Wale wa miaka ileeee!!

Wale wa miaka ileeee!!

Nyamaza wewe, miaka ya tisini juzi sana mbona?
shikamoo babu! nami ni mzee kwa wengi wa sasa. sitadanganya ya miaka ya 70 hali nilikuwa ndani ya kokwa za mzee wangu! hahahaa. kila zama na kitabu chake. kuna ambao hata radio za Phillips hawakuziona mkuu
 
Idadi ya kupima hazihesabiki.....lakini sikumbuki kama nilishawahi kuchukua majibu....achilia mbali kuyasubiria.....

Mzee mwenzagu wasambaa wanasema....

KAMA NI MBWAI,MBWAI....
Kwakweli acha iwe mbwai tu kuliko kufa kwa presha ya kujitafutia
 
Aah hio redio imenikumbusha tangazo la sabuni ya mshindi.
 
Betrii zikiisha inapiga miluzi balaa. Ukiifungua kama hukumbuki step utakuta vitu vimejaa na bado spika hujairudishia. Hahaha
Ahahaahaahhahhahha we jamaa kata kimoja hapo mkuu
46fd774599a7147449e4b7dff21bb769.jpg
 
betri zilikuwa national au abc zikiisha mnazigongagonga na kuziweka juani eti zinajichaj
 
Dah!Sitasahau hadithi ya Bint chura kila jumamosi saa nane mchana,natamani wairudie niiaikie tena ilikuwa kama sio 1991 basi 1992 RTD kipindi cha mama na mwana mtangazaji nimemsahau
 
Michezo ya radio nilikuwa sikosi hasa Pwagu na Pwaguzi, aaaah wapi Ben Kiko???
 
Wakati huo ugonjwa mkubwa ulikuwa kaswende tiba tetracycline
Kombora na ombi lako kama sio usikumwema palipigwa ngoma sio mchezo vipindi kama mkoa kwa mkoa malima nderema au nadhir mayoka sio mchezo kipindi hicho ndio niliusikia wimbo wa kila munu ave na kwao wakati sijui umekwenda wapi?
 
Wakati wa kazi ujuzi iliupata humu humu kazini, J.pili salamu kwa wagonjwa, ajuaye bwana mgonjwa kuwa salama mzima kuwa mfu, zilipendwa, Nyaisanga na mwenzie wa makabila yetu wote wame RIP. Dada Sara Dumba, External service tunasikiliza wapigania uhuru wakitoa sera zao.ANC PAC, Frelimo na wengine hasa juma pili mchana tukiwa likizo nilikuwa nashinda kwenye redio nasikiliza sera.

Tunatoka huko tunakuja kuletewa eti vyombo vya habari kumsikiliza mkuu wa mkoa??? wapi na wapi. Deko
 
Back
Top Bottom