Wakuu wa wilaya waliotemwa...

Mrembo wa Upanga aliyekuwa Lushoto katemwa? Naona Lushoto kuna DC mwingine kabisa..........
Unnamaana nani Sophie Mjema? si naona yupo Temeke sasa...

Naona Hafsa Mtasiwa kateuliwa Pangani, huyu dada si ndio mke wa Dr Mtasiwa aliekuwa mganga mkuu au majina yanafanana? maskini toka oyster bay hadi Pangani kweli kama mtu una dili zako za maana mjini uDC piga chini tu labda kama una political ambition
 
Si jambo la busara kufurahia masahibu yaliyompata binadamu mwanziyo kuna siku yatakufika na wewe jambo lamsingi nikuombeana heri,pili hizi nikazi za watu kuna wakati ukifika ni lazima utawapisha wengine,tatu kuna suala la kufikia umri wa kustaafu sasa cha ajabu ni nini? au mtu mzima unashangilia matukio ya kawaida yote haya ni kukosa busara,cha msingi ni kuwatakia kila la kheri kwa maisha mapya Mungu Ibariki Tanzania.
Bahati Akili -Ilala dsm.


Hapo kwa Nyarubanja si ungeandika tu Bahati Akili
 
Alianzia Chunya,bdae akapelekwa Karagwe, Tarime na Kiteto! Kada wa ukweli ambaye huwa najiuliza kwanini hajawahi bahatika kuteuliwa ktk Sekretarieti ya CCM Taifa. Badala yake wanakuwemo watu kama Nape,Makamba na Mwigulu!

timbilimu si nasikia Mkuu anataka kuichangua secretariat ya chama huenda jamaa akakumbukwa. Siamini kama huo ndio mwisho wake. Na kina huyu aliyekuwa Mbeya Mjini naye siamini kama ndio ametoswa moja kwa moja.
timbilimu Frank nilionana naye kule Kayanga....ni kijana mwenye damu kali sana ya CCM, kama ulivyosema, kwa kweli inashngaza kada mkuu kama yeye aachwe........pengine ule mvutano kati yake na Waziri Nchimbi bado unachangia....
Kimbunga Mkuu heshima mbele...........Evance Ballama alishafikisha wakati wa kustaafu......kama ulivyosema kwa sababu ya utendaji wake......pengine magamba watampa nafasi nyingine ya kimkataba......
 
Charles Mlingwa toka Unaibu Waziri hadi ukuu wa wilaya.

Duh naona wamemsahau Dr. Luka Siame

Yaani hovyo kabisa si afadhali aendelee tu kufundisha na kufanya tafiti zake hapo Zoology UDSM? Nafikiri ni kazi nzuri zaidi kuliko kwenda kuhangaishana na DED huko wilayani.
 
mgeni wenu anaitwa capt. Ngatuni siyo Katuni. Jamaa ametulia sana yule hana papara na ana busara.
Kimbunga,
Geofrey Ngatuni hajatulia hata kidogo wala hana busara, na bahati mbaya sana huyu jamaa ana papara mno. Kama humfahamu vizuri uliza watu wa Musoma alipokuwa mkuu wa wilaya kabla ya kupigwa chini. Ni mtu wa hovyo sana huyu.
Nitakukumbusha kisa kimoja cha hivi karibuni, ITV waliripoti kiuwepo kwa njaa kali sana katika kata moja ya wilaya ya Musoma na kuonyesha picha za wananchi wakichemsha majani ya porini pamoja na mboga mboga ili kukidhi mahitaji yao ya chakula. Mtendaji wa Kata pamoja na diwani wakahojiwa na kuthibitisha kwamba kweli wananchi wa kata ile walikuwa wanakabiliwa na njaa hivyo kuhitaji msaada wa haraka.

Sasa maajabu yalikuja kujitokeza pale mkuu wa wilaya Geofrey Ngatuni alipokanusha kwamba hakuna njaa wilayani musoma bali vyombo vya habari vilikuwa vinalikuza tu jambo hilo. Ingawa baadae watu walivyoendelea kupiga kelele, vyombo vya habari kulishikia bango suala hilo na baraza la madiwani kutoa tamko la kumtaka mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Musoma awajibike kwa kushindwa kusimamia zoezi la upatikanaji na usambazaji wa chakula toka ghala la taifa shinyanga, ndipo tukamuona Ngatuni na mkurugenzi wake wakienda kuwatembelea waathirika wa njaa na kuagiza chakula cha msaada kiwafikie.

Sasa ukisema kwamba Ngatuni ana sifa hizo ulizokuwa umezitaja, nitakukatalia katakata, kama angekuwa ametulia, hana papara na ana busara, mara tu baada ya kupata taarifa za itv angechukua jukumu la kutafuta taarifa sahihi toka eneo husika kabla ya kukimbilia kukanusha, kitua ambacho alikuwa hana taarifa nacho.
 
Last edited by a moderator:
Mlingwa ameshuka mno toka awe DG TAWIRI,ubunge,unaibu waziri hadi DC kweli mpanda ngazi hushuka
 
Alianzia Chunya,bdae akapelekwa Karagwe, Tarime na Kiteto! Kada wa ukweli ambaye huwa najiuliza kwanini hajawahi bahatika kuteuliwa ktk Sekretarieti ya CCM Taifa. Badala yake wanakuwemo watu kama Nape,Makamba na Mwigulu!

Frank Uhahula akiwa katibu mkuu wa uvccm aliwahi kuwa na ugomvi mkubwa sana na Emmanuel Nchimbi akiwa mwenyekiti wa uvccm hadi mzee mkapa akaamua kuwatenganisha kwa kumteua Uhahula kuwa mkuu wa wilaya ya Chunya huku akimteua Nchimbi kuwa mkuu wa wilaya ya Bunda.

Alipokuwa Tarime alitaka kuleta jeuri yake ya uvccm, akakumbana na nguvu ya marehemu Chacha Wangwe na kisha baadae John Heche akiwa diwani Tarime mjini. Aliwahi kupigwa ngumi kwenye kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Tarime na diwani mmoja wa Chadema baada ya kumsemea lugha mbofu mbofu!! Baada ya hapo alikuwa akipita mitaani anazomewa na wananchi na baadae hali ilikuwa ngumu hadi gari yake kupondwa mawe na wananchi. Ndipo aliomba uhamisho kutoka Tarime na kuhamishiwa wilayani Kiteto.

Kuachwa kwake katika nafasi hii ya udc inaweza kuwa imechangiwa na bifu lake na nchimbi kwani nchimbi yuko karibu sana na kikwete. Hata hivyo kwa kuwa sometimes mkuu wa kaya hatabiriki anaweza kumpa chaka jengine.
 
Walioachwa
Uchambuzi zaidi umebaini kuwa miongoni mwa walioachwa na wilaya zao kwenye mabano ni pamoja na Evans Balama (Mbeya), Zainab Kukwega (Makete), Samwel Kamote (Bukoba), Salum Nyakonji (Ngara) na Othman Mdoe (Mwanga).

Wengine walio...achwa ni Musa Samizi (Moshi), Hawa Mchopa (Ruangwa),Dk Ian Lengibori (Babati), Winfrid Ligubi (Hanang), Frank Uhaula (Kiteto), Geofrey Ngatuni (Musoma Mjini), Esther Wakali (Ileje), Gabriel Kimoro (Mbozi) na Kanali John Mzurikwao (Sumbwanga).

Wengine walioachwa ni Joyce Mgana (Nkansi), Philimon Shelutete (Geita), Zainabu Kondo (Magu), Henry Clemence (Mkuranga), Thomas Ole Sabaya (Songea), Kanali Edmund Mjengwa (Mbinga), Bahati Matala (Kahama) na Grace Mesaki (Iramba).

Pia wamo Florence Horombe (Nzega), Stanley Kolimba (Uyui), Kapteni Seif Mpembenwe (Handeni) na Rashid Ndaile (Mkinga).
 
Kuna mmoja aliwacharaza ndugu zake kwenye ugomvi wa kugombea nyumba ya urithi, kama sijasahau ni kutoka wilaya za mkoa wa Mara

Bado yupo?
 
Frank Uhaula alikuwa safi, namfahamu alichobugi step ni kukaa wilayani muda mrefu sana, walitupwa kwenye ukuu wa wilaya kupunguza mvutano wa kisiasa na m.kiti wake Nchimbi, yeye akaenda Chunya, Nchimbi ( Bunda). Nchimbi akatoka kule na akagombea ubunge hadi alipo sasa. Nadhani alikuwa kwenye kambi pinzani ambayo haikupata madaraka. Ndiyo siasa ilivyo ukijunga na kambi inayoanguka na wewe unaanguka , wako wengi.

Ushauri, Frank Uhaula - jipange na upinzani CDM , unaweza pata jimbo na huo utakuwa ni mwanzo wa kurudi kwenye limelight.

Ni mzuri nilisoma naye namfahamu, aaah Uha Uha Uha .... waliokuwepo mahala watafahamu.
 
Alianzia Chunya,bdae akapelekwa Karagwe, Tarime na Kiteto! Kada wa ukweli ambaye huwa najiuliza kwanini hajawahi bahatika kuteuliwa ktk Sekretarieti ya CCM Taifa. Badala yake wanakuwemo watu kama Nape,Makamba na Mwigulu!
Yes, ni kada wa ukweli lakini shida yake hajiheshimu. Analewa ovyo halafu anaanza ku-deal na VCD! hana sifa za uongozi.
 
timbilimu Frank nilionana naye kule Kayanga....ni kijana mwenye damu kali sana ya CCM, kama ulivyosema, kwa kweli inashngaza kada mkuu kama yeye aachwe........pengine ule mvutano kati yake na Waziri Nchimbi bado unachangia....
Kimbunga Mkuu heshima mbele...........Evance Ballama alishafikisha wakati wa kustaafu......kama ulivyosema kwa sababu ya utendaji wake......pengine magamba watampa nafasi nyingine ya kimkataba......
Ogah umenikumbusha ile bifu kati ya Comrade Nchimbi na Frank.
 
Last edited by a moderator:
Frank Uhahula akiwa katibu mkuu wa uvccm aliwahi kuwa na ugomvi mkubwa sana na Emmanuel Nchimbi akiwa mwenyekiti wa uvccm hadi mzee mkapa akaamua kuwatenganisha kwa kumteua Uhahula kuwa mkuu wa wilaya ya Chunya huku akimteua Nchimbi kuwa mkuu wa wilaya ya Bunda.

Alipokuwa Tarime alitaka kuleta jeuri yake ya uvccm, akakumbana na nguvu ya marehemu Chacha Wangwe na kisha baadae John Heche akiwa diwani Tarime mjini. Aliwahi kupigwa ngumi kwenye kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Tarime na diwani mmoja wa Chadema baada ya kumsemea lugha mbofu mbofu!! Baada ya hapo alikuwa akipita mitaani anazomewa na wananchi na baadae hali ilikuwa ngumu hadi gari yake kupondwa mawe na wananchi. Ndipo aliomba uhamisho kutoka Tarime na kuhamishiwa wilayani Kiteto.

Kuachwa kwake katika nafasi hii ya udc inaweza kuwa imechangiwa na bifu lake na nchimbi kwani nchimbi yuko karibu sana na kikwete. Hata hivyo kwa kuwa sometimes mkuu wa kaya hatabiriki anaweza kumpa chaka jengine.
Mwita Maranya hiyo ya Tarime ni kawaida sana manake kule ngumi mbele na mapanga mkononi! Hata mabiti nadhani yalimkuta mambo fulani hivi.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom