Wakuu jaribuni basi ku balance mzani

Wakuu jaribuni basi ku balance mzani

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,508
Reaction score
830,009
Siasa za Bongo sasa zimebebwa na chama kimoja tuu
Mijadala ya kisiasa kwasasa imetawaliwa na chama kimoja tuu
Matukio ya kisiasa Bongo yote kwasasa yote ni ya chama kimoja tuu
Mitandao ya kijamii bongo habari zake za kisiasa zote zimeelemea chama kimoja tuu
Hii sio sawa kabisa.. Hakuna mizania ya haki hapa.. No kama vile vyama vingine ni mahututi ama ni mfu kabisa

Je asili inachukua mkondo wake? Does nature taking its cause!?💪🏿✌🏿
Tulipofika ni A point of no return.. Na hakuna nguvu inayotumika bali mambo yanaenda yenyewe.. Very natural.. Very automatically..!

Ni afadhali kidogo huko kwende kandanda.. Japo Mnyama nyota yake inang'ara zaidi lakini walau mtani jembe anasikika kidogo.. Mtani ni majeruhi lakini si mahututi..
Maneno ya Mungu yanasema hivi

Mathayo 5:13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu
Kuna chama tayari kimeshakuwa chumvi iliyoharibika.. Isiyofaa tena.. Imeshatupwa na inakanyagwa na watu..

Nani anaweza kunionesha walau mada moja mitandaoni iliyotawala walau kwa masaa machache ama iliyoenda viral? Achana na zile mada mbovu zilizokosa ladha na uhalisia za mbubujikwa machozi, tlaa tlaah, yule Yohana mbatizaji kinyonga na wengine

Ni wakati wa mabadiliko na hakuna nguvu ya kibinadamu kuizuia. Kama Mnyama anavyoenda fainali na kuchukua kikombe ndivyo hivyo navyo CHADEMA inavyoenda kuchukua nchi
Simba ilitinga fainali mwaka 1993 wakati mageuzi yanaasisiwa.. Simba inaenda kuchukua ubingwa mwaka huu wakati mageuzi yakiwa kwenye kilele cha ubora na kukubalika

Kuna coincidence ya ajabu hapa na iko kiroho zaidi! Upande wa RED unang'ara na kukubalika kila kona! Lakini upande ule mwingine kumefubaa kumefifia hakuna nuru .. Na kuna kila dalili ya matanga!
Sijui mnanielewa?
Good morning TANGANYIKA,💗
 
Je asili inachukua mkondo wake? Does nature taking its cause!?💪🏿✌🏿
Tulipofika ni A point of no return.. Na hakuna nguvu inayotumika bali mambo yanaenda yenyewe.. Very natural.. Very automatically..!

Ni wakati wa mabadiliko na hakuna nguvu ya kibinadamu kuizuia. ndivyo hivyo navyo CHADEMA inavyoenda kuchukua nchi

Sijui mnanielewa?
Good morning TANGANYIKA,💗
Mkuu Mshana Jr ,tumekuelewa
ila kwa sisi wa longi tunajua all the games people play,1995 ilikuwa hivi kwa NCCR Mageuzi na Lyatonga,2015 was the same kwa Chadema na moto wa Lowassa.

The game ya siasa zetu haichezwi kwenye zile dakika 90 uwanjani,the game inachezwa mezani!。

Huyu Maza kaingia na nia njema ya dhati,kaitisha timu zote zikae mezani,tujadili kwa pamoja the rules of the game,watu mkakataa!,akina sisi watazamaji wazuri wa huu mchezo,tukawashauri Chadema, P'se, Msisusie Mkutano wa Vyama, Wasilisheni Hoja Zenu Mezani, Zitamfikia Samia, Ana Nia Njema na Nchi Hii, Mpeni Ushirikiano!.
mkagoma kwa kisingizio hamuwezi kukubali kukaa mezani huku mnene wenu yuko 'pahala salama'!。Tukamuombea msamaha Watanzania tumshukuru Mungu kupata mtu mwenye moyo wa kusamehe. Je, tumuombe asamehe tu bila kuombwa msamaha au akomae naye? 。 Huyu mama alivyo Rahimu na asivyo mtu wa hiyana,akatusikiliza akatenda Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito! mnene wenu sio tuu akaachiwa,bali pia mapene mkavutishwa,mkamwagiwa!,ndipo mkakaa mezani!,mkakubaliana kugawana nusu mkate,mambo yalikuwa yanakwenda safi!

Mara Mbelgiji katua nchini akawavuruga!,sisi watu wa jicho la tatu takaona, tukawatonya kwa kuwauliza Msikie Tundu Lissu Hapa, Anauliza Kama Wenzake Wana Akili Kweli! Maridhiano Ayaita Ujinga. Je, Lissu Bado ni Asset or Sasa ni A Liability?

Sumu ikawaingia,mara Kamanda akatangaza kukosa imani,na kujuta kukaa mezani, sisi watu wa ushauri,tukamshauri Nimemwelewa sana Mbowe, usipoteze imani na Rais Samia. Alivyo kwa Kauli na Matendo hawezi kuwa ni yeye!

Kamanda akaamua Mbelgiji hatufai hivyo kwenye uchaguzi wa ndani mkamletea lile tutusa ,jamaa akasirika ndipo akaamua kumpandia kamanda kule kule juu kileleni na kumpopoa kwa mtindo wa tutabanana hapa hapa kwenye ile vita ya ama zake ama zangu!,ama zao,ama zetu!,mimi kama kawaida yangu kwanza nikawashauri Chadema Japo Lowassa Alikuwa a Liability CCM, Akawa Asset Chadema. Lissu is a Very Bad Liability, but is The Only Asset Chadema Has Kuwangiza Ikulu!. Je... ?

Hapa na mimi naomba kukiri udhaifu wangu,sikuamini kama TAL angeshinda!hivyo nikamshari kukubali matokeo na kukubali kushindwa Pre GE2025 - Baada ya Mbowe kutetea uenyekiti wake, masikini Tundu Lissu, kwishney! Je, atabaki ama atatimka? Lissu Cool down, usiitishe Press kumjibu Mbowe!

Najivunia kuchangia kufanyika uchaguzi wa haki Chadema kupitia onyo hili The Voices From Within: Warning kwa Chadema, Be Very Careful, Msifanye Ujinga Wowote!, Mkileta Tuu Ujinga!, Tarehe 21 Jan. Kutakuwa Hakuna Uchaguzi!. mara ndio pap,kamanda chali!kichaa kachukua chama,kakamata usukani,mwendo ni mzobe mzobe!

NRNE ya kamanda sio kususia uchaguzi bali kushinikiza reforms na kama hakutafanyika reforms basi Chadema haitashiriki!,kamanda mpya katangaza vita na wenye mamlaka,kuwa bila reforms,hakuna uchaguzi!,kitu ambacho ni impossible!,sisi washauri wa bure,tukashauri tena Pre GE2025 - DSM - Pascal Mayalla amshauri Lissu kutumia jukwaa la JamiiForums kusoma maoni ili kuondokana na siasa za harakati na kufanya siasa za mikakati si ndio akatangaza kukinukisha,, wenye mamlaka ndio kama hivyo wameamua kumuhifadhi mahala sana kupisha uchaguzi kwa kumbambikia uhaini !,kwenye hili la uhaini, its a mistake Uhaini My God!. Kuna Uwezekano Anadanganywa na Kadanganyika? I Don't Believe This!. Sitatizwi na Uongo Wao, Natatizwa na The Motives Behind Such Lies!

Ila pia kwenye hili la uhaini, msiwe na shaka wala wasiwasi Pre GE2025 - Wazalendo Wapenda Haki, Msiwe na Wasiwasi, Uhaini ni Matendo na Mipango Mkakati wa Kuutenda, Sio Maneno!, Maneno ni Sedition tuu na Sio Treason! hakuna kesi hapo!。

Kwa vile the real game inachezwa mezani,na matokeo yanapatikania mezani ila yanatangaziwa uwanjani , ile timu ya ushindi,tuliisha maliza kazi siku nyingi!,matokeo tayari tunayo kibindoni,uzuri wa jf ni kuwa wa kwanza kujua,nami mwana jf mwenzenu wa kule sina hiyana nimewajulisha wazi kabisa Pre GE2025 - LGE2024 - Mwana JF, Be The First to Know CCM Ndie The Overall Winner wa Uchaguzi Mkuu wa 2025 Kufuatia Ushindi Serikali za Mitaa。CCM Amekomba Almost Everything!

Hizi kukuru kakara zenu,ni kukuru kakara za mtu anayetafuta,bila kujua kuwa tafuta yote hii ni kujifurahisha tuu,na kuimalizia hiyo ruzuku ya mwisho mwisho!,wenzenu ni watu waliopata, ushindi tayari wanao kibindoni, wahangaikie nini?, ndio maana wametulia tuu,wamejituliza tuli ,wanasubiria tuu siku ya siku ya kipenga kipulizwe wapeleke timu na kuingiza uwanjani kukamilisha tuu zile taratibu za kumtangaza mshindi!

Siku hiyo ni siku ya
Unachukua。。 。
Unaweka。。。
malizia。。 。。

P
 
Hii mada haina tofauti na mada za wajinga akina Tlaah na Lucas, huwezi kuponda chama unachoshabikia, n lazima utakisifia tuu hata kama wanafanya ujinga na unajua hilo bado utasifia tuu mana mnakuwa vipofu wa vyama vyenu.
 
Asali ni juisi,chakula ama tunda?
IMG-20250512-WA0060.jpg
 
Siasa za Bongo sasa zimebebwa na chama kimoja tuu
Mijadala ya kisiasa kwasasa imetawaliwa na chama kimoja tuu
Matukio ya kisiasa Bongo yote kwasasa yote ni ya chama kimoja tuu
Mitandao ya kijamii bongo habari zake za kisiasa zote zimeelemea chama kimoja tuu
Hii sio sawa kabisa.. Hakuna mizania ya haki hapa.. No kama vile vyama vingine ni mahututi ama ni mfu kabisa

Je asili inachukua mkondo wake? Does nature taking its cause!?💪🏿✌🏿
Tulipofika ni A point of no return.. Na hakuna nguvu inayotumika bali mambo yanaenda yenyewe.. Very natural.. Very automatically..!

Ni afadhali kidogo huko kwende kandanda.. Japo Mnyama nyota yake inang'ara zaidi lakini walau mtani jembe anasikika kidogo.. Mtani ni majeruhi lakini si mahututi..
Maneno ya Mungu yanasema hivi

Mathayo 5:13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu
Kuna chama tayari kimeshakuwa chumvi iliyoharibika.. Isiyofaa tena.. Imeshatupwa na inakanyagwa na watu..

Nani anaweza kunionesha walau mada moja mitandaoni iliyotawala walau kwa masaa machache ama iliyoenda viral? Achana na zile mada mbovu zilizokosa ladha na uhalisia za mbubujikwa machozi, tlaa tlaah, yule Yohana mbatizaji kinyonga na wengine

Ni wakati wa mabadiliko na hakuna nguvu ya kibinadamu kuizuia. Kama Mnyama anavyoenda fainali na kuchukua kikombe ndivyo hivyo navyo CHADEMA inavyoenda kuchukua nchi
Simba ilitinga fainali mwaka 1993 wakati mageuzi yanaasisiwa.. Simba inaenda kuchukua ubingwa mwaka huu wakati mageuzi yakiwa kwenye kilele cha ubora na kukubalika

Kuna coincidence ya ajabu hapa na iko kiroho zaidi! Upande wa RED unang'ara na kukubalika kila kona! Lakini upande ule mwingine kumefubaa kumefifia hakuna nuru .. Na kuna kila dalili ya matanga!
Sijui mnanielewa?
Good morning TANGANYIKA,💗View attachment 3332196
"Baada ya chadema kupigwa roba ya mbao, nchi imetulia". Credit: mropokaji wa mbogamboga
 
Hii mada haina tofauti na mada za wajinga akina Tlaah na Lucas, huwezi kuponda chama unachoshabikia, n lazima utakisifia tuu hata kama wanafanya ujinga na unajua hilo bado utasifia tuu mana mnakuwa vipofu wa vyama vyenu.
Sasa wewe unasimama wapi mkuu 'Mbaga Jr'

Hujawahi sifia chama hata siku moja?

Ninakubaliana na unapowataja "wagonjwa wa akili" kama hao uliowaorodhesha hapo juu. Lakini kweli huoni tofauti ya hao na hiki kinachotokea sasa?
Hata ungekuwa unaishi kwenye pango kusikofika mwanga, na ukatokea kufika mahali hapa sasa hivi; kama ni binaadam wa kawaida bila shaka utasisimkwa tu na unachokiona mbele yako.

Sasa tueleze wewe, huko upande wa pili, CCM, ni kipi kinakusisimua wewe na hao hapo uliowataja kwa majina?
 
Huyu wa pili Ndani ya Saa 36 kujitoa mhanga, je underground wako wangapi???View attachment 3332242
Mkuu mzigo ushakuwa mzito kwao na katika kitu kinawapasua kichwa ni namna walivyojiingiza kwenye huu mtego wa kuipigia promo Chadema kwa gharama zao(kulaumia kupo tena mno ,kati ya waasisi wa chama na majuniors) wapo wanaoitwa wakaidi na wapo wanaoomba msamaha kwa upotofu anyway .....

Kimsingi niseme wameshakubaliana kwa pamoja wautue ,shida ni namna tu ya kuutua.

Hiki kinachofanyika hapa nikumtengenezea Mama mazingira tu juu ya namna ya kuutua ila wakati wowote utalisikia tamko ikiwezekana kuanzia leo ,wakati wowote ishara zitaanza kusikika kuhusu hatima ,kaeni kwa kutulia tu
 
Siasa za Bongo sasa zimebebwa na chama kimoja tuu
Mijadala ya kisiasa kwasasa imetawaliwa na chama kimoja tuu
Matukio ya kisiasa Bongo yote kwasasa yote ni ya chama kimoja tuu
Mitandao ya kijamii bongo habari zake za kisiasa zote zimeelemea chama kimoja tuu
Hii sio sawa kabisa.. Hakuna mizania ya haki hapa.. No kama vile vyama vingine ni mahututi ama ni mfu kabisa

Je asili inachukua mkondo wake? Does nature taking its cause!?💪🏿✌🏿
Tulipofika ni A point of no return.. Na hakuna nguvu inayotumika bali mambo yanaenda yenyewe.. Very natural.. Very automatically..!

Ni afadhali kidogo huko kwende kandanda.. Japo Mnyama nyota yake inang'ara zaidi lakini walau mtani jembe anasikika kidogo.. Mtani ni majeruhi lakini si mahututi..
Maneno ya Mungu yanasema hivi

Mathayo 5:13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu
Kuna chama tayari kimeshakuwa chumvi iliyoharibika.. Isiyofaa tena.. Imeshatupwa na inakanyagwa na watu..

Nani anaweza kunionesha walau mada moja mitandaoni iliyotawala walau kwa masaa machache ama iliyoenda viral? Achana na zile mada mbovu zilizokosa ladha na uhalisia za mbubujikwa machozi, tlaa tlaah, yule Yohana mbatizaji kinyonga na wengine

Ni wakati wa mabadiliko na hakuna nguvu ya kibinadamu kuizuia. Kama Mnyama anavyoenda fainali na kuchukua kikombe ndivyo hivyo navyo CHADEMA inavyoenda kuchukua nchi
Simba ilitinga fainali mwaka 1993 wakati mageuzi yanaasisiwa.. Simba inaenda kuchukua ubingwa mwaka huu wakati mageuzi yakiwa kwenye kilele cha ubora na kukubalika

Kuna coincidence ya ajabu hapa na iko kiroho zaidi! Upande wa RED unang'ara na kukubalika kila kona! Lakini upande ule mwingine kumefubaa kumefifia hakuna nuru .. Na kuna kila dalili ya matanga!
Sijui mnanielewa?
Good morning TANGANYIKA,💗View attachment 3332196
Wananchi hawaitaki CCM, tumekichoka na CCM wanajuwa hili na ndiyo maana wanavunja amani iliyopo hapa nchini kwa kuwageuzia kibao Chadema
 
Mkuu mzigo ushakuwa mzito kwao na katika kitu kinawapasua kichwa ni namna walivyojiingiza kwenye huu mtego wa kuipigia promo Chadema kwa gharama zao(kulaumia kupo tena mno ,kati ya waasisi wa chama na majuniors) wapo wanaoitwa wakaidi na wapo wanaoomba msamaha kwa upotofu anyway .....

Kimsingi niseme wameshakubaliana kwa pamoja wautue ,shida ni namna tu ya kuutua.

Hiki kinachofanyika hapa nikumtengenezea Mama mazingira tu juu ya namna ya kuutua ila wakati wowote utalisikia tamko ikiwezekana kuanzia leo ,wakati wowote ishara zitaanza kusikika kuhusu hatima ,kaeni kwa kutulia tu
Kuna Jambo LITATOKEA very soon, naona kama vile Ngoma imevuma Sana sana
 
Back
Top Bottom