Mzee Msasambegu, kama utakua umenielewa mimi naongelea vyuo vikuu ambavyo hata wewe nina uhakika unavijua. Sasa ukinitajia hivyo Kampala University, St john, IMTU, Hubert Kairuki sijui St Joseph na vingine vya namna hiyo hapo nadhani utakua hujanielewa.
Mimi nimesoma kipindi vyuo vikuu viko 2 tu, University of Dar es salaam na Sokoine University of Agriculture, hata Muhimbili ilikua ni Faculty tu iliyokua chini ya UDSM, hiyo Mzumbe ilikua ni Institute hakikua chuo kikuu, sasa hivi vingine ukiona vinachukua hata wa Division 3 usifikiri hilo liko kwa vyuo vyote. Hata shule za secondary tu huwezi kuniambia mwanafunzi anayeingia kidato cha kwanza shule kama St. Francis au Marian girls/boys atakua na uwezo kama yule wa shule ya Anna Mkapa secondary school au Frederick Sumaye secondary school na shule za aina hiyo.
Mfano kama hicho St Joseph ni juzi tu tumesikia mambo yake ya kufutwa baadhi ya campus zake. Entry point zinazoonyeshwa kwenye makaratasi huwa si kigezo cha kuchukuliwa, kikubwa hapo huwa ni competition iliyopo.
Hayo mambo ya at least two principals na vitu kama hivyo si kwamba watu 20,000 wakipata hivyo vi-principals wote watachuliwa tu. Hivi mtu wa Division 3 anaweza kuchukuliwa Computor Science au Computor Engineering au any Engineering? ukiachana na hizo unazoziita min entry, hizo ni kukuonesha tu kwamba angalau mtu wa points hizo anaweza hata akajaza hiyo kozi lakini si lazima achaguliwe. Mkuu kama kweli umepita katika vyuo vikuu vya uhakika mbona hili lipo wazi kabisa? Usibaki kuangalia hizo entry points.
Mwisho kabisa, hizo "or or or" na "and and and" unazozitumia zinakuonesha level yako na hata hilo jina lako la Mzee nani sijui linakua halina maana tena.