Wakuu nimeitwa TRA. Usalama upo kweli?

Wakuu nimeitwa TRA. Usalama upo kweli?

Nimepigiwa simu TRA wananiita. Namba ya simu ni ya kawaida. Je uzima upo? Sehemu niliyo itwa ni tofauti na kituo changu cha Kodi..

Usalama upo kweli?

N. B : Mimi sio mfanyabiashara mkubwa wala wa Kati.

Usiogope. Nenda kama ulivyo. Mto wanaume huvuka tukifika darajani. Nenda kifua mbele wewe mlipa kodi, ndiyo bosi wao.
 
Nafsi yako na upeo wako wa kiakili vinakuambiaje kulingana na mazingira yenyewe ya kuitwa kwako?

Hata kama ni tofauti na kituo chako, hakikisha sio sehemu nyingine tofauti na ofsi iliyo maeneo ya wazi inayohusika na mambo ya kodi TRA, na uzingatie sana masaa yako ya kwenda. Kama utakuwa na wasiwasi, wakati unatoka piga routes za nyoka kabla hujashika route ya kurudi unapokaa.

Vinginevyo kaa usubiri barua rasmi.
 
Back
Top Bottom