Walimu mmezidi njaa acheni hizo

Walimu mmezidi njaa acheni hizo

Zaidi ya kutoa onyo, mkuu hana access kwenye mshahara wa mualimu wote muaajiri wao ni katibu mkuu, ila anauwezo wakuandika barua kupendekeza uhamishwe shule nyingine.
Mwajiri wa mwalimu sio katibu mkuu ni mkurugenzi mtendaji wa halmashauri. Hujui kitu Kaa kimya, hapa sijasema ana mamlaka ya kwenda ATM Kwa kadi yako kuchota mshahara NO nimesema ana uwezo wa kuenforce Kwa njia yoyote ulipe hilo deni. Madeni madogo madogo ya mitaani kama kukopa sabuni, chumvi, mafuta ya taa, dagaa na sukari yanalipika bila kusubiri mshahara hivyo uwezo wa kulipa hata kwa kuuza kuku au bati za nyumba iliyokushinda kumalizia upo
 
Ili mtu aweze kukopa dukani kwako ni vizuri awe ameshajenga trust isiyopungua miezi sita awe na contribution katika duka lako na unabidi kuwa na mtaji mkubwa au size ya Kati ili kuwawezesha wakopaji kukopa na watu wa cash kununua tofauti na hapo unatafuta lawama na kufunga duka lako
Maisha hayako hiyo.

Unaweza ukawa njema this time - lakini next time ikawa ngumu.
 
Hata sio walimu tu.
Ni hulka yetu watanzania wote,kuna jamaa mshahara wake ni kama 6m hivi,lakini namdai laki mbili tu huu mwezi wa tano sasa na nadhani hana mpango wa kunilipa.
 
Hivi ukija kulala humu ndio utalipwa!? Kwani wewe jinsia Gani!? Kama ni mwanaume!! Dahhh Dunia imekwisha!!
Yani una mdai mtu unatuambia sisi!? Ndio maana wanaume tunadharaulika
 
Kwenye maisha binadamu tunatofautiana sana ndo maana kuna mtu anaweza kuuwa kuroga ata kudhuru mtu kisa deni la elf 2 na mwingne anaweza enda mbali zaidi ad kujiua kisa madeni/ mapenzi

Yan kwel unaanzisha uzi na unatoa lugha za hovyo kisa deni la 45 na inafikia ad hatua unadharau ad taaluma za watu kisa deni la 85 ww si unaweza ata kuuwa ww
Tupunguze kejeri kwenye taaluma za watu
 
Hapa eneo ninapoish nimefungua kiduka cha wastani tu. Kwakuwa mimi ni mtu wa misafara mara kilwa mara Zenji nikirud safari zangu huwa nakagua biashara au madeni.

Sasa cha ajabu kuna walimu wa shule wawili magumu kulipa madeni, pia kuna walimu wa madrasa hawa wa madrasa wakikopa tena hurudisha haraka sana wakati hawana hata mshahara maalum.

Hawa walimu wa shule wanalipwa halafu wagumu kulipa deni kuna mmoja mpaka nimemsamehe nilikuwa namdai 45,000 ila hawa wawili sitaawaacha abadan jumla nawadai 88,000 walidanganya kulipa kwa bili
Ujinga tu mbona hujaja kutushaurisha wakati hujawakopesha?? au lengo unataka tujuwe umeanzisha duka.
 
Mkuu unakosea sana...una takwimu za kuonesha kuwa walimu wamewazidi wengine wote kwa njaa? Mbona ulichokiandika kinaonesha na wewe ni njaa kali?...
Katika maisha yangu kuna kitu niliwahi kujifunza nilipomuona chizi akimcheka chizi mwenzake.
 
Fanya hivi, omba ratiba ya vipindi vya masomo Kwa wanafunzi waulize huyo ticha anafundisha somo gn baada ya hapo check kwenye timetable ni mda upi ana kipindi uende ukamvurumushe darasani kabisa ikiwezekana subiri mda wa assembly ukamfokee na makofi juu
Alihama shule ndio pona yake ila ningemfanyia tukio na anangelipa na ya usumbufu.
 
Mnapenda kutafuta attention za watu kupitia walimu kunamtanzania Gani ambae hakopi?
Mfabyabiashar gani unaenda kuwasema wateja wako mitandaoni au sababu ualimu au unataka usifiwe kuwatja taja walimu
Acheni hizo
Uchache wa akili tu ndo unatuzuzua
 
Tema mate chini. Hujawahi kudai wewe, asikwambie mtu walimu wanakera ahsee
Mwalimu Mpwayugu upooo
JamiiForums-575292719.jpg
 
Back
Top Bottom