kwenye blue hapo!! hao baadhi ni wabunge na walio kua wabunge...hivi kuna haja gani ya kurecycle??????
Wana recycle kwa kuwa "mwenzao" anakuwa ameangukia pua na hivyo wanatafuta namna ya kumpoza ili aweze kusonga mbele na maisha.
Kumteua mbunge kuwa Mkuu wa Mkoa/Wilaya, huu ni ubadhirifu. Moja, ataendelea kulipwa posho zote za Mbunge na haswa mafuta, wakati tukijua wazi kwamba anatumia gari la Mkuu wa Mkoa/Wilaya.
Kwa wastani, wabunge wanakuwa ama Dodoma au Dar kwa shughuli za Bunge kwa miezi 6 kwa mwaka [Bunge la Bajeti miezi 3, Vikao vingine 3 vya wiki mbili mbili sawa na mwezi na nusu, ukijumlisha na vikao vya Kamati za Bunge tayari unapata miezi karibu 6].
Kwa kipindi chote hicho, Mkuu wa Mkoa/Wilaya anatumia gari na dereva wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa/Wilaya. Matokeo yake ni kwamba mtu mmoja anajikuta analipwa mara mbili. Kama Rais angeteua mwingine ambaye si mbunge, angeweza kubaki kwenye kituo chake cha kazi kwa miezi 10 na kuwa nje ya kituo kwa miezi labda miwili tu ambapo hela ya mafuta, matengezo ya gari la mkuu wa mkoa na posho za dereva zingeweza kusalimika.
Tumeona mawaziri kibao wanajivinjari na mashangingi ya serikali na madereva wao wakiwa majimboni kwao wakifanya shughuli za kubunge, kitu ambacho ni makosa maana tayari huyo waziri analipwa na Bunge kufanya hizo shughuli za kibunge lakini bado serikali pia inalipia gharama za waziri kwenda jimboni kwake na wapo ambao kila weekend yuko jimboni kwake na hawezi kuulizwa maana ni sehemu ya majukumu yake kama mbunge.
Hapa ndipo kuna umuhimu wa wabunge kutokuwa sehemu ya serikali. Kuna mgongano mkubwa sana mbunge anapoteuliwa kuwa waziri au mkuu wa wilaya/mkoa, kwa kuwa inamnyima fursa ya kuwa huru kuwatumikia wananchi na pia inaongeza gharama kwa mlipa kodi na ni ubadhirifu wa mali ya umma.