Walichosema CUF - Nyaraka

Sasa huu ujinga wa CCM wa kuwalaghai watu kwamba mtu hafai kuwa kiongozi kwa sababu tu ana matone ya damu ya warabu itabidi ukome. Natazamia pia wale wajumbe wenzetu hapa JF ambao wamekuwa wakishindilia sana kwamba Salim hafai kuwa Rais wetu kwa kisingizio cha u-Hizbu itabidi wawe wastaarabu watoke hadharani hapahapa watubu, vinginevyo wanyamaze kimya milele katika hili maana inaonekana ama hawajui wanaloliongea au nao ni sehemu ya propaganda za ovyo za CCM!
Mimi nashukuru kwamba wewe mwenyewe sasa umeanza kufahamu mambo. Punguza jazba utazidi kufahamu zaidi. Tokea lini Zanzibar mtu akakosa cheo kwa sababu ya kuwa na damu ya Kiarabu. ,Nani kakueleza hivyo aliyekuwa Bingwa wa histotoria. Hebu angalia utawalam wa hivi sasa. Katika Baraza la Mawaziri la Mheshimiwa Karume. Wamo wenye damu ya Uarabu, Wamo wenye damu ya Uhindi (Ukumbaro), Wamo wenye damu ya Unyamwezi, Wamo wenye damu ya Ushirazi, Wamo wenye damu ya Uhadimu,wamo wenye damu ya Upemba. wamo wenye damu ya Utumbatu- ni mchanganyiko maalum. Ukitaka data zaidi wenyewe wakiruhusu nitakupa na majina. Please jifunze historia. Na acha jazba.
 
Kitila kumbuka JK anaongoza Nchi kwa nguvu za Ukada .Mambo hayo yanatumika China , Burma nk lakini hawachelewi kuchemsha .CUF ni chama makini sana na wote walio kuwa wanabisha wameona .Heko CUF hadi mwisho itajulikana .Wacha tungoje spinning ya CCM sasa .

He. Kwani kuna mashindano ya spinning. If it is spinning it is CUF who is spinning. There is no spinning from the other side.
 
Hivi kweli wewe unafahamu kisa kile? Wafuate wakueleze. Au unataka tukueleze humu waliowaulisha watu wale. Ni kweli hawana hatia. Lakini unaifahamu hiyo, kadhia wewe?

Of all pple wewe si wa kutoa maelezo hapa... labda urudi ukamalizie shule yako pale Kivukoni ili upate cheti cha ukadhia kwanza......
 
Hivi who is Kibabu Kingunge Ngombare ??? Why Kingunge? nachofahamu babu yangu ambaye ni mdogo yake na kingunge kwa sana anaanza kuwa kama mtoto hata kumbukumbu zinapotea... sasa tunawezaje kuamni kuwa kingunge bado anazo kumbukumbu za kutosha??? Hivi akilala huko nyumbani kwake akapumzika kuna shida gani? Akae atulie aache kizazi cha dot com kifanye kazi zake. Kingungeee Kingungeee Let him rest in peace
 
Of all pple wewe si wa kutoa maelezo hapa... labda urudi ukamalizie shule yako pale Kivukoni ili upate cheti cha ukadhia kwanza......
Leo MWK umekutana na kisiki, kama kawaida yako unakimbilia kusema mambo ya Kivukoni... Nina wasiwasi kuwa hata wewe ulipita pale..
 
Du nimesoma habari yote... nimesikitishwa kwa sababu heri mungekuwa mumesikia wenyewe... CCM waliyosema na CUF pia waliyosema...

Na kusitikitisha ni kwamba CUF walikiri kukiuka makubaliano ya kuongelea mambo ya muafaka hadharani bila kuwepo makatibu wakuu wote... lakini haikuandikwa... sasa rafiki yangu kama mwanakijiji ndio amepigwa bao hivyoo.... kwa sabubu haikuandikwa...

CUF wamesema walishakubaliana ... quote walizotoa za kuonyesha kukubalina kwa hakika ni dhaifu sana... tena kupita. kiasi...

CCM ofcourse ina mapungufu yake... lakini du CUF...

Nimeona quote ya Maalim Seif ya Kulazimishia Uwaziri Kiongozi... narudia usemi wangu Kwamba Maalim Seif ni hatari sana kwa utulivu wa Zanzibar... rudini tena muone ile quote.
 
Nimeona quote ya Maalim Seif ya Kulazimishia Uwaziri Kiongozi... narudia usemi wangu Kwamba Maalim Seif ni hatari sana kwa utulivu wa Zanzibar... rudini tena muone ile quote.
Ah huyo mtu yuko tayari hata kwa gharama za kuwauza wazee wake wa Mtambwe, lakini apate Kin'gora naye- adekshie mitaani.
 
Du nimesoma habari yote... nimesikitishwa kwa sababu heri mungekuwa mumesikia wenyewe... CCM waliyosema na CUF pia waliyosema...

Na kusitikitisha ni kwamba CUF walikiri kukiuka makubaliano ya kuongelea mambo ya muafaka hadharani bila kuwepo makatibu wakuu wote... lakini haikuandikwa... sasa rafiki yangu kama mwanakijiji ndio amepigwa bao hivyoo.... kwa sabubu haikuandikwa...

CUF wamesema walishakubaliana ... quote walizotoa za kuonyesha kukubalina kwa hakika ni dhaifu sana... tena kupita. kiasi...

CCM ofcourse ina mapungufu yake... lakini du CUF...

Nimeona quote ya Maalim Seif ya Kulazimishia Uwaziri Kiongozi... narudia usemi wangu Kwamba Maalim Seif ni hatari sana kwa utulivu wa Zanzibar... rudini tena muone ile quote.

Kasheshe, nilisikiliza taarifa ya habari ya saa mbili jana usiku na nikasikia walivyosema kuwa "CUF wamekiri kukiuka makubaliano". Lakini kukiri kukiuka makubaliano si sawa na kukiri kufanya makosa kuwaambia watu kinachoendelea hasa yale makubaliano yanapotumika kunufaisha upande mmoja.
 
Kasheshe, nilisikiliza taarifa ya habari ya saa mbili jana usiku na nikasikia walivyosema kuwa "CUF wamekiri kukiuka makubaliano". Lakini kukiri kukiuka makubaliano si sawa na kukiri kufanya makosa kuwaambia watu kinachoendelea hasa yale makubaliano yanapotumika kunufaisha upande mmoja.

Hii ilikuwa ni muhimu kujibiwa na kuonekana kwenye ripoti kama walikuwa wanataka tuwajue kwamba wao hawa-spin.

Ikumbukwe hii ilikuwa ndio chanzo cha malumbano tuliyonayo leo....

CUF ni waongo tu! na Wagomvi wakubwa... hilo liko wazi...
 
Du nimesoma habari yote... nimesikitishwa kwa sababu heri mungekuwa mumesikia wenyewe... CCM waliyosema na CUF pia waliyosema...

Na kusitikitisha ni kwamba CUF walikiri kukiuka makubaliano ya kuongelea mambo ya muafaka hadharani bila kuwepo makatibu wakuu wote... lakini haikuandikwa... sasa rafiki yangu kama mwanakijiji ndio amepigwa bao hivyoo.... kwa sabubu haikuandikwa...

CUF wamesema walishakubaliana ... quote walizotoa za kuonyesha kukubalina kwa hakika ni dhaifu sana... tena kupita. kiasi...

CCM ofcourse ina mapungufu yake... lakini du CUF...

Nimeona quote ya Maalim Seif ya Kulazimishia Uwaziri Kiongozi... narudia usemi wangu Kwamba Maalim Seif ni hatari sana kwa utulivu wa Zanzibar... rudini tena muone ile quote.


Hivi huko CCM hakuna watu wenye uwezo wa kuchambua hoja kwa umakini kama walivyofanya CUF? Hivi hawawezi hata kuweka mawazo yao kwenye maandishi? Kasheshe kwa nini usiwasaidia hata uka-post hapa ile paper ya Kingunge ili nayo tuichambue? Au alikuwa anaongeaongea kila lililokuja kichwani mwake kama kasuku?
 
Kwa kweli Tanzania tunaipeleka pabaya kwa sababu ya kuendekeza uchama, CUF au CCM. Hakuna nchi katika Africa itmepata maendeleo kwa kuendelea na itikadi za chama kilichopigania uhuru. CCM siyo wakweli. Umeongea ajenda nne, bado moja kwani zile nne si zimeisha? kwa nini wanachama waliokupa 'mandate' ya kunegotiate wasiambiwe? hilo ni kosa kwa nini? kwani makubaliano ni ya watu wawili au ni kwa manufaa ya wote hasa wanachama? lazima tukubali kuwa siasa inafanywa na wawakilishi na ndiyo maana nchi inatumia fedha nyingi katika uchaguzi ili wawakilisha kadhaa waongee kwa niaba ya wapiga kura wao. ninapata shida sana kuelewa itikadi za ubabe zinazotumiwa na CCM (Chukua Chako Mapema au ni Chakula Chako Mfukoni?). Unakamata watu na kuwafungulia mashitaka ya uhaini kwa sababu wamefika UN offices kutoa masikitiko yao kuhusu wanavyoonewa? Hata kama walifanya makosa, uhuru wa mawazo uko wapi nchi hii? Haki za Binadamu ziko wapi? If anything bad is gonna happen to our mother land is due to the irresponsible characters of our so called CCM elite! Tujaribu kuangalia ukweli na tusifumbwe macho na maneno ya kejeli na yasiyo na mantiki yanayotolewa na wazee kama Makamba na Kingunge au Shamhuna. Warioba alikuwa kiongozi mkuu wa nchi, anaona mbali. Akisema wanamwona kichaa! God bless my motherland.
 
Source: Habari Leo
Shadrack Sagati
Daily News; Thursday,May 15, 2008 @00:01

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba
amesema kitendo cha Chama cha Wananchi (CUF) kutaka kuingizwa katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni sawa na uhaini. Akizungumza na gazeti hili jana, Makamba alisema suala la kuundwa kwa serikali ya kitaifa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2010 lilitolewa kama pendekezo na CUF, lakini yeye alilikataa.



Alisema suala la kuundwa kwa serikali ya kitaifa kamwe halikuwahi kujadiliwa kwenye vikao vyao. "Sisi tuliona hilo suala halituhusu bali linahusu dola, ndiyo maana tukalikataa kulijadili kwa kina," alisema.

Hata hivyo, wakati wa vikao hivyo kutojadili suala hilo kumbukumbu za kikao cha kamati hizo cha Januari 21, 2008 kilichofanyika saa 2.30 usiku, Kingunge Ngombale-Mwiru aliyekuwa mwenyekiti mwenza wa CCM alitoa taarifa ya mjadala wa suala hilo.

Kwa mujibu wa kabrasha la muhtasari wa vikao hivyo, Kingunge alianza kwa kusema "wameelewana kuwa pande zote mbili zinataka ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko wa siasa Zanzibar na kwamba unahitajika mustakabali mpya wa siasa ambao utatokana na uchaguzi ulio huru na wa haki mwaka 2010.
"Hata hivyo katika kipindi hiki cha kuelekea 2010 kuwe na njia ya kujengeana imani ambazo katika hatua za siasa zitajumuisha na Rais wa Zanzibar aliyepo madarakani kuteua mawaziri kadhaa kutoka CUF waingie serikalini.

"Lakini kwa kuwa hili la Rais kuteua mawaziri kutoka CUF ni la dola na si la vyama, basi CUF watatayarisha mapendekezo yao na kisha watayawasilisha kwa CCM yaweze kufikishwa kwa viongozi wa juu."

Jana Makamba akizungumza na gazeti hili alisisitiza kuwa suala hilo halikujadiliwa na hawakufanya hivyo kwa vile Zanzibar kuna Rais halali ambaye alishinda uchaguzi uliopita, hivyo asingeweza kujadili kuundwa kwa serikali ya kitaifa kabla ya 2010.

Lakini kwenye muhtasari wa vikao hivyo, wakati wa mjadala wa suala hilo baadhi ya wajumbe walitaka ufafanuzi kuhusu suala hilo la baadhi ya mawaziri kutoka CUF kama ni ombi, makubaliano, au ni mapendekezo ya CUF.

Ndipo Makamba aliyekuwa mwenyekiti wa kikao alitoa ufafanuzi kwa kusema, "CUF itawasilisha mapendekezo yake rasmi kwa maandishi kwa Katibu Mkuu wa CCM ili naye ayawasilishe kunakohusika."

Jana katibu mkuu huyo wa CCM alisema alilikataa suala hilo la CUF kwa vile chama hicho kilitaka kuingia serikalini kwa kupitia mlango wa nyuma, jambo ambalo alidai haliwezi kamwe kutokea.

"Mimi nilikataa kwa sababu kuundwa serikali ya kitaifa ni pale tu ambako kuna mgogoro wa siasa, lakini Zanzibar hakuna kitu kama hicho, kujadili suala kama hili wakati kuna serikali ambayo iko madarakani kwa halali ni sawa na uhaini," alisema Makamba.

Pia katika kumbukumbu za vikao vya mazungumzo vinaonyesha kuwa suala la kuundwa kwa serikali ya kitaifa kabla ya uchaguzi wa 2010 lilianza kujadiliwa katika kikao Mei 3 hadi 9, mwaka huu.

Suala hilo lilikuwa katika ajenda ya pili ambayo ilikuwa inasema njia ya kuimarisha mazingira ya uelewano wa siasa na uendeshaji wa uchaguzi huru na haki Zanzibar.

Katika nyaraka za vikao hivyo inaonyesha kuwa CUF ilitoa masharti ya kumtambua Rais Amani Karume; lakini liambatane na dhamira ya dhati ya CCM kuihakikishia CUF kwamba kiongozi huyo naye atawatangaza wawakilishi wa CUF kuingia kwenye serikali ya kitaifa.

Pia chama hicho kilisema kitamtambua tu Rais Karume kama kitahakikishiwa kuwa lengo la mazungumzo hayo ni kuunda serikali ya pamoja mara tu baada ya mazungumzo kukamilika na makubaliano kutiwa saini.

CCM ilipokea pendekezo hilo la CUF na kuomba muda wa kulitafakari. Kesho yake ujumbe wa CCM kupitia kwa katibu wake Vuai Ali Vuai ulisema suala la uteuzi wa wawakilishi waliopendekezwa na CUF linazungumzika na ujumbe wa CCM utalifanyia kazi.

Hata hivyo, wajumbe wa CCM walisema tangazo la kumtambua Rais Karume aliyechaguliwa katika uchaguzi wa 2005 haliwezi kutumika kumlazimisha Rais aunde serikali ya pamoja kabla ya mwaka 2010.

Juzi CUF iliweka hadharani nyaraka mbalimbali kuonyesha makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo hayo na namna walivyoandaa rasimu ya majadiliano hayo ambayo yalikuwa yatiwe saini na makatibu wakuu.
 
Hivi huko CCM hakuna watu wenye uwezo wa kuchambua hoja kwa umakini kama walivyofanya CUF? Hivi hawawezi hata kuweka mawazo yao kwenye maandishi? Kasheshe kwa nini usiwasaidia hata uka-post hapa ile paper ya Kingunge ili nayo tuichambue? Au alikuwa anaongeaongea kila lililokuja kichwani mwake kama kasuku?

Mkuu Kitila Mkumbo;

Kwi kwi kwi; unataka mzee Kingunge atumie computer... kwi kwi kwi... ila kwangu mimi ile ni mashine kubwa mkuu imejaa hekima sana... watu tu hawaangalia kwa undani.

By the way mimi nimeona wote wanatuchezea ;

Ukiniuliza natamani chama chetu kitukufu makini (CHADEMA) ndio sasa kilitakiwa kiingilie na kusema ukweli usio lalie upande wowote... hii ni nafasi nzuri sana ya chama chetu hiki makini, cha wasomi, chenye watu wanaochambua mambo kwa makini, chenye uzalendo wa hali ya juu kuliko vyote; chenye nia njema kuliko vyama vyote; kisichokuwa na mafisadi hata chembe, chenye kuweka masilahi ya Taifa mbele... kiingilie kama thirdy part kumalizia kazi ambayo kwa asilimia nyingi iko karibu sana kuisha...

Maoni tu!
 
Sioni jipya kwa wanachodai CCM. Kwamba Rais wa Zanziba alishinda kihalali is open to discussion. Kama Zanziba inaundwa na visiwa viwili vya unguja na pemba na Rais hana mbunge hata mmoja toka Pemba, nadhani ni vigumu kukubaliana na assessment hiyo!
 
Sioni jipya kwa wanachodai CCM. Kwamba Rais wa Zanziba alishinda kihalali is open to discussion. Kama Zanziba inaundwa na visiwa viwili vya unguja na pemba na Rais hana mbunge hata mmoja toka Pemba, nadhani ni vigumu kukubaliana na assessment hiyo!

Ah Jobo nawe. Kwani anayechagua Rais ni Wabunge (Wawakilishi) au ni wananchi katika ujumla wao.
 
Mkuu Kitila Mkumbo;

Kwi kwi kwi; unataka mzee Kingunge atumie computer... kwi kwi kwi... ila kwangu mimi ile ni mashine kubwa mkuu imejaa hekima sana... watu tu hawaangalia kwa undani.

By the way mimi nimeona wote wanatuchezea ;

Ukiniuliza natamani chama chetu kitukufu makini (CHADEMA) ndio sasa kilitakiwa kiingilie na kusema ukweli usio lalie upande wowote... hii ni nafasi nzuri sana ya chama chetu hiki makini, cha wasomi, chenye watu wanaochambua mambo kwa makini, chenye uzalendo wa hali ya juu kuliko vyote; chenye nia njema kuliko vyama vyote; kisichokuwa na mafisadi hata chembe, chenye kuweka masilahi ya Taifa mbele... kiingilie kama thirdy part kumalizia kazi ambayo kwa asilimia nyingi iko karibu sana kuisha...

Maoni tu!


kasheshe...
mtu mwenye hakima hawezi kuyapinga hadharani yale aliyoyasema muheshimiwa warioba. so mi nakuomba tena umchunguze huyu mzee kisha urudie kauli yako.
 
Huyu mzee angekuwa na busara asingesema uongo mbele ya waandishi wa habari wakati anajua kuwa kuna document za kudhibitisha kuwa amesema uongo, ana busara hata kidogo angekuwa na busara CCM isingekwenda mrama na yeye anaangalia tu.
 
Back
Top Bottom