Walioandaa mgomo UDSM kuadhibiwa

Walioandaa mgomo UDSM kuadhibiwa

Wafukuzwe tu, tena ingependeza rais awachape hata fimbo na kuwafukuza. Mi nilishasema tangu mwanzo kuwa serikali ya Dr Magufuli ilishajitanabaisha toka mwanzo kuwa wanafunzi lazima watapata mikopo hakuna wa kukosa sasa wao kilichowafanya wagome ni nini????? Wapumbafu sana hawa vijana. Mbona wafanyakazi wa halmashauri safari hii mishahara ilichelewa kwa siku kazaa mbona hawakugoma?? Ina maana hao vijana wanadharau serikali, wanamdharau rais. Yaani wafukuzwe wale wote waliochochea mgomo liwe fundishooooo.


Mara nyingi wanaofukuzwa na kuchapwa viboko huwa viongoz wako wa baadae na kukutawala mfano samwel sitta,zito kabwe......
 
Wanawaadhibu kukwepa aibu tu, walijinasibu mkopo fasta kwa wote, mambo yamekuwa kinyume kama awamu iliyopita tu, sasa kwa kuwa watoto wamemuumbua malaika hadharani wanafanywa kuku wa kafara, haita saidia kuwaumiza bali tekelezni waibu wenu mapema kama hela ilikuwepo kwa nini itoke baada ya mgomo? Malaika angeanza na bodi ya mikopo sio watoto wa maskini hawa.

Alafu mburulaz wajue huu mkopo walitakiwa wapewe mwezi April mwishoni lakini umecheleweshwa kwa mwezi mzima sasa hao wanafunzi mnataka wale mawe?? Notes wanunue na nini?? Bundles za kusomea watoe wapi??
 
Kama unafikiri watanzaniq wote wanamaisha kama yako pole sana. Umeenda chuo kweli wewe? Uliza ni wanafunzi wangapi wanshindwa kufanya usajili ili waweze kuingia darasani boom linapochelewa?
Ukitambua kuwa boom unayopewa university inakusaidia kutatua hata matatizo yako yasiyokuwa ya kitaaluma unawezaje kugoma boom ikichelewa? tumia akili ya kawaida (common sense, ingawa it may not common to you)
 
Wafukuzwe tu, tena ingependeza rais awachape hata fimbo na kuwafukuza. Mi nilishasema tangu mwanzo kuwa serikali ya Dr Magufuli ilishajitanabaisha toka mwanzo kuwa wanafunzi lazima watapata mikopo hakuna wa kukosa sasa wao kilichowafanya wagome ni nini????? Wapumbafu sana hawa vijana. Mbona wafanyakazi wa halmashauri safari hii mishahara ilichelewa kwa siku kazaa mbona hawakugoma?? Ina maana hao vijana wanadharau serikali, wanamdharau rais. Yaani wafukuzwe wale wote waliochochea mgomo liwe fundishooooo.

Mkopo ulitakiwa kuingia April mwishoni lakini wameingiziwa May 31.. Je wewe unaona hiyo ni haki?? Mwezi mzima huo waliocheleweshewa ulitaka wale nini na mahitaji mengine wayapataje..
 
Alafu mburulaz wajue huu mkopo walitakiwa wapewe mwezi April mwishoni lakini umecheleweshwa kwa mwezi mzima sasa hao wanafunzi mnataka wale mawe?? Notes wanunue na nini?? Bundles za kusomea watoe wapi??
Tatizo mashabiki wengi wa ccm hawajafika chuo so hawajui ugumu wa maisha ya pale wanafikiri ni sawa na shule ya bweni, utakula maharage ya shule na uji wa shule material anakuja nazo mwalimu ndio maana yanatoka povu tu hapa. Wangejua watoto wengine hata nauli tu ya kufika chuo imechangiwa na ukoo mzima wangefunga midomo yao kuwakebehi hawa vijana.
 
Ukitambua kuwa boom unayopewa university inakusaidia kutatua hata matatizo yako yasiyokuwa ya kitaaluma unawezaje kugoma boom ikichelewa? tumia akili ya kawaida (common sense, ingawa it may not common to you)

Ukishapewa pesa tena ambayo utailipa hutakiwi kuulizwa unaitumiaje... Hata ukiamua kulewa ni sawa tu..

Cha msingi ni kwamba muda wa kupewa pesa nyingine ukifika upewe chako.. Boom la pili walitakiwa kupewa April mwishoni, lakini wamepewa May 31.. Je hiyo ni sawa??
 
Miongoni mwa nchi zenye watu wanafki yetu inaongoza. Ulishawahi kwenda chuo wazazi hali zao ni za kawaida na unategemea boom kwanza kulipia ada ili uweze kufanyia usajili, then boom hilohilo ndio liendeshe maisha yako ya chuo, boom hilohilo utoe kidogo utume kwa wazazi ili maisha yao yasonge, then boom hilohilo usaidie wadogo zako, halafu hela hiyo unayoitegemea kwa hali na mali inacheleweshwa kwa sababu zisizo za msingi? Kama hujawahi kuwa katika hali hiyo huwezi jua kwanini wanafunzi wanagoma boom linapochelewa
Hayo mengine siyo kusudio la kutolewa kwa pesa hizi. Tuwe waungwana.
 
Tatizo mashabiki wengi wa ccm hawajafika chuo so hawajui ugumu wa maisha ya pale wanafikiri ni sawa na shule ya bweni, utakula maharage ya shule na uji wa shule material anakuja nazo mwalimu ndio maana yanatoka povu tu hapa. Wangejua watoto wengine hata nauli tu ya kufika chuo imechangiwa na ukoo mzima wangefunga midomo yao kuwakebehi hawa vijana.

Watu wajinga sana hawa... Ni hawahawa wakicheleweshewa mishahara kwa wiki tu inakuwa shida ila wanafunzi wamecheleweshewa pesa zao mwezi mzima alafu bado wanawatukana... Kama huyo magu alifikiri kuongoza nchi ni kama kusimamia barabara na madaraja atachemsha
 
Tukidai haki zetu wanasema utovu Wa nidhamu daah wanatakutuhadhibu kwa kulinda uovu wao.
 
Ukishapewa pesa tena ambayo utailipa hutakiwi kuulizwa unaitumiaje... Hata ukiamua kulewa ni sawa tu..

Cha msingi ni kwamba muda wa kupewa pesa nyingine ukifika upewe chako.. Boom la pili walitakiwa kupewa April mwishoni, lakini wamepewa May 31.. Je hiyo ni sawa??
kwa jiba lako (FisadiKuu), hoja yako ni sawa. Kumbuka mkopo una masharti yake pia.
 
kwa jiba lako (FisadiKuu), hoja yako ni sawa. Kumbuka mkopo una masharti yake pia.

Masharti ni kupewa kila baada ya miezi miwili... Sasa miezi ilishapita, watatu nao umepita bado mlitaka wakae kimya.. Au ndio ulofa na upumbavu tulioambiwa??
 
Wewe kabinti hujasoma peke yako hivyo vyuo na wewe si wakwanza kupokea hiyo pesa. Tatizo ni starehe za nyie vijana, na kutokuwa na nindhamu ya matumizi ya pesa.
Nyie mabinti kutoka katika familia za kawaida huwa mkifika huko hufanya kazi za kuoa wanaume masharobaro. Wewe ndio wa kununua vimodo kumlewesha kulipa chumba kisa ushamba. Vijana wa kiume ni kujipodoa ili kuwavutia mabinti wasiojitambua na ulevi. Ukiingia kwenye haya hiyo hele haikai ikatosha.
Nindhamu ya kutumia pesa ni muhimu kwa kuhakikisha kuwa unatumia akiba ya mwisho pale unapopata pesa nyingine na si vinginevyo. Tegemea ulichoshika mkononi usitegemee utakachotafuta.Serikali huudumia mambo mengi, inaweza tokea myumbo wa kikodi na makusanyo mkajikuta mnasubiri kwa muda mrefu. Baki na akiba angalau ya wiki tatu au mwezi wakiwahi burudika kidogo kisha funga mkanda.
unabwabwaja tu hata huelewi maana, unaweza kuweka akiba ya hela ambayo hujaishika?! Kama dadako ananunua wanaume ni huyo huyo si wanawake wote, pole kwa kushindwa malezi ya mabinti zenu hapo home, tukana hao si wa nje ya familia yako. Naona umekuzwa na pesa za hongo ndio maana umekariri akili ya kuhongwa tu.
 
Miongoni mwa nchi zenye watu wanafki yetu inaongoza. Ulishawahi kwenda chuo wazazi hali zao ni za kawaida na unategemea boom kwanza kulipia ada ili uweze kufanyia usajili, then boom hilohilo ndio liendeshe maisha yako ya chuo, boom hilohilo utoe kidogo utume kwa wazazi ili maisha yao yasonge, then boom hilohilo usaidie wadogo zako, halafu hela hiyo unayoitegemea kwa hali na mali inacheleweshwa kwa sababu zisizo za msingi? Kama hujawahi kuwa katika hali hiyo huwezi jua kwanini wanafunzi wanagoma boom linapochelewa
Umeongea vyema kabisa tuliopita maisha hayo tunajua vizuri sana wengine hawaelewi hii watakubishia tu, nishawai kula msosi wa bila mafuta geto wala chumvi kwa mwezi mzima afu hapo hapo nikapige shule nipate first class
 
Miongoni mwa nchi zenye watu wanafki yetu inaongoza. Ulishawahi kwenda chuo wazazi hali zao ni za kawaida na unategemea boom kwanza kulipia ada ili uweze kufanyia usajili, then boom hilohilo ndio liendeshe maisha yako ya chuo, boom hilohilo utoe kidogo utume kwa wazazi ili maisha yao yasonge, then boom hilohilo usaidie wadogo zako, halafu hela hiyo unayoitegemea kwa hali na mali inacheleweshwa kwa sababu zisizo za msingi? Kama hujawahi kuwa katika hali hiyo huwezi jua kwanini wanafunzi wanagoma boom linapochelewa

Uongo huu tumeutumia sana ulipokuwa tunasoma, boom tulilitumia kwa ulabu, mademu, kununua simu kali, viwalo bomba, Tv rediao na vitu vingine vingi ambavyo havina uhusiano na masomo. Lakini kila tulipoaka sympathy ya wananchi tulitumia sababu hiyo ei wazazi masikini Tanzania wakati bar zote mikoani zinauza na TBL ndio mlipa kodi mkubwa, hao wau masikini wananunua magari, wanajenga nyumba kali, soko la bidhaa zote za china lakini linapokuja kulipia elimu eti wazazi masikini. Uongo huu ifike muda sasa usitumike tena. Hao wanaoimba hapo wanaonekana masikini hao?
 
Back
Top Bottom