Semistocles
JF-Expert Member
- Jul 2, 2016
- 1,932
- 1,126
hakuna mwenye mapepo hapa!Kila amtukanaye mwalimu ana mapepo. Hakuna mwalim kilaza ndio maana alisomea kazi hiyo na akafaulu. Pia hakuna mwalm wa sec ambaye alifeli ndio akaenda kusomea ualimu, kuna walimu wana Division I zao wamesomea ualimu leo mnasema ni vilaza hizo ni kauli za kipumbavu......samahani kwa hili cyo tusi.
Ungeniambia kuna baadhi ya walimu hawana maadili mema pengine ni kutokana na malez walivyolelewa kwenye familia zao na jamii inayowazunguka imewafanya wawe hivyo.
Pili lazima ujaribu kutathmin mfumo wa elimu ya sasa na zamani tulivyosoma sis ni tofauti. Zaman kati ya wanafunzi 50 darasani wanafaulu 3 au 1 lakin sasa hivi darasa lina wanafunzi 100 wote wanafaulu kwenda secondary halafu hajui kusoma hata kunakili notes ubaoni ni hawezi. Unadhani hapo kilaza ni mwalimu au mwanafunzi?
Mnaomtusi mwalimu leo mnajitakia matatizo ambayo kamwe kujiondoa kwayo lazima uingie gharama maana Mungu anawaona.
Mwalimu ndiye amebeba hatima nzuri ya maono ya mtoto. Je wanafunzi wanaofaulu leo na kujiunga form 5 na 6 na kufanya viziri hadi Universities hao wamefundishwa na mashetani?
Mungu anawaona. Ipo siku hawa walimu mnaowatusi leo mtakuja kuwakumbuka, mtawatafuta hamtawaona wakati watoto wenu watakuwa kwenye uhitaji wa walimu kama hawa.
Napinga kabisa kwamba walimu ni vilaza bali walimu wameenda shule, wana div 1au2. Nani atakwenda Chuo kikuu ma div 3?
Chungeni sana vinywa vyenu visije vikasababisha mkose mema ya nchi na mbingu pia.
mchango wenu ni mkubwa lakini lazima mkubali kukosolewa na kubadilika.
kuvunja wanafunzi viuno imekuwa kwenu ni jambo la kawaida tu, eti "tunawafunza maadili".
yapi????