Mkuu wewe unasoma? au ulisoma? Division 3 asome law yaani LLB? Mimi sijasoma hiyo law, masomo yangu ni ya sayansi na nimesoma miaka ya nyuma, lakini competition iliyopo kwenye hiyo LLB hasa kwa vyuo vinavyotambulika kama University of Dar es salaam sidhani. Labda inawezekana maana siku hizi vyuo vimekua kila mahala, vingine hata kwenye magodown ya bia. Tuseme ukweli tu, education entry points zake ni za chini ukilinganisha na kozi zingine.
Kitu nimekiona watu hata pale kwenye ukweli ulio wazi kabisa hawataki kukubali kwa sababu tu mtu yuko upande huo. Kila kitu kimekua ni siasa, mtu akiambiwa chama chake kina mapungufu hata umshikie bastola hawezi kukubali. Hivi kweli mtu anaweza kukataa kwamba ualimu ni kozi inayochukua wenye ufaulu mdogo? Najua utamaduni wa kukipenda chako ni muhimu, lakini pale unaposemwa ukweli watu wakubali. Hivi kuna uele ualimu wa grade III yaani baada ya form 4 mtu anaenda kusoma chuo cha ualimu aje afundishe primary (nasikia wameiondoa hiyo kitu au wanampango wa kuindoa), mtu aliyepata Division one atakwenda kusoma kweli hiyo UALIMU DARAJA LA III?