watu unapoteza muda!

Mimi naamini kabisa mtu kama una winning spirit unaweza kufanikiwa popote pale, na ndio maana nikatoa mfano wa wazungu au wahindi wanakuja hapa hata kiswahili hawajui wanakwenda vijijini huko wanajifunza lugha wanaelewa utamaduni wa watu wanapiga kazi wanafanikiwa mbona hawalilii hovyo, na hiyo sio wenye miradi mikubwa mimi namjua mzungu mmoja mbelgiji kaja hapa hata na mtaji sio mkubwa hivyo kaanzia chini kabisa kaanzisha kampuni ya mambo ya umeme electrical installations alianza na watu 3 miaka 5 baadae ameajili watz 40, anatumia milioni 50 kwa mwezi kwa mishahara tu, na ukiongea nae akikwambia roadblocks alizopambana nazo huwezi amini lakini leo huyo katoka, fikiria ilibidi ajifunze kiswahili ili tu aweze kuwasilana na kuwaelekeza wafanyakazi nini cha kufanya achilia mbali makashi kashi ya serikali, sasa kwa nini sisi tushindwe wakati ni wa hapa hapa?

Na anaishi na wafanyakazi vizuri na wanampenda na wala hajaribu kutaka kuwabadilisha wawe wazungu, mtu akileta mambo sijui kufiwa au kuuguza unakwenda lakini lazima ulipie siku kwa overtime na inawezekana, sasa sisi yuliozaliwa hapa kwa nini tunalalamika tu na kutaka kubadilisha watu?
 
Sijui ndugu una draw argument yako ukirefer wapi! Kutokana na expeience, exposure au ni kwakufikiri tu! Kwanza kabisa nataka nikuambie hata kama mtanzania na mzungu wange bid for the same tender nawakasubmit kila kinachotakiwa at the same time. Tender atapewa mzungu na siyo mtz. Mifano hii iko wazi sina haja yakueleza! Hii inaonyesha wazi ni jinsi gani serikali na Watz walio wengi bado hatuna ile element ya 'usisi' na tunathamni wageni kuliko wazawa!
Pili nataka nikuambie kuna watz wenye hela zao nyingi tu na hawana mahali pakuzispend au mazingira hayako comfortable kwao! Ukumbi wa Dar live ulikuwepo? Ulijua kama endapo huo ukumbi baada yakujengwa ungejaza watu kama ilivyo sasa? Mlimani city ilikuwepo? Je baada yakuwepo unaona watu wanavyojazana? I think you should not underate the Tanzanians we deserve the best just like those Europeans and others. Chamuhimu tunie kuleta mabadiliko ili kila mtu aweze kuishi comfortable since we have one life and we have to live it! Tukibadili mtazamo tutabadili kutenda kwetu na mabadiliko yakweli automatically yatakuja! Let's do it kuliko kukatishana tamaa!





Na hapo ndio mnapokosea kwa maana mko out of touch na ndio maana nikakutolea mfano wa wazungu au wageni wengine kabla hawajaamua kuja Tanzania wanafanya kwanza utafiti na wanajifunza nakusoma kwanza watu wakoje na wanautamaduni gani kwa hiyo hawezi kuja hapa na kuanza kuongelea mambo ya kujenga bustani ya kupumzikia wakati huyo unaemjengea wala haelewi maana ya hicho kitu, ana matatizo mengine kabisa, ukimwambia mtanzania wa kawaida kwamba watoto hawana mahali pa kuchezea eti unataka kuwajengea hawezi kukuelewa, na ndio maana hata ukiaangalia makampuni makubwa kwa mfano Samsung wanauza bidhaa ambao ziko tofauti na bidhaa za wanazouza sehemu nyingine unafikiri kwa nini? si wanajua mazingira ni tofauti, TV inayotengezwa for African market sio sawa na for European market huo ni mfano tu!

Kwa hiyo wazo lako labda sio baya lkn kwa kwetu hapa halitaeleweka, ni bora hata ungeanzisha tuition kwa watoto ya kujitolea bure hapo ungeeleweka! kuna kina kitabu kinaitwa "what makes people tick"
ukikisoma kinaelezea jinsi ya kuweza kutambua tabia na tamaduni za watu ili uweze kuishi na kuendana nao vinginevyo utakuwa unaonekana kichekesho kwa sababu hutaeleweka!
 
Mkuu, ulichotaka kufanya wewe ni kuuza huduma. Ulichotakiwa kufanya ni kusoma vizuri na kuielewa Public Procurement Act ya mwaka 2004, halafu ungejua nini cha kufaya ili ufanikiwe kuuza huduma yako.

Maana ya kuuza huduma sijakudaka bado, ninachojua kama raia mwema mwenye mapenzi kwa nchi yangu na kadiri viongozi wa nchi walivyokuwa wanatutembelea na kutukazia kurudi kusaidia kwa njia ye yote njema kujenga nchi yetu,ndio mwamko nilikuwa nao na sasa nakutana na vipingamizi ambavyo rais alipotuusia huko majuu hakutuambia matatizo tunayokutana nayo, na sasa tunapokutana na matatizo kama hayo kuna uzio mkubwa ambao vigumu kumfikishia rais aliyetualika.
 
Sasa wewe unang'ang'ania huko ughaibuni, ni nani atakayeleta mabadiliko hapa nchini. Rudi, mchango wako unahitajika.
 
sijui ndugu una draw argument yako ukirefer wapi! Kutokana na expeience, exposure au ni kwakufikiri tu! Kwanza kabisa nataka nikuambie hata kama mtanzania na mzungu wange bid for the same tender nawakasubmit kila kinachotakiwa at the same time. Tender atapewa mzungu na siyo mtz. Mifano hii iko wazi sina haja yakueleza! Hii inaonyesha wazi ni jinsi gani serikali na watz walio wengi bado hatuna ile element ya 'usisi' na tunathamni wageni kuliko wazawa!
Pili nataka nikuambie kuna watz wenye hela zao nyingi tu na hawana mahali pakuzispend au mazingira hayako comfortable kwao! Ukumbi wa dar live ulikuwepo? Ulijua kama endapo huo ukumbi baada yakujengwa ungejaza watu kama ilivyo sasa? Mlimani city ilikuwepo? Je baada yakuwepo unaona watu wanavyojazana? I think you should not underate the tanzanians we deserve the best just like those europeans and others. Chamuhimu tunie kuleta mabadiliko ili kila mtu aweze kuishi comfortable since we have one life and we have to live it! Tukibadili mtazamo tutabadili kutenda kwetu na mabadiliko yakweli automatically yatakuja! Let's do it kuliko kukatishana tamaa!

yaani wewe umeongea...i second you for that....its sad, lakini maisha ndivyo yalivyo. Pole muanzisha mada, i know where you're coming from.
 
Shida ni kwamba huyu kama ukisoma origin post yake analalamika kwamba ameshindwa na sasa anarudi alikotoka, na mimi ndio nikamwambia hiyo ni kawaida ya watz wanaoishi nje (sio wote) wakija hapa wanataka wote tubadilike tuwe kama wao wanasahau kwamba sisi tumelelewa vingine na tuna priorities tofauti, kwa hiyo japokuwa kuwa na bustani sio jambo baya lkn haliwezi kuwa priority kwa mtz wa kawaida na hawezi kukuelewa, kwa hiyo leo hii ukienda ofisini kwa mtu halafu unaanza kumwambia unataka kujenga sijui bustani atakupuuza tu!

Tanzania sasa hivi tuna matatizo mengi sana wadogo zetu hawasomi hawana vitabu, wengine hawawezi hata kwenda shule kisa njaa, wengi wanashindwa kulipa sh 2000 kwa mwaka kwenda shule huwezi amini lkn ndio ukweli sasa mambo ya bustani ya kupumzika yana nafasi kweli?


Nchini Marekani miaka mingi iliyopita hali ilikuwa kama Tanznaia ambapo maeneo ya bustani za kupumzikia yalikuwa haba na hakuna aliyekuwa anayatunza ingawa maeneo yalikuwa yametengwa tayari na pengine kutotenda na hivyo kuyanunua kwa malengo ya vizazi vijavyo. Kwa makusudi kuna aliyejitokeza kujenga hali ambayo kwa sasa wengi wanaifurahia kama picha zionekanavyo hapa chini.

An urban park, also known as a municipal park (North America) or a public park, public open space or municipal gardens (United Kingdom), is a park in cities and otherincorporated places to offer recreation and green space to residents of, and visitors to, the municipality. The design, operation and maintenance is usually done by government, typically on the local level, but may occasionally be contracted out to a private sector company.
Common features of municipal parks include playgrounds, gardens, hiking, running andfitness trails or paths, bridle paths, sports field and courts, public restrooms, boat ramps and/or picnic facilities, depending on the budget and natural features available.

220px-Central_Park_from_Rock.jpg
220px-%C5%9Al%C4%85ski_Ogr%C3%B3d_Zoologiczny_-_kotlina_dinozaur%C3%B3w.jpg
220px-Piedmont-park-urban-park.jpg
220px-Lago_del_rosedal_palermo_chico.jpg


Kizazi cha leo tusipofanya haya hata watoto na wajukuu wetu wabaki kutulaumu wakati nafasi na mazingira ya leo kufanya jambo hili inawezekana? Challenges ni kitu cha kawaida, lakini nia ingali pale pale, na kama narudi majuu ni shauri ya kusubiria muda kama wadau wengi walivyonishauri hapa.

Nawashukuru wadau wengi mlivyo nipa moyo, yote nimeyahifadhi kwa lengo kwamba ipo siku system itabadilika na kuruhusu wenye nafasi ya kufanya mazuri kwa nchi yetu hawatawekewa mikwara.

Sina nia ya kuhodhi maeneo hayo, bali najitolea kuyaandaa kwa mkataba, na pale jiji, halmashari itakapokuwa tayari kuyahudumia baada ya mkataba kuisha ni vema tu maana utume wangu utakuwa umekamilika kwa wakati kwa ajili ya vizazi vijavyo.
 
In the early 1900s, according to Cranz, U.S. cities built neighborhood parks with swimming pools, playgrounds and civic buildings, with the intention of Americanizing the immigrant residents. In the 1950s, when money became available after World War II, new parks continued to focus on both outdoor and indoor recreation with services, such as sports leagues using their ball fields and gymnasia. These smaller parks were built in residential neighborhoods, and tried to serve all residents with programs for seniors, adults, teens and children. Green space was of secondary importance.
As urban land prices climbed, new urban parks in the 1960s and after have been mainlypocket parks. These small parks provide greenery, a place to sit outdoors, and often aplayground for children.
All four types of park continue to exist in urban areas. Because of the large amount of open space and natural habitat in the former pleasure grounds, they now serve as important wildlife refuges, and often provide the only opportunity for urban residents to hike or picnic in a semi-wild area. However, these parks can be targeted by city managers or politicians as sources of free land for other uses. Partly for this reason, some of these large parks have "friends of X park" advisory boards that help protect and maintain their semi-wild nature.
images
images
images
images
images
images


Kuna waliojitolea kuandaa maeneo mazuri ya kupumzikia kama haya, na baada ya machache kuonekana yanawavutia wengi, serikali ilifunguka na kununua maeneo zaidi kwa kuyaandaa kwa ajili ya mapumziko na michezo mbalimbali ambayo ni huru kuyatumia bila malipo kwa kuwa yanahudumiwa na serikali.


 
Hali ya mazingira ya kukatisha tamaa kwa watanzania kutokana na serikali kutojali maisha ya watumishi wa umma na wananchi, nabadili mawazo na kuwa waliobahatika kuwa huko majuu na kupata nafasi ya kupiga box waliona mbali kuliko tulioamua kurudi kwani tumepoteza hata mafao tuliopigia box. Inakatisha tamaa mambo yasiyvyoleta matumaini na kwa kuwa sikutupa jongoo na mti wake naamua kuridi kupiga box ughaibuni pamoja na kwamba nako maisha magumu yanawafungua macho wazungu waliozoea kutupa hifadhi katika nchi zao.

Nimejitahidi kuishawishi serikali katika mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na kutaka kuchukua maeneo ya wazi kimkataba ambayo yalitengwa kwa ajili ya michezo na burudani mbalimbali ili niyaendeleze kwa malengo yayo hayo kuwa viwanja vizuri vya michezo na bustani za mapumziko, nimeishiwa kutishiwa mambo ambayo sikutegemea. Kitu kama hicho ndicho kinachofanyika katika nchi nilikokuwa napiga box na mtu anayejitolea kufanya hivyo anaonekana yupo kwenye chanda cha dhahabu ndani ya kisahani lakini bongo unaonekana usiyefaa na wa kutaka kujineemesha wakati sitahitaji pesa toka serikalini na maeneo hayo yanazidi kutia aibu kila kukicha. Kuna mengi ila sipendi kuyatapika hapa.
Usikate tamaa kabisa CCM inaishia kaburini. Haya mambo yatatekelezeka miaka mitatu tu ijayo. Achana kwanza na Dhaifu. Hata wale watoto wa primary walimshtukia juzi. Alipanick sana lakini ukweli ni kuwa tutakuwa na serikali endelezi siku za kabibuni. Ukiona vinaharibika sana, kumbuka vizuri haviko mbali.
 
Maana ya kuuza huduma sijakudaka bado, ninachojua kama raia mwema mwenye mapenzi kwa nchi yangu na kadiri viongozi wa nchi walivyokuwa wanatutembelea na kutukazia kurudi kusaidia kwa njia ye yote njema kujenga nchi yetu,ndio mwamko nilikuwa nao na sasa nakutana na vipingamizi ambavyo rais alipotuusia huko majuu hakutuambia matatizo tunayokutana nayo, na sasa tunapokutana na matatizo kama hayo kuna uzio mkubwa ambao vigumu kumfikishia rais aliyetualika.

unapoishawishi serikali ikupe eneo uliendeleze unakuwa unaiuzia huduma serikali. Ukipewa wewe eneo hilo kinyemela yataibuka malalamiko. PPA 2004, inasimamia jinsi serikali inavyoweza kutoa tenda kama hizo. Kama vipi, tupe concrete example ya park uliyotaka kupewa na uzoefu wako katika shughuli hiyo. Hata ughaibuni hakuna nchi ambayo raia anaenda tu serikalini na kusema yeye apewe eneo fulani la mji ajenge park! park husimamiwa na serikali za miji husika kwa kushirikiana na makampuni yaliyoshinda tenda kwa kufuata sheria ya manunuzi.
By the way, nchini kwako hukaribishwi! hakuna mtu aliyekukaribisha Tanzania toka ughaibuni...
 
Shida ni kwamba huyu kama ukisoma origin post yake analalamika kwamba ameshindwa na sasa anarudi alikotoka, na mimi ndio nikamwambia hiyo ni kawaida ya watz wanaoishi nje (sio wote) wakija hapa wanataka wote tubadilike tuwe kama wao wanasahau kwamba sisi tumelelewa vingine na tuna priorities tofauti, kwa hiyo japokuwa kuwa na bustani sio jambo baya lkn haliwezi kuwa priority kwa mtz wa kawaida na hawezi kukuelewa, kwa hiyo leo hii ukienda ofisini kwa mtu halafu unaanza kumwambia unataka kujenga sijui bustani atakupuuza tu!

Tanzania sasa hivi tuna matatizo mengi sana wadogo zetu hawasomi hawana vitabu, wengine hawawezi hata kwenda shule kisa njaa, wengi wanashindwa kulipa sh 2000 kwa mwaka kwenda shule huwezi amini lkn ndio ukweli sasa mambo ya bustani ya kupumzika yana nafasi kweli?


Nimependa mwono wako kwamba unatambua matatizo kadhaa na kwako ukitanguliza tatizo la kukosekana kwa vitabu mashuleni kitu kinachosababisha wadogo zetu kukosa kupata elimu inayofaa kwa ajili ya future yao. Ningefurahi kama ungajaribu kutambua maana ya kupanua wigo katika masuala ya maendeleo, wewe mwenzangu saidia elimu, mimi mazingira, Sunshine huduma za afya, mwingine usafiri nk, huoni kama tutakuwa kwa kiwango fulani tumejitahidi kupanua wigo wa huduma badala ya mimi kufuata tu huduma ambayo we unasambaza vitabu wakati pale Mbagala wanatatizo la usafri watu kuwahi kazini? Vyuo vingi havina mazingira ya uwazi wanafunzi kupata sehemu ya kupumzikia kupata hewa nzuri wakati wakijisomea? Akina mama wanaopata taabu ya kujifungua kwa sababu hakuna wanaowekeza zaidi katika afya ili kunusuru afya ya mama na mtoto?

Unaonaje kama nguvu hizi tungeziunganisha kuendeleza nchi kwa kila aliye na nafasi na uwezo wa kufanya kitu fulani akifanye? Kumbuka maendeleo ya nchi si elimu tu, si sehemu za kupumzikia tu, si huduma za afya tu nk. Zote kwa pamoja zinakamilisha nchi kuendelea.

Kwamba tutazame upande mmoja tu ni sawa na ukifika pale Kariakoo mitaa kando ya mzunguko wa uhuru maduka yananayouza simu na vifaa vyake huenda yanazidi hata 500 na zaidi, unaweza kuyapanga upande mmoja wa barabara toka Fire hadi Manzese. Hii ndiyo biashara ya kuiga, hakuna kubuni kitu kingine ambacho mtu anaweza kujihakikishia kuwa na kipato, na matokea yake mtu yupo na duka lake zinaweza kupita siku tatu hadi wiki moja hana mteja, kwani mitaa yote ile simu za aina moja tu za kichina mbona inachosha hata macho?

Tunahitaji kuwa wapana wa kubuni mambo ya maendeleo. Kwani hata hao wadogo zetu unaosema wanahitaji vitabu mashuleni, wakati wa mapumziko wanahitaji kwenda sehemu yenye uwazi na hewa safi kupumzika huku akisoma kitabu chake, kwani sehemu nyingi hewa nzito na hakuna kwa kupumulia, kwani toka kwenye daladala, majumbani, mitaani na makazini ni kupumuliana tu, kupokezana hewa ile ile, na pengine kuivuta hewa iliyopumuliwa na mwenzako, hayo ndiyo unayotaka ndugu yangu.

We msomi na umeendelea, tunatazamia utatusaidia kuibua mengi zaidi ya kupanua wigo katika maendeleo, kwani hatuwezi kuendelea kufanya mambo ya kuiga kwa jirani kwa vile ana cooler ya vinywaji baridi nami naagiza biashara hiyo hiyo. Kwa nini usifanye utafiti huduma gani watu hawana sasa hivi katika eneo hilo?
 
unapoishawishi serikali ikupe eneo uliendeleze unakuwa unaiuzia huduma serikali. Ukipewa wewe eneo hilo kinyemela yataibuka malalamiko. PPA 2004, inasimamia jinsi serikali inavyoweza kutoa tenda kama hizo. Kama vipi, tupe concrete example ya park uliyotaka kupewa na uzoefu wako katika shughuli hiyo. Hata ughaibuni hakuna nchi ambayo raia anaenda tu serikalini na kusema yeye apewe eneo fulani la mji ajenge park! park husimamiwa na serikali za miji husika kwa kushirikiana na makampuni yaliyoshinda tenda kwa kufuata sheria ya manunuzi.
By the way, nchini kwako hukaribishwi! hakuna mtu aliyekukaribisha Tanzania toka ughaibuni...

Serikali imelala kwa vile viongozi wanafikiria zaidi maisha binafsi kuliko uwajibikaji kwa jamii. Maeneo hayo yamesahauliwa na hata hayapangiwi bajeti, na hata kama bajeti yanayo inaishia kununulia soda wakubwa maofisini na kufanyia semina elekezi zisizoleta mabadiliko katika utumishi. Bajeti inayoidhinishwa na bunge badala ya kutumika kama ilivyokusudiwa kwa maendeleo, inatumika kufanya makongamano na semina elekezi na pesa inaishia huko pamoja na posho zake. Mtu binafsi hana nafasi ya kufanya kongamano au semina elekezi ya kutengeneza au kuyaendeleza maeneo wazi, ni kazi tu basi kadiri ya plan ambayo imeidhinishwa na idara husika za serikali.

Malengo ni kutoa mfano mmoja kwanza ambao unaweza kuwavutia wengi na kisha baada ya miezi au mwaka kuona eneo lilivyo kivutio itahamasisha maeneo mengine hata wewe ukaingia mkataba kuyaendeleza kwa utaratibu ambao mimi nilipanga kufanya. Serikali ikishakaa sawa na kuwa na uwezo wa kuyahudumia maeneo hayo, muda wa mkataba ukiisha basi, huduma hiyo inaweza kuhamishiwa kwenye halmashauri ya jiji au mji ili kuendelea kuistawisha. Huu ndio utaratibu ambao hata mataifa yaliyoendelea yamepitia na sasa maeneo hayo ni kivutio na hata wakuu wetu wanaposafiri wanaenda kubembea huko, hayakuja yenyewe, kuna watu waliojituma kubuni, kuyatengeneza na kuyaendeleza.
 
Serikali imelala kwa vile viongozi wanafikiria zaidi maisha binafsi kuliko uwajibikaji kwa jamii. Maeneo hayo yamesahauliwa na hata hayapangiwi bajeti, na hata kama bajeti yanayo inaishia kununulia soda wakubwa maofisini na kufanyia semina elekezi zisizoleta mabadiliko katika utumishi. Bajeti inayoidhinishwa na bunge badala ya kutumika kama ilivyokusudiwa kwa maendeleo, inatumika kufanya makongamano na semina elekezi na pesa inaishia huko pamoja na posho zake. Mtu binafsi hana nafasi ya kufanya kongamano au semina elekezi ya kutengeneza au kuyaendeleza maeneo wazi, ni kazi tu basi kadiri ya plan ambayo imeidhinishwa na idara husika za serikali.

Malengo ni kutoa mfano mmoja kwanza ambao unaweza kuwavutia wengi na kisha baada ya miezi au mwaka kuona eneo lilivyo kivutio itahamasisha maeneo mengine hata wewe ukaingia mkataba kuyaendeleza kwa utaratibu ambao mimi nilipanga kufanya. Serikali ikishakaa sawa na kuwa na uwezo wa kuyahudumia maeneo hayo, muda wa mkataba ukiisha basi, huduma hiyo inaweza kuhamishiwa kwenye halmashauri ya jiji au mji ili kuendelea kuistawisha. Huu ndio utaratibu ambao hata mataifa yaliyoendelea yamepitia na sasa maeneo hayo ni kivutio na hata wakuu wetu wanaposafiri wanaenda kubembea huko, hayakuja yenyewe, kuna watu waliojituma kubuni, kuyatengeneza na kuyaendeleza.

Mkuu, unachosema ni sahihi na naona hoja yako ni ya msingi kabisa. Hata hivyo, inabidi ujiulize huo mkataba utakaoufunga na serikali utafungwa kwa kutumia sheria ipi? Hakuna mkataba bila sheria. Ndio maana nikasema ipitie sheria ya manunuzi ya mwaka 2004.
 
Back
Top Bottom